Bilcanas ya Mbowe inaondolewa vyombo sasa

Bilcanas ya Mbowe inaondolewa vyombo sasa

Hahahahaha NHC mwenyewe kasema Mbowe ameenda mahakamani.Tukiwa waongo tusisahau tunachokihubiri.Chuki za Ukanda na itikadi ndiyo lugha yetu kwa sasa watanzania


Kwani Mbowe ni Babako?
 
Hii ni siasa tu sijui kama nimjuavyo mbowe bilioni 2 ingemshinda lakini wakaona ili wamwaibishe watoe vitu nnje
Wakauze basi na majengo wabaki nayo mbowe ataanza upya pesa aliyonayo hashindwi kuanza upya
 
Wamefanya vyema kama anadaiwa kodi kweli ila tu wasije kumlipa fidia kama kwenye kesi ya samaki
 
Ndo maana siku zote nasema CHADEMA Chama cha matapeli. Watu wanaohubiri uongo juu ya wengine ya kwao hawa semi. Navyofahamu kwa huyu Bwana mkubwa bado yapo mengi tu ya namjia. Ikiwemo kufikishwa mahakamani kama muhimu uchumi. Muda ndo kila kitu Tusubiri.
Hilo deni ni la mbowe na familia yake halina uhusiano na chadema.Ikiwa vip chadema inaweza kumtimua Mbowe, cdm si mali ya mtu binafsi, aachen kupotosha umma.Ni wangapi wanamadeni ndani ya ccm mbona hajayaegesha kwa ccm.Mbowe atabeba msalaba wake kama yeye na sio CDm
 
Hilo deni ni la mbowe na familia yake halina uhusiano na chadema.Ikiwa vip chadema inaweza kumtimua Mbowe, cdm si mali ya mtu binafsi, aachen kupotosha umma.Ni wangapi wanamadeni ndani ya ccm mbona hajayaegesha kwa ccm.Mbowe atabeba msalaba wake kama yeye na sio CDm

Jana nilikuwa mahali fulani muda wa jioni. Nikaona tbc wakiongelea hili la mgogoro wa nhc na mbowe. Hawakusahau kusema mbowe mwenyekiti wa cdm taifa anadaiwa kodi. Nilihisi ni propaganda ya aina fulani ili kuchafua taswira ya chama.
 
Haya yote yanatufundisha, kabla ya kutoa boriti kwenye jicho la nduguyo toa kibanzi kilichokwako, kila mtu alipe kodi
 
Mkuu hayo maswali yako hayana umuhimu,swali muhimu ni moja tu,je ni kweli anadaiwa? mimi naweza kuwa nawadai watu wawili wewe na mwenzako,nnapokuja kwako kuchukua pesa yangu kama muda tuliokubaliana umefika usije ukaniuliza mbona umekuja muda huu wala usiniulize kwamba mbona mwenzangu yeye humdai,ya mwenzako hayatakusaidia,wewe dumbukia mfukoni nipe changu nikuache huru.

Tofautisha kudaiwa na mtu binafsi na taasisi ya umma. Hapo kila kitu kiko wazi kabisa hata kama Mbowe anadaiwa lakini hayo madai yamesukuwa na utashi wa kisiasa hakuna lingine. Sasa tujiulize, kama hii mbinu ya kunyamazisha kila anayekosoa kwa kuwa anadaiwa nchi yetu itakuwa kwenye hali gani? Tunajua kabisa wanachama wa ccm wengi wanamadeni ya taasisi za umma na mkono hauwagusi kisa hawakosoi chochote kwenye serekali. Hiki kinachoendelea kitaishia kujenga nidhamu ya woga kama enzi za Nyerere, hatimaye wananchi wakaishia kuvaa viraka. Hakuna anayepinga Mbowe kudaiwa lakini isiwe yeye peke yake wakati waidawa ni wengi na sababu halisi za kudai sio uzalendo bali ni utashi wa kisiasa.
 
Hueleweki mkuu, inamaana kuna watu wapo immuned kulipa kodi??

Wewe huelewi hata kinachoongelwa. Wanazungumzia malipo ya pango siyo kodi!!! Usichangie maana huelewi hata kinachojadiliwa, endelea kusoma ili uelimike taratibu.
 
Tit for tat...!!

Mbowe sbb ya UKUTA, si anaandamanisha watu... kumbe serikali inamdai, na anaipinga serikali... sasa mm kama unanipinga, na nakudai, hata kama ni NHC but NHC ni serikali, lazima nita react...!!

Mbowe aachane na UKUTA.. la sivyo, ajenge BILLICANAS kwingine..!!
Fact
 
Back
Top Bottom