Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 26,065
- 23,948
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema jina la Tume ya Uchaguzi (NEC) litabadilika Ijumaa Aprili 12, 2024 na kuwa Tume Huru ya Uchaguzi.
Katika taarifa iliyotolewa leo katika mitandao ya kijamii ya ofisi hiyo imesema:
“Tunapenda kuvitaarifu vyombo vyote vya habari kwamba, kufuatia tangazo la Serikali namba 225 la Machi 29, 2024 Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi namba 2 ya mwaka 2024, itaanza kutumika rasmi Aprili 12, 2024.
“Hivyo, kuanzia Aprili 12, 2024 jina la Tume litabadilika na litakuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi au kwa kiingereza Independent National Electoral Commission,”imesema taarifa hiyo.
Chanzo: mwananchi digital