fered mbataa
JF-Expert Member
- Feb 19, 2012
- 240
- 35
Mkuu kwanza nikupongeze kwa kutobweteka na kazi za kuajiliwa pekee. "You are on the right track" kuendelea kufanya kazi huku ukitafutafuta kipato cha nje.
Hati ya kimila kwenye baadhi ya benki inafanya kazi lakini hakikisha kijiji husika kimeshajiliwa.
Kuhusu kiasi cha kuanzisha biashara hii, sina data lakini jaribu kupita pita kwenye maduka yanayouza mashine kama hizi upate bei. Pia usisahau kujaribu kuomba ushauri kwa wazoefu wa biashara hii ili wakwambie kipi kinafaa - e.g Printer gani nzuri, za kudumu lakini za bei poa. Wapi kuna mafundi wazuri wa kutengeneza mashine zikisumbua, etc.
Mbali na hilo nikuongezee ushauri wa bure tu:
1. Hakikisha hii biashara katika eneo unapoiweka kuna mzunguko mzuri zaidi wa biashara ya aina hii mfano karibu au ndani ya vyuo ni sehemu nzuri zaidi kuliko maeneo ya viwanda.
2. Tunza hesabu zako vema utakapokuwa umeanzisha biashara yako. Kila senti inahesabika. e.g kuuza karatasi moja au kutoa copy moja sh. 50 ni kidogo lakini ni kubwa pia maana (ndogo) x (idadi kubwa) x (muda) = Utajiri. Hivyo zingatia na kuheshimu kila mteja anayepiga hodi kwako, kila akiingia amini kuwa ni biashara mpya anakuongezea.
3. Zunguka (unguza sori) ukijalibu kunadi biashara yako na kueleza wazi kwa marafiki, mashule, maofisi, etc ili biashara yako ijulikane.
Kumbuka:
wakati kuna watu wengi sana wanatafuta mahali pa kuuza huduma na bidhaa zao, wapo watu wengi zaidi wasiojua pa kupata huduma au bidhaa hizo
Above all: Mtegemee Mungu katika kila kitu, inalipa.
Nashukuru kwa ushauri wako wa thamani sana kwangu. Mambo mengine nilipanga kuyafanya ulisoyasema mfano pita pita mashuleni na vyuoni kuelezea ile uniqueness ya biashara yangu na pia namtegemea MUNGU. Asante