Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,018
- 20,489
Mganga/kigagula wa ccm aliwatapeli kuwa Mkweree ndio chaguo la watz! Inawezekana na nao walimdhurumu akageuza ungo!!!
Mwaka 1995 Kikwete aliposhinda raundi ya kwanza Nyerere alisema 'bado mdogo' wakati umri wa kikwete wakati huo ni mkubwa kuliko umri wa Nyerere wakati anaukwaa urais 1961. Watu hawakumwelewa Nyerere kuwa alimaanisha Kikwete hawezi urais kistaarabu. Leo ndo tunajua ukweli kile alichokimaanisha Nyerere kuwa ni Kikwete hawezi kuwa Rais tatizo halikuwa umri.
Mwanzoni kabisa mwa utawala wa Kikwete (nasita kuweka neno Rais), vyombo vya habari vilimuandama sana kuandika kila kukicha maovu aliyoyafanya ikiwemo kashfa ya Kiwila, kila kukicha utasikia hili na lile kuhusiana na udhaifu wa utawala wa wake, ninaamini mengi yaliyokuwa yakisemwa dhidi yake yalikuwa ya kweli kwasababu hakuwahi kushtaki kwamba anasingiziwa na kushushiwa heshma yake bure, sana sana nakumbuka alisema "Watanzania mtanikumbuka" mmoja wa watu waliokasirishwa na kauli yake hiyo nilikuwa ni mimi maana sikuona tutamkumbuka kwa lipi? kumbe huyu mtu anaona mbali sana yeye binafsi utawala wake ulikuwa una madhaifu mengi tuu lakini aliweza kutabiri kwamba kipindi cha Kikwete hali itakuwa mbaya zaidi yatajitokeza mambo ambayo lazima tutamkumbuka hata kwa udhaifu wake, hebu fikiria yafuatayo katika utawala wa Mkapa.
1. Kasi ya Mfumuko wa bei ilikuwaje? Na spidi ya kuanguka kwa shiringi dhidi ya fedha za kigeni ilikuwaje?
2. Kasi ya ukuaji wa uchumi ilikuwaje?
3. Ni mara ngapi uongozi wake ulikwenda kukopa katika mabenki ya biashara ili kughalamia shughuli za kawaida za serikali kutokana na serikali kutokuwa na pesa?
4. Wakati gani serikali yake iliagiza kila wizara au mkoa ikate bajeti ya matumizi yake kwa zaidi ya 30% kutokana na kukosa uwezo?
5. Deni la Taifa lilikuwaje?
6. Kasi ya ongezeko la mapato ya serikali ilikuwaje? (hivi karibuni TRA wameshindwa kufikia lengo kwa zaidi ya 10?)
7. Ni mara ngapi wananchi walijitokeza hadharani kupinga ugumu wa maisha?
8. Ni miradi mingapi mikubwa ya maendeleo ilianzishwa katika kipindi chake?
9. Kiwango cha ubabaishaji katika uteuzi kilikuwaje rejea "turnover" ya mawaziri.
10. Katika sector ya michezo mkapa hakuwa karibu sana kama kikwete, lakini mkapa alijenga uwanja wa soka na baadaye Kikwete akamleta maximo na kula chakula cha jioni na timu ya taifa mara kadhaa.
11. Ni kiasi ganii neno udini lilitamkwa hadharani aidha na yeye mwenyewe kama kiongozi wa nchi au wananchi.
12. Mara ngapi alijitokeza hadharani kulumbana kisiasa kwa minajiri ya kujisafisha?
Haya ni machache yanayonifanya nimkumbuke Mkapa nikilinganisha na yanayojitokeza ktka utawala Kikwete na yamenifanya niamini kwamba huyu mtu ni mnajimu alijuaje kwamba nitamkumbuka?
Mkapa kichwa bwana
Sasa si hiyo ni siasa, kila mwanasiasa anavutia kwenye chama chake. Wewe unatarajia Dr. Slaa awasifie CCM?wote yale yale tu...
si ni mkapa huyuhuyu juzi aliita wapinzani wa tanzania ni kokoto?
Umeambiwa anamapungufu yake lakini hayawezi kulinganishwa na yuleeeeeeeeeeekihwa akajiuzia mali ya uma kwa bei poa ref,kiwira nbc nk.
silence is the best noise one can make...........mkapa ni kiongozi shupavu sana.......sio kama huyu mwizi, mtoto mwizi na sasa amemfundisha mkewe wizi ( rejea ile hundi feki)
Unaonaje tuanzishe kampeni ya kumrudisha Mkapa?silence is the best noise one can make...........mkapa ni kiongozi shupavu sana.......sio kama huyu mwizi, mtoto mwizi na sasa amemfundisha mkewe wizi ( rejea ile hundi feki)
mwanzoni kabisa mwa utawala wa kikwete (nasita kuweka neno rais), vyombo vya habari vilimuandama sana kuandika kila kukicha maovu aliyoyafanya ikiwemo kashfa ya kiwila, kila kukicha utasikia hili na lile kuhusiana na udhaifu wa utawala wa wake, ninaamini mengi yaliyokuwa yakisemwa dhidi yake yalikuwa ya kweli kwasababu hakuwahi kushtaki kwamba anasingiziwa na kushushiwa heshma yake bure, sana sana nakumbuka alisema "watanzania mtanikumbuka"[/b] mmoja wa watu waliokasirishwa na kauli yake hiyo nilikuwa ni mimi maana sikuona tutamkumbuka kwa lipi? Kumbe huyu mtu anaona mbali sana yeye binafsi utawala wake ulikuwa una madhaifu mengi tuu lakini aliweza kutabiri kwamba kipindi cha kikwete hali itakuwa mbaya zaidi yatajitokeza mambo ambayo lazima tutamkumbuka hata kwa udhaifu wake, hebu fikiria yafuatayo katika utawala wa mkapa.
1. Kasi ya mfumuko wa bei ilikuwaje? Na spidi ya kuanguka kwa shiringi dhidi ya fedha za kigeni ilikuwaje?
2. Kasi ya ukuaji wa uchumi ilikuwaje?
3. Ni mara ngapi uongozi wake ulikwenda kukopa katika mabenki ya biashara ili kughalamia shughuli za kawaida za serikali kutokana na serikali kutokuwa na pesa?
4. Wakati gani serikali yake iliagiza kila wizara au mkoa ikate bajeti ya matumizi yake kwa zaidi ya 30% kutokana na kukosa uwezo?
5. Deni la taifa lilikuwaje?
6. Kasi ya ongezeko la mapato ya serikali ilikuwaje? (hivi karibuni tra wameshindwa kufikia lengo kwa zaidi ya 10?)
7. Ni mara ngapi wananchi walijitokeza hadharani kupinga ugumu wa maisha?
8. Ni miradi mingapi mikubwa ya maendeleo ilianzishwa katika kipindi chake?
9. Kiwango cha ubabaishaji katika uteuzi kilikuwaje rejea "turnover" ya mawaziri.
10. Katika sector ya michezo mkapa hakuwa karibu sana kama kikwete, lakini mkapa alijenga uwanja wa soka na baadaye kikwete akamleta maximo na kula chakula cha jioni na timu ya taifa mara kadhaa.
11. Ni kiasi ganii neno udini lilitamkwa hadharani aidha na yeye mwenyewe kama kiongozi wa nchi au wananchi.
12. Mara ngapi alijitokeza hadharani kulumbana kisiasa kwa minajiri ya kujisafisha?
Haya ni machache yanayonifanya nimkumbuke mkapa nikilinganisha na yanayojitokeza ktka utawala kikwete na yamenifanya niamini kwamba huyu mtu ni mnajimu alijuaje kwamba nitamkumbuka?
Mwaka 1995 Kikwete aliposhinda raundi ya kwanza Nyerere alisema 'bado mdogo' wakati umri wa kikwete wakati huo ni mkubwa kuliko umri wa Nyerere wakati anaukwaa urais 1961. Watu hawakumwelewa Nyerere kuwa alimaanisha Kikwete hawezi urais kistaarabu. Leo ndo tunajua ukweli kile alichokimaanisha Nyerere kuwa ni Kikwete hawezi kuwa Rais tatizo halikuwa umri.