Bila haki, uhuru, demokrasia ya kweli nje na ndani ya bunge, kukosekana uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa raia kukosoa, Tanzania itabaki maskini

Wadiz

JF-Expert Member
Nov 10, 2022
5,411
11,061
Msingi wa maendeleo ya binadamu ni haki, uhuru na demokrasia, kuna mahali serikali ya Tanzania hii ya CCM haijitambui na Dunia haina macho dhidi ya Tanzania, pengine ndiomana Magufuli ilibidi afe (mnisamehe ntaeleza), dhamira ya Magufuli kuua upinzani ilikuwa ya kitoto na ya kipumbavu, Magufuli hakuwa mwelevu wa mambo msingi ya ubinadamu kwa mapana, Magufuli alikosa kifua Cha kiume, alikosa sifa za ustahimilivu wa kimungu.

Magufuli didn't know that diversity is healthy so is the difference in opinions. I wish he had guts to listen, digest, pick or ignore and move forward. He was a president in solitary confinement

Ukiua demokrasia, haki na uhuru, unajikosea haki ya kukosolewa ambayo ni chachu ya kujirekebisha kama chachu ya maendeleo, hulka ya ubinafsi ya mwanadamu ni sharti idhibitiwe.

Vyombo vya habari vinapaswa kuwa huru kukosoa pamoja na raia, vyombo vya habari husemra wananchi wakaa kimya walio wengi.

Ni muhimu kuwa vyombo vya habari credible visivyofungamana na yeyote hivyo ni wajibu wa serikali kuweka mazingira hayo.

Wabunge wa COVID-19 na yule wa nkasi, Kwa namna yoyote Serikali makini ingewapa Kambi rasmi ya upinzani bila kujali akidi yao, hekima za kidemokrasia ni zaidi ya akili za kawaida.

Taifa la Tanzania bila haki, uhuru, na demokrasia hasa kwanzia na state organs, Kisha ukaenda kwenye sekta ya habari, Raia wake, uwajibikaji na vitendo katika tafsiri ya cheo ni dhamana basi umaskini itakuwa ni sehemu ya kurasa za maisha yote ya Watanzania.

Akili ni nywele sio sahihi akili ni kichwa na kichwa ni uwakilisho wa Mungu kwenye maisha ya mwanadamu.

Mwenye macho ataona umuhimu wa kuwa na katiba inayokubalika na kuwa na nchi ambayo, viongozi, serikali na wananchi wake wanaishi ukatiba katika maisha yao kwenye nyanja zote.

Mungu awape hekima, busara na ustahimilivu na utulivu katika usomaji wenu wa ujumbe huu.

Asanteni 🙏🙏🙏

Wadiz
 
Back
Top Bottom