Bila kufanya haya, tusahau suala la kuondokana na Mgao wa Umeme

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Kuna watu wanaamini kabisa kuwa Bwawa la Umeme la Rufiji likianza kazi basi suala la Mgao wa umeme litakuwa historia kwenye nchi hii.

Kwa namna ninavyosoma taarifa mbalimbali za kiutafiti zinazohusu masuala ya Mazingira napenda kuwaambia hawa watu wakiwemo viongozi wetu kuwa inawezekana wakawa sahihi kwa muda fulani ila kwa muda mrefu hawatakuwa sahihi

Kwa hali ya mabadiliko ya hali ya hewa ilivyo inasemwa kuwa huko mbeleni suala la ukame litakuwa jambo la kawaida sana duniani na inawezekana hata uzalishaji wa chakula ukapungua sana.

Kwa haya ni sahihi kusema kuwa hata Bwawa la Nyerere inawezekana lisiwe efficient kwa miaka mingi ijayo kutokana na changamoto hizi.

Kwa upande mwingine kuna vyanzo ya umeme vinavyoonekana kuwa vya uhakika zaidi katika miaka mingi ijayo. Vyanzo hivyo ni pamoja na Nyuklia na Jua ambavyo kwa bahati nzuri sana vyote kwa hapa Tanzania tunavyo.

Ushauri wangu.
1. Kuna teknolojia mpya salama zaidi ya kutengeneza plant ndogo za nyuklia. Serikali ialike wataalam kutoka nchi za Ujerumani au Scandinavia wajenge hata plant moja ya namna hiyo kwenye moja ya mikoa yenye bahari/ maziwa hapa Tanzania. Tukipata megawat hata 10,000 au 20,000 sio mbaya. Uzuri madini ya uranium tunayo kinachotakiwa ni teknolojia tu.

2. Kuna mikoa/ sehemu hapa nchini ambayo Jua linawaka kwa uhakika kwa miezi si chini ya 10 au 11. Serikali iwekeze haraka uzalishaji wa Umeme Jua kwenye mikoa hii hata megawat 3000 - 5000

Inawezekana watu wakasema tuna gesi ila kiuhalisia gesi tuliyonayo ni ya matumizi ya miaka 30- 50 kama sikosei hivyo inawezekana huko mbeleni nayo ikaisha.


Naomba kuwasilisha.
 
IMG-20231127-WA0087.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suluhisho kwa sasa ni umeme wa gesi tu
Umeme wa gesi sawa ila nao sio wa uhakika kwa miaka mingi ijayo maana reserve ya gesi nayo siyo ya milele.

Niliwahi kusoma sehemu kuwa reserve yetu kwa matumizi ya LNG ni miaka 30 sasa it seems baada ya miaka 30 tunaweza kuingia kwenye matatizo ya kutafuta nishati nyingine mbadala
 
Hii ni hoja ya msingi sana,maeneo kama Singida na Dodoma jua linawaka mwaka mzima,lakini tunawaza Nishati za kale ambazo hazina uhakika kwa siku za usoni.
Ila kwenye Nuclear plants hapo Mzee namna ya kutunza bila kuathiri binadamau,maana watumishi wa Shirika letu kwa uzembe hawajambo.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
Siyo lazima wafanye Tanesco tunaweza fanya kwa mfumo wa PPP kukawa na kampuni binafsi ambayo nayo ina share na wana manage kwa pamoja
 
Kuna watu wanaamini kabisa kuwa Bwawa la Umeme la Rufiji likianza kazi basi suala la Mgao wa umeme litakuwa historia kwenye nchi hii.

Kwa namna ninavyosoma taarifa mbalimbali za kiutafiti zinazohusu masuala ya Mazingira napenda kuwaambia hawa watu wakiwemo viongozi wetu kuwa inawezekana wakawa sahihi kwa muda fulani ila kwa muda mrefu hawatakuwa sahihi

Kwa hali ya mabadiliko ya hali ya hewa ilivyo inasemwa kuwa huko mbeleni suala la ukame litakuwa jambo la kawaida sana duniani na inawezekana hata uzalishaji wa chakula ukapungua sana.
Hivi unajua katika suala la Ukame wala UMEME hautakuwa kigezo, Kabla haujakosa taa za kuangalia utakuwa umekufa kwa njaa..., Kumbuka hayo maji ya kutoka kwenye Bwawa sio kwamba yakipita kwenye Bwawa yanayeyuka hapana ndio hayo hayo yanaendelea kwenye safari yake (kwahio kuyatumia kuzalisha umeme ni efficiency tu ya kawaida) kwahio cha maana ni kutokuharibu vyanzo vya maji ili tusife kwa njaa na madhara ya ukame
Kwa haya ni sahihi kusema kuwa hata Bwawa la Nyerere inawezekana lisiwe efficient kwa miaka mingi ijayo kutokana na changamoto hizi.
Halitakuwa efficient kutokana na kwamba tuna watawala na sio viongozi..., tuna madalali na sio wazalendo wala thinkers, tatizo ni waliopo madarakani
Kwa upande mwingine kuna vyanzo ya umeme vinavyoonekana kuwa vya uhakika zaidi katika miaka mingi ijayo. Vyanzo hivyo ni pamoja na Nyuklia na Jua ambavyo kwa bahati nzuri sana vyote kwa hapa Tanzania tunavyo.
Hivi unajua bottleneck ya Jua, upepo na all other so called green energies ni nini ? Tatizo ni storage ya hio nishati jua likiwaka mchana inabidi ulitunze kwenye battery ili usiku utumie..., na ndio maana hapa nilishasema energy mix is way forward lakini kiunganiko au moyo wa hio energy mix ni Bwawa la Nyerere....

Ushauri wangu.
1. Kuna teknolojia mpya salama zaidi ya kutengeneza plant ndogo za nyuklia. Serikali ialike wataalam kutoka nchi za Ujerumani au Scandinavia wajenge hata plant moja ya namna hiyo kwenye moja ya mikoa yenye bahari/ maziwa hapa Tanzania. Tukipata megawat hata 10,000 au 20,000 sio mbaya. Uzuri madini ya uranium tunayo kinachotakiwa ni teknolojia tu.
Kwa nchi yeney vyanzo lukuki vingine na upuuzi na kutokujali na uzembe hio ni welcoming a disaster..., nuclear ina hatari yake na jinsi ya ku-maintain yale mabaki ni tatizo tunaweza kujikuta tunajimaliza umeongelea kubadilika kwa mazingira je unajuaje hayo matetemeko au disaster kama za Tsunami zikija itakuwaje (uliza Japan pamoja na kukosa kwake vyanzo vya nishati kuna kipindi ilibidi ifunge baadhi ya mitambo yake) it's a risky endeavor ambayo kwa nchi yenye njia ambazo ni safe na efficient zaidi kutumia hio njia
2. Kuna mikoa/ sehemu hapa nchini ambayo Jua linawaka kwa uhakika kwa miezi si chini ya 10 au 11. Serikali iwekeze haraka uzalishaji wa Umeme Jua kwenye mikoa hii hata megawat 3000 - 5000
Ili zikishapatikana ziwekwe wapi tununue batteries ili tuweze kuhifadhi huo umeme (another costly issue) ukisema zipelekwe kwenye grid directly sawa wakati wa mchana je usiku ? Ni kitu gani kitafanya hio balancing act ? Ila there is a way ambayo nimesuggest hapo juu kwa Bwawa la Nyerere kutumika kama Battery
Inawezekana watu wakasema tuna gesi ila kiuhalisia gesi tuliyonayo ni ya matumizi ya miaka 30- 50 kama sikosei hivyo inawezekana huko mbeleni nayo ikaisha.


Naomba kuwasilisha.
Energy mix hakuna ambacho hakiishi hata jua likiwaka linahitaji battery (kwa mfano wako hapo juu) kwahio sio reliable, upepo halikadhalika.., Nuclear nayo si ni renewable (By the way gesi asilia ukiamua kwenda mwendo wa Biogas basi haiwezi kuisha - Lakini sio efficient (kutumia gesi Biogas kuchemsha maji kwenye boilers kuzungusha motors).....
 
Hivi unajua katika suala la Ukame wala UMEME hautakuwa kigezo, Kabla haujakosa taa za kuangalia utakuwa umekufa kwa sha maji kwenye boilers kuzungusha motors).....
Sijakuelewa ndugu

Do you mean umeme wa Solar unatumika mchana tu usiku hautumiki?

Nchi kubwa za Uarabuni mbona zinatumia Solar as source of Energy na usiku umeme haukatiki?

Ninaposema tutumie Solar namaanisha ni ujumla wote unaofanya umeme wa Solar uwe efficient sio panels tu.
 
Sijakuelewa ndugu

Do you mean umeme wa Solar unatumika mchana tu usiku hautumiki?
Umeme kwa ujumla wake unatumika pale unapozalishwa kwahio sababu usiku hakuna uzalishaji inabidi umeme utunzwe sehemu fulani (batteries) na mpaka dakika huu duniani tatizo kubwa la solar na upepo haujafanya stride kubwa zaidi sababu bottleneck ni batteries...

Ndio mchana unaweza ukatengeneza na kuweka directly kwenye grid lakini ukiingia kwenye grid ni either utumike au utunzwe na kwenye kutunza ndio narudi palepale..., Kwenye HEP ni rahisi unaweza ukazima some generators au vyovyote vile its easier to scale kwenye kutumia boilers unaweza kuzima baadhi ya boilers kwenye solar inabidi uweke hio DC kwenye Battery au as my suggestion HEP ndio iwe Battery....
Nchi kubwa za Uarabuni mbona zinatumia Solar as source of Energy na usiku umeme haukatiki?
Zinatumia as part of energy mix tena hizo nchi zina mafuta ya kutupa hence kwao kutumia hata fuel kwao ni efficient siku tutakapopata efficiently batteries kuna jua la kutosha jangwani kuwasha umeme wa dunia nzima (ila ndio hivyo efficient storage is still a problem)
Ninaposema tutumie Solar namaanisha ni ujumla wote unaofanya umeme wa Solar uwe efficient sio panels tu.
Narudi tena storage is still an issue unless utumike ushauri niliosema Bwawa ndio liwe Battery
 
Sijakuelewa ndugu

Do you mean umeme wa Solar unatumika mchana tu usiku hautumiki?

Nchi kubwa za Uarabuni mbona zinatumia Solar as source of Energy na usiku umeme haukatiki?

Ninaposema tutumie Solar namaanisha ni ujumla wote unaofanya umeme wa Solar uwe efficient sio panels tu.
Nimesoma sehemu SaudiArabia na Katar wanajenga madude makubwa ya umeme wa solar baada ya shirika la mazingira la Dunia kukomalia uchafuzi wa mazingira kutokana na matumizi ya mitambo inayotumia diesel au petrol , wameiona isiwe shida wameelekea HUKO,hata SISI kuwekeza KWENYE umeme wa jua tunaweza shida ni viongozi tuliokuwa nao wanafikiri vitu kwa udogo mno,
 
Nimesoma sehemu SaudiArabia na Katar wanajenga madude makubwa ya umeme wa solar baada ya shirika la mazingira la Dunia kukomalia uchafuzi wa mazingira kutokana na matumizi ya mitambo inayotumia diesel au petrol , wameiona isiwe shida wameelekea HUKO,hata SISI kuwekeza KWENYE umeme wa jua tunaweza shida ni viongozi tuliokuwa nao wanafikiri vitu kwa udogo mno,
Kuna mpango ulikuwepo Kwamba umeme wa solar kutumika Jangwani kwamba uweze kutumika dunia nzima; kampuni nyingi ziliwekeza kwenye mahekari na mahekari ila kama nilivyosema storage bado ndio tatizo unatunza vipi umeme kwa matumizi ya offpeak (battery efficiency bado haijawa at par ingawa bado wanaumiza vichwa kutumia vitu kama thermal storage, hydrogen gas, Mechanical Storage n.k.) ila bado efficiency ni ndogo..., hivyo mkuu kutumika kwa solar kwa matumizi ya umeme bila advance in battery storage its still a Pipe Dream...

Ingawa narudia tena kwa Bongo kufanikisha hili lazima Bwawa litumike kama storage that is the only cheapest and efficient way I can see in the next foreseeable future (bila hivyo tutawekeza ili watu wapige pesa za miradi)
 
Kuna mpango ulikuwepo Kwamba umeme wa solar kutumika Jangwani kwamba uweze kutumika dunia nzima; kampuni nyingi ziliwekeza kwenye mahekari na mahekari ila kama nilivyosema storage bado ndio tatizo unatunza vipi umeme kwa matumizi ya offpeak (battery efficiency bado haijawa at par ingawa bado wanaumiza vichwa kutumia vitu kama thermal storage, hydrogen gas, Mechanical Storage n.k.) ila bado efficiency ni ndogo..., hivyo mkuu kutumika kwa solar kwa matumizi ya umeme bila advance in battery storage its still a Pipe Dream...

Ingawa narudia tena kwa Bongo kufanikisha hili lazima Bwawa litumike kama storage that is the only cheapest and efficient way I can see in the next foreseeable future (bila hivyo tutawekeza ili watu wapige pesa za miradi)
Bado sijapata hoja yako vizuri ndugu ingawa unaonekana unayo.

Hiyo storage concern issue yake ni nini hasa? Umeme wa Solar si unazalishwa kila siku?

Hizo nchi za Uarabuni mbona hatusikii iyo unayosema storage concern?
 
Kuna watu wanaamini kabisa kuwa Bwawa la Umeme la Rufiji likianza kazi basi suala la Mgao wa umeme litakuwa historia kwenye nchi hii.

Kwa namna ninavyosoma taarifa mbalimbali za kiutafiti zinazohusu masuala ya Mazingira napenda kuwaambia hawa wat
Pamoja na mawazo yako mazuri, ipo changamoto kubwa ya fikra za kidalali ambazo kwazo uwezo wa ndani wa kufanya mambo ya kimaendeleo.

Tofauti ya kimaendeleo duniani husababishwa na nchi masikini kutegemea teknolojia kutoka nchi tajiri ambapo huuziwa miradi kwa gharama za juu zaidi hata 1000℅ ya uhalisi.

Hata kwenye nyuklia na jua, mambo yatakuwa hayo hayo kama fikra hazijabadika kwa raia na viongozi kwa ujumla.

Tukiamua kuiga wachina ni rahisi sana. Waruhusiwe wawekeze miaka 10, serikali iandae vijana wa Ku copy na Ku paste, baada ya hapo unawasaidia wazawa kufanya shughuli zile zile wakishindana na wachina sokoni.
Kitakachofuata ni kuwabana wachina kwa kodi na urasimu mwingine mpaka wakimbie wenyewe.
 
Pamoja na mawazo yako mazuri, ipo changamoto kubwa ya fikra za kidalali ambazo kwazo uwezo wa ndani wa kufanya mambo ya kimaendeleo.
Tofauti ya kimaendeleo duniani husababishwa na nchi masikini kutegemea teknolojia kutoka nchi tajiri ambapo huuziwa miradi kwa gharama za juu zaidi hata 1000℅ ya uhalisi.
Hata kwenye nyuklia na jua, mambo yatakuwa hayo hayo kama fikra hazijabadika kwa raia na viongozi kwa ujumla.
Tukiamua kuiga wachina ni rahisi sana. Waruhusiwe wawekeze miaka 10, serikali iandae vijana wa Ku copy na Ku paste, baada ya hapo unawasaidia wazawa kufanya shughuli zile zile wakishindana na wachina sokoni.
Kitakachofuata ni kuwabana wachina kwa kodi na urasimu mwingine mpaka wakimbie wenyewe.
Mawazo mazuri sana
 
Rwanda wameanza kuwekeza umeme wa nuclear
Nimeangalia documentary ya DW kama wiki mbili/ moja iliyopita wameelezea vizuri sana kuwepo wa teknolojia mpya ya nyuklia ambayo sio threat kwa kiwango kikubwa kwa mazingira na usalama ambayo imezifanya baadhi ya nchi za ulaya kuamua kurudi upya kwenye umeme wa nyuklia ambao ndo the most reliable.

Sasa sisi tuna uranium kwa nini tushindwe kuvutia teknolojia ya namna hii? Ni maamuzi tu
 
Back
Top Bottom