Binadamu hatupendani hasa makazini wengine tunafosi tu

Binadamu hatupendani hasa makazini wengine tunafosi tu

Jinsia ya kike kwa kazini honestly ni jipu...japo mie pia wa kike [emoji2]

Sijajua ni damu yangu ya kunguni ama nini lakini maisha yangu ya tangu high school,chuo hata kazini jinsia ya kike ndio imekuwa tatizo zaidi kwangu

Sijui hata nawakosea nini manake kiuhalisia i don't talk much wala sina mazoea sana in real life
Wana inferiority complex....
 
Ila tuseme ukweli tu japo wapo wanokataa

Ni hivi mwanamke ameumbwa kua ni mama wa Nyumbani tu ndo shughuli kubwa anayoiweza hii

Ona sasa watu wanavohangaika makazini kisa hawa Wanawake mnakua mna ubeza Uislamu ila hii ndo nature ya mwanamke ni kukaa nyumbani akalea familia
 
Katika ajira siku zote, ingia muda unaopaswa kuingia, fanya unachopaswa kufanya kwa weledi mkuu bila kufanya ushindani na wengine. Acha utendaji wako uongee wenyewe.

Chochote kisichokuhusu na kisicho na athari yeyote kwako ama ajira yako basi kipuuze kama vile hukioni.

Boss sio rafiki yako na haijalishi kwa kiasi gani anaonyesha kukupenda, ni kwamba anapenda nguvu yako na utendaji wako kwa wakati husika, akikosa matumizi na wewe atakuondosha bila kufikiria mara mbili.

Muda wa kuondoka ukifika fanya kama vile umefukuzwa, ni kwamba toka nduki uende nyumbani. Kazini sio kijiwe cha soga, usiweke mazoea sana.

Wafanyakazi wenzio sio rafiki zako. Ujamaa wenu unaishia pale muda wenu wa kazi unapoishia. Hawapaswi kujua zaidi ya kile chenye mahusiano na kazi yenu.

Kubwa na la muhimu zaidi, hakuna anaekupenda kazini hivyo usitarajie kuwa kuna anaethamini uwepo wako hapo. Kila rafiki wa kazini ni snitch mtarajiwa, ikitokea akapata fursa ya kukusnitch atakuuza bila jitimai ya nafsi.
[emoji2956][emoji2956]
 
Anaecheza na ajira yako basi huyo anacheza na maisha yako, ni adui yako. Deal nae kama adui vile.

All is fair in love and war. Ukipata chance ya kumdhibiti usifikirie mara mbili.

Ila kumbuka kazi inatafutwa ila sio uhai. Ukiona madhara ya chuki zao yanaweza kuathiri uhai wako basi jiepushe na shari kwa kutafute kwingine ndugu.

Afya yako ya akili ni muhimu kuliko ujira wa kazi. Usiruhusu wapumbavu wachache waharibu furaha yako.
Ukiona havivumiliki na huna njia ya kuvibadilisha basi ni wakati wa kubadilisha mazingira yako ndugu.
[emoji2956]
 
Mkiambiwa mjiajiri mnaona watu wajinga ukute umeajiriwa na mtu alie jiajiri. Ukiona kazi huwezi acha sitaki kuamini mtu anaejiheshimu asiefuatilia ya watu anaweza letewa figisu kama mwanaume kuwa na misimamo yako hutayumbishwa. Alafu unaandika kama wanaokuletea figisu wapo jf na kama wapo wataje mwaga nyongo
Hata Rais ameajiriwa....
 
Haiwezekani mtu sili kwako, hunipi msaada wowote, sina ukaribu wowote na wewe hizi chuki, fitina, figisu zinatoka wapi? Uwepo wangu kazini wewe unapungukiwa nini?

Tuheshimiane jinsia ya kike kazini upuuzi tupu. Mwenye masikio na asikie sitaki mazoea

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
Sio makazini tuu sehemu yeyote yenye riziki hatutaki Fulani atuzidi.

Ubinafsi ni hulka ya binadamu so usishangae sana.
 
Hii ni shida

Kuna jamaa yangu kwenye kitengo chake yupo me 1 na ke 5, mwanzo walikuwa me 2 ila mwenzie uzalendo ulimshinda akaachia ngazi.
Hivyo na jamaa nae anafanya michakato ya kusepa.
Maana anakwambia hana amani na kazi kabisa, sababu ya hao mademu.
Sasa wanawake Wana hicho kitobo ni ngumu kushindana nao hasa kama boss ni mwanaume
 
Short tale..
Alisoma shule za seminari kuanzia kidato cha 1 mpk cha 4. Akapata mfadhili wa kumsomesha kidato cha 5&6. Akafaulu vizuri. Akapata scholarship nchi za nje. Akaweza kupata bsc. na masters. Alikua kijana mwenye haiba nzuri, mwerevu, mpole na mcha Mungu. Kiongozi flani (kwa sasa he is late) akaunyaka wasifu wake. Akamrudisha nchini na kumpa kitengo katika balozi za nchi zilizoko kusini.

Alivyoingia pale, wahafidhina wakamuona ni tishio. Aliendelea kumcha Mungu. Behind the scene kuna njama zikasukwa. Akapewa kesi ya human trafficking. Mpk kuja kuprove sio kweli, miaka imepita shwaa. Hakuweza kupata ajira tena. His character was assasinated. Akarudi mbwinde kuishi. Akaamua kulima zake mahindi madongoni. His career slapped him hard.

10 years later:
Paroko mmoja katika shirika la white fathers anatembelea mbwinde. Akasikia story yake. Ashukuriwe Mungu kuna mchongo wa maana na huyu victim ni fit candidate. Akatafutwa, fanyiwa counselling, pigishwa interview, akafaulu. Sasa aanze kujiandaa kwenda kureport nchi za mbali....guess what.......
Akapata ajali ya bodaboda, akiwa na passport yake mkononi. He is no more!![emoji20][emoji20]

Kuna msemo unasema keep your friends close and your enemies closer. Naona hapa ulibackfire kinoma....
MUNGU atutetee katika sehemu zetu za kujipatia kipato. Kuna vita sana ktk kuupata mkate wa kila siku..
Neema ya Kristo ikae nawe...
Dunia hii....
 
Ukitaka mwanadamu yoyote asivuke mipaka, muoneshe kuwa akivuka huo mpaka unao uwezo wa kufanya jambo lolote wakati wowote.

Ukiletewa umbea wa A kutoka kwa B mfuate B ukiwa na A mwambie wazi ulichoambiwa na A. hautaletewa tena umbea na mtu yoyote atakayefahamu ulichokifanya, mwisho wa siku hautakuwa tena sehemu ya umbea na majungu.
 
Back
Top Bottom