Bila kuchelewa, Serikali ya Tanzania ijipambanue kupata uchaguzi huru na haki ili kuondoa upotoshaji

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Kwanza naomba Mods, uzi huu usiunganishwe na nyengine.

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na kauli mbali mbali kuhusu Madai ya tume huru ya uchaguzi Tanzania.

Si vyama vya upinzani tu lakini hata wadau wa maendeleo na demokrasia wamesikika wakihimiza kwa serikali kuleta tume huru ya uchaguzi KABLA YA KUFANYIKA UCHAGUZI

Aidha serikali imeahidi kufanya uchaguzi wa uwazi, huru na haki kupitia kauli za Mh Rais alipozungumza na Mabalozi wakati wa chakula cha pamoja kuukaribisha mwaka mpya, Waziri Mkuu Bungeni, waziri wa mambo ya nje kule UN na waziri wa mambo ya Ndani alipozungumza na Kaimu Balozi wa Marekani hivi karibuni.

Katikati ya maelezo hayo kutoka kwa wakubwa hao, pia alisikika Katibu Mkuu wa CCM ndugu Bashiru akieleza maelezo ambayo yana ukakasi mkubwa . Hata waziri mkuu naye ufafanuzi wake una ukakasi. Kusema tume iliyopo ni huru huko ni kujitia pamba za sikio.

Suali linakuja hii ahadi ya Serikali kufanya uchaguzi huru na haki ni kwa tume iliyopo au kuna nini?
Kwa mtazamo wangu ikiwa hakukufanywa marekebisho yoyote katika muundo wa Tume na mfumo wake wa ufanyaji kazi basi hakuna Tume huru na katu uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki.

CCM na Sereikali yake waTAMBUWE KWAMBA WADAU WANADAI TUME HURU KWA SABABU HII ILIYOPO HAIKO HURU.

Kushupalia vifungu vya sheria na kunukuu kwa ustadi kuhusu uhuru wa tume iliyopo hakusaidii kitu ikiwa mfumo wa uteuzi na uwajibikaji uko kwa mtu hilo ni tatizo

Kukosekana kwa Tume kuhojiwa na kuwajibishwa mahakamani hilo nalo ni tatizo.

MWISHO

Serikali kushindwa kutoa ufafanuzi wa Uchaguzi huru na haki NA HATUA ZIPI ITACHUKUWA ILI WADAU WAWEZE KUPIMA KAMA KWELI KUNA NIA HIYO ni kama inavizia na kuweka hadaa kwa wadaU HAO. hAPA KUNA KILA ISHARA YA ULAGHAI.

Uchahguzi huru na haki ni Process, huwezi kusubiri hatua ya mwisho ndio usaeme uchaguzi ulikuwa huru wakati hatua muhimu zote hazina uwazi na ushirikishwaji.

Serikali itoe ufafanuzi wa wazi inakusdudia kufanya nini. Huu ni mwezi wa Pili mwishoni kuelekea wa tatu, itakuwa imebaki miezi saba tu na hatua nyengine muhimu za uchaguzi zinaendelea.

Kwa ufupi kuna ahadi ya Uchaguzi huru na haki kwenye mazingira yasiyoruhusu.

Serikali itoe ratiba ya hatua za kufanya uchaguzi huru na haki na ufafanuzi unaojitosheleza.

Bila kufanywa marekebisho ya muundo na mfumo huko ni kulaghai watu.

Kinachotakiwa ni Tume Huru ya Uchaguzi ili kupata uchaguzi huru na haki na wala sio ahadi ya uchaguzi huru na haki katika mfumo usioruhusu haki kupatikana.

Ni hayo tu

Kishada.
 
Kwanza kabisa ungetuambia Tume hii ya bara inatatizo gani mpaka useme sio huru?
 
Kwanza kabisa ungetuambia Tume hii ya bara inatatizo gani mpaka useme sio huru?
Mkuu pamoja na kufafanuliwa kote huko na mto hoja kuhusu kasoro iliyopo ktk mfumo wa uteuzi wa tume na uwajibikaji wake ambao una shinikizo kutoka ktk mamlaka yake ya uteuzi, kukosekana kwa kuhojiwa kwake wala kuwajibishwa mahakamani, bado hujaona mantiki ya wazi kabisa yenye kuhusiana na tatizo la tume ya sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu pamoja na kufafanuliwa kote huko na mto hoja kuhusu kasoro iliyopo ktk mfumo wa uteuzi wa tume na uwajibikaji wake ambao una shinikizo kutoka ktk mamlaka yake ya uteuzi, kukosekana kwa kuhojiwa kwake wala kuwajibishwa mahakamani, bado hujaona mantiki ya wazi kabisa yenye kuhusiana na tatizo la tume ya sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
We umejuaje inaongozwa na mamlaka juu wakati wana sheria yao inayowaongoza kuendesha uchaguzi
 
Kwanza kabisa ungetuambia Tume hii ya bara inatatizo gani mpaka useme sio huru?
Soma hayo maelezo yatakusaidia.

Kwa ufupi Mamlaka ya utuzi wa mkurugenzi na mwenyekiti wa Tume, Wakurugenzi wa halmaqshauri na wengine ambao wanahusika kwenye uchaguzi. hufanywa na Mwenyekiti wa chama ambae ni rais.

Pili matokeo ya Urais kutopingwa na kuhojiwa mahakamani.
 
Naziona dalili za CCM kuwahadaa mabeberu na ndugu zao Watanzania. Bila kubadilishwa sheria na mfumo wake hakuna Uchaguzi huru na haki hapa.
 
Soma hayo maelezo yatakusaidia.

Kwa ufupi Mamlaka ya utuzi wa mkurugenzi na mwenyekiti wa Tume, Wakurugenzi wa halmaqshauri na wengine ambao wanahusika kwenye uchaguzi. hufanywa na Mwenyekiti wa chama ambae ni rais.

Pili matokeo ya Urais kutopingwa na kuhojiwa mahakamani.
Shida yenu si Tume huru shida yenu mnataka tume huru kwa maslahi ya chadema na si kwa siasa kiujumla
 
Haki na uhuru wa uchaguzi utokane na mfumo wenyewe na sio utashi hewa wa mtu. Mfumo uliopo hauko huru kamwe uchaguzi hauwezi kuwa huru.
 
Shida yenu si Tume huru shida yenu mnataka tume huru kwa maslahi ya chadema na si kwa siasa kiujumla
Shida ni tume huru, Na uhuru , haki na uwazi hautaki kumwilikwa tochi, lazima uonekane wazi wazi kwenye process. Unashangaa wakurugenzi wa halmashauri na manispaa waliojificha na kukataa kuchukua fomu za ugombea za wapinzani wapo hadi leo wanalindwa na mamlaka za uteuzi, hawakuwajibishwa hadi leo. Hata hili hulioni au ndio mapenzi niuwe?
 
Kwanza kabisa ungetuambia Tume hii ya bara inatatizo gani mpaka useme sio huru?
Alisikika mtu mmoja mchana kweupe akihutubia maelfu, "eti Mkurugenzi Mimi nikupe nyumba na kukupa garinzuri harafu umtangaze mpinzani kuwa ameshinda" baada ya hapo hao wasimamizi "huru" hukimbia ofisi siku "mpinzani" anapotaka either kuchukua au kurudisha fomu!

Nadhani kwa murtadha huu bado tuu unaamini tume iliyopo ni huru! Nadhani wenzie walikuwa wanauma na kupuliza yeye Mwenye akili kaamua kuuma kabisa mchana kweupe!!

Kaleta matatizo kwa vibaka wa kura maana dunia itakaa attention kujua je hao "wakurugenzi" watafanya nini? Then "tunaenda Zimbabwe" Hata sisi tusiohusika ndipo kitakuwa kilio na kusaga meno!!
 
Alisikika mtu mmoja mchana kweupe akihutubia maelfu, "eti Mkurugenzi Mimi nikupe nyumba na kukupa garinzuri harafu umtangaze mpinzani kuwa ameshinda" baada ya hapo hao wasimamizi "huru" hukimbia ofisi siku "mpinzani" anapotaka either kuchukua au kurudisha fomu!

Nadhani kwa murtadha huu bado tuu unaamini tume iliyopo ni huru! Nadhani wenzie walikuwa wanauma na kupuliza yeye Mwenye akili kaamua kuuma kabisa mchana kweupe!!

Kaleta matatizo kwa vibaka wa kura maana dunia itakaa attention kujua je hao "wakurugenzi" watafanya nini? Then "tunaenda Zimbabwe" Hata sisi tusiohusika ndipo kitakuwa kilio na kusaga meno!!
Kwahiyo shida yako sio ufanisi wa Time ya uchaguzi ila tatizo lako ni maneno ya Raisi
 
Upotoshaji mwingi kuhusu tume huru ya uchaguzi unafanywa na viongozi wa CCM. Wanadhani watanzania hawaelewi kinachoendelea.
 
Vapur zingine bwana zinakera
Kwanza naomba Mods, uzi huu usiunganishwe na nyengine.

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na kauli mbali mbali kuhusu Madai ya tume huru ya uchaguzi Tanzania.

Si vyama vya upinzani tu lakini hata wadau wa maendeleo na demokrasia wamesikika wakihimiza kwa serikali kuleta tume huru ya uchaguzi KABLA YA KUFANYIKA UCHAGUZI

Aidha serikali imeahidi kufanya uchaguzi wa uwazi, huru na haki kupitia kauli za Mh Rais alipozungumza na Mabalozi wakati wa chakula cha pamoja kuukaribisha mwaka mpya, Waziri Mkuu Bungeni, waziri wa mambo ya nje kule UN na waziri wa mambo ya Ndani alipozungumza na Kaimu Balozi wa Marekani hivi karibuni.

Katikati ya maelezo hayo kutoka kwa wakubwa hao, pia alisikika Katibu Mkuu wa CCM ndugu Bashiru akieleza maelezo ambayo yana ukakasi mkubwa . Hata waziri mkuu naye ufafanuzi wake una ukakasi. Kusema tume iliyopo ni huru huko ni kujitia pamba za sikio.

Suali linakuja hii ahadi ya Serikali kufanya uchaguzi huru na haki ni kwa tume iliyopo au kuna nini?
Kwa mtazamo wangu ikiwa hakukufanywa marekebisho yoyote katika muundo wa Tume na mfumo wake wa ufanyaji kazi basi hakuna Tume huru na katu uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki.

CCM na Sereikali yake waTAMBUWE KWAMBA WADAU WANADAI TUME HURU KWA SABABU HII ILIYOPO HAIKO HURU.

Kushupalia vifungu vya sheria na kunukuu kwa ustadi kuhusu uhuru wa tume iliyopo hakusaidii kitu ikiwa mfumo wa uteuzi na uwajibikaji uko kwa mtu hilo ni tatizo

Kukosekana kwa Tume kuhojiwa na kuwajibishwa mahakamani hilo nalo ni tatizo.

MWISHO

Serikali kushindwa kutoa ufafanuzi wa Uchaguzi huru na haki NA HATUA ZIPI ITACHUKUWA ILI WADAU WAWEZE KUPIMA KAMA KWELI KUNA NIA HIYO ni kama inavizia na kuweka hadaa kwa wadaU HAO. hAPA KUNA KILA ISHARA YA ULAGHAI.

Uchahguzi huru na haki ni Process, huwezi kusubiri hatua ya mwisho ndio usaeme uchaguzi ulikuwa huru wakati hatua muhimu zote hazina uwazi na ushirikishwaji.

Serikali itoe ufafanuzi wa wazi inakusdudia kufanya nini. Huu ni mwezi wa Pili mwishoni kuelekea wa tatu, itakuwa imebaki miezi saba tu na hatua nyengine muhimu za uchaguzi zinaendelea.

Kwa ufupi kuna ahadi ya Uchaguzi huru na haki kwenye mazingira yasiyoruhusu.

Serikali itoe ratiba ya hatua za kufanya uchaguzi huru na haki na ufafanuzi unaojitosheleza.

Bila kufanywa marekebisho ya muundo na mfumo huko ni kulaghai watu.

Kinachotakiwa ni Tume Huru ya Uchaguzi ili kupata uchaguzi huru na haki na wala sio ahadi ya uchaguzi huru na haki katika mfumo usioruhusu haki kupatikana.

Ni hayo tu

Kishada.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom