Benjamin Mkapa: Watanzania mtanikumbuka

Benjamin Mkapa: Watanzania mtanikumbuka

Akumbukwe kwa nini naye huyo? Kuna tofauti gani ya maisha baina ya utawala wake na ule wa Mwinyi na Kikwete? Rumba bado ni kali tu na Tanzania hatujawahi kuwa na ahueni ya maisha hata siku moja. Na hapo wala sijagusia mambo mengine….

Myonge myongeni lakini haki yake mpeni. Kwanini uangalie upande mmoja tu wa udhaifu lakini hutaki kukubali mafanikio yake? Angalia miradi ya barabara, hali ya barabara za lami katika jiji lamwanza, daraja la mkapa ..nk. hivi unakumbuka mkapa aliikutaje nchi hii kutoka kwa mwinyi? nchi ilikuwa muflisi na kama waliopo leo kwa mwenendo wao ndiyo wangerithi kutoka kwa mwinyi sijui ungesema nini.
 
hali ya uchumi ilikuwa bora zaidi wakati wa Mkapa kuliko wakati wa Mwinyi na JK. kwa hilo kweli Ben tunakukumbuka. hali ya uchumi ingekuwa nzuri zaidi kama migodi na mikataba ya aina hiyo ingewekwa kwa maslahi ya nchi zaidi kuliko ilivyo kwa sasa. pia madeal ya rada na mengineyo yasingekuwepo Ben ungekuwa shujaa wa kukumbukwa milele Tz
 
Dhambi zinatofautiana mkubwa ndio maana yesu alisema anayesamehewa sana hupenda sana na anayesamehewa kidogo hupenda kidogo wakati wa yule CD.

Romans 3:23 "for all have sinned and fall short of the glory of God". Mungu amekataza dhambi na hakuna dhambi iliyohalalishwa mbele ya mungu, wala hakuna dhambi ndogo na kubwa. Rudi kwa mchungaji akupe neno la kiroho.
 
Kwa Wizi kweli tutakukumbuka. Yaani wewe ndiye ulifungua milango ya mafisadi. Ulikuwa lege lege ambaye hukujua nini maana ya urais.
 
Wakuu,

Tutake tusitake kwa hali ilivyo sasa wengi wetu tunamkumbuka Mzee Nkapa kwa mambo mengi mojawapo ikiwa ni kujenga uchumi na miundombinu mbalimbali nchi nzima na jambo kubwa ambalo sisi wanyonge hatutalisahau ni kulinda bidhaa tunazotumia kila siku sisi watu wa chini zisipande bei kiholela. Wakati wa uongozi wa Mkapa hakukuwa na porojo porojo. Serikali ilikuwa na heshima mbele ya umma. Lakini leo hii, uchumi hovyo, bei za bidhaa zinapanda kiholela, serikali inaendeshwa kiswahiliswahili na kukosa heshima mbele ya wananchi, n.k. Ndiyo maana nasema pamoja na mapungufu yake akiwa kama binadamu, Mkapa anabaki kuwa shujaa wa kukumbukwa mbele ya kikwete!
 
EPA, NYUMBA ZA SERIKALI, MEREMETA,KIWIRA. KUUZWA KWA BENKI YA NBC, UBINAFSISHAJI WA MASHIRIKA YA UMMA, SHERIA ZA DHAHABU, KUVULIWA URAIA JENERALI ULIMWENGU, UCHAGUZI ZANZIBAR MWAKA 2000. hayo yalifanyika chini ya BEN, je hayo ndo ya kumkumbukia?, au kwa sababu njaa ya leo kali kuliko ya jana , basi njaa ya jana si njaa?.
 
sjapata mda wa kusoma comment zote but mimi napenda kuweka wazi swala moja, tofauti kubwa ya mkapa na kikwete ;mkapa was real a man and alikuwa na final say as a president ;akisema acha utaacha,,, fanya utafanya but huyu mwenzetu kasema acha we fanya,,, akisema usifanye nyie ndo kwanza mnaongeza spidi he doesn't have the final say as the president na ndo maana tupo hapa tulipo tunalalamika tuuuuu ye anabakia kukenua meno tu kwenye majukwaa
 
Mwanzoni kabisa mwa utawala wa Kikwete (nasita kuweka neno Rais), vyombo vya habari vilimuandama sana Mkapa na kuandika kila kukicha maovu aliyoyafanya ikiwemo kashfa ya Kiwila, kila kukicha utasikia hili na lile kuhusiana na udhaifu wa utawala wa wake, ninaamini mengi yaliyokuwa yakisemwa dhidi yake yalikuwa ya kweli kwasababu hakuwahi kushtaki kwamba anasingiziwa na kushushiwa heshma yake bure, sana sana nakumbuka alisema "Watanzania mtanikumbuka" mmoja wa watu waliokasirishwa na kauli yake hiyo nilikuwa ni mimi maana sikuona tutamkumbuka kwa lipi? kumbe huyu mtu anaona mbali sana yeye binafsi utawala wake ulikuwa una madhaifu mengi tuu lakini aliweza kutabiri kwamba kipindi cha Kikwete hali itakuwa mbaya zaidi yatajitokeza mambo ambayo lazima tutamkumbuka hata kwa udhaifu wake, hebu fikiria yafuatayo katika utawala wa Mkapa.

1. Kasi ya Mfumuko wa bei ilikuwaje? Na spidi ya kuanguka kwa shiringi dhidi ya fedha za kigeni ilikuwaje?
2. Kasi ya ukuaji wa uchumi ilikuwaje?
3. Ni mara ngapi uongozi wake ulikwenda kukopa katika mabenki ya biashara ili kughalamia shughuli za kawaida za serikali kutokana na serikali kutokuwa na pesa?
4. Wakati gani serikali yake iliagiza kila wizara au mkoa ikate bajeti ya matumizi yake kwa zaidi ya 30% kutokana na kukosa uwezo?
5. Deni la Taifa lilikuwaje?
6. Kasi ya ongezeko la mapato ya serikali ilikuwaje? (hivi karibuni TRA wameshindwa kufikia lengo kwa zaidi ya 10?)
7. Ni mara ngapi wananchi walijitokeza hadharani kupinga ugumu wa maisha?
8. Ni miradi mingapi mikubwa ya maendeleo ilianzishwa katika kipindi chake?
9. Kiwango cha ubabaishaji katika uteuzi kilikuwaje rejea "turnover" ya mawaziri.
10. Katika sector ya michezo mkapa hakuwa karibu sana kama kikwete, lakini mkapa alijenga uwanja wa soka na baadaye Kikwete akamleta maximo na kula chakula cha jioni na timu ya taifa mara kadhaa.
11. Ni kiasi ganii neno udini lilitamkwa hadharani aidha na yeye mwenyewe kama kiongozi wa nchi au wananchi.
12. Mara ngapi alijitokeza hadharani kulumbana kisiasa kwa minajiri ya kujisafisha?

Haya ni machache yanayonifanya nimkumbuke Mkapa nikilinganisha na yanayojitokeza ktka utawala Kikwete na yamenifanya niamini kwamba huyu mtu ni mnajimu alijuaje kwamba nitamkumbuka?
 
Mwanzoni kabisa mwa utawala wa Kikwete(nasita kuweka neno Rais), vyombo vya habari vilimuandama sana kuandika kila kukicha maovu aliyoyafanya ikiwemo kashfa ya Kiwila, kila kukicha utasikia hili na lile kuhusiana na udhaifu wa utawala wa wake, ninaamini mengi yaliyokuwa yakisemwa dhidi yake yalikuwa ya kweli kwasababu hakuwahi kushtaki kwamba anasingiziwa na kushushiwa heshma yake bure, sana sana nakumbuka alisema "Watanzania mtanikumbuka"
Kikwete katika awamu yake ya kwanza aliinjinia kutolewa kwa kashfa dhidi ya BWM na hapo kwenye red, ni kweli jamaa hakushitaki bali aliamua kukaa pembeni na hata wakati wa kampeni zilizomfanya JMK kurudi madarakani jamaa alikaa pembeni kabisa na ilibidi watumwe wazee kwenda kumwomba ashiriki kampeni (mmoja wa wazee ni kingunge) kwani upepo haukuwa upande wao.

Nakuhakikishia kabisa kuwa aliposimama BWM pale jangwani wananchi waliisikia sauti yake na kukumbuka mazuri aliyowafanyia yanayojumuisha hayo uliyoyaainisha.

Mkapa sio msafi lakini anabaki kuwa kiongozi makini aliyekuwa anaijua Tz na umaskini wake na hivyo akajitoa kuiba huku akirahisisha maisha kwa mtz wa hali ya chini
 
Mh Rais Mkapa ninakukumbuka sana!Hii awamu ya nne inaongozwa na marais watatu(RA, EL na JK) na kila mtu ana mawaziri wake sasa ndio matatizo tulionayo!
 
Ilikua rahisi kwa Rais wa tatu kutabiri kinachokuja kwani alimfahamu ajaye nyuma yake (rais wa nne) ana uwezo gani kiutendaji kwani aliufahamu utendaji wake kwa miaka kumi aliyofanya kazi chini yake kama waziri wa mambo ya nchi za nje. Kama asingelazimishwa na nguvu ya 'Mtandao' iliyokuwepo kuna kila dalili ya kuamini kwamba 'kijiti' kingekwenda kwa mtu mwingine kabisa.
 
Ni kweli kabisa mkuu Hilo halina ubishi, BWM alikuwa mtaalamu na kukaa kimya kwake ilkuwa nibusara. Si unajua wahenga walisema "don't argue with a fool people might not distinguish who is a fool between you". Kwa vile BWM alijua aliyowafanyia watanzania ni makubwa, lakini akaona hizo cheap media mudslinging campain zilizoanzishwa na wanasiasa wasio makini akaona akae kimya. Nakuhakikishia ktk miaka 4 ya awamu ya JK iliyobakia mengi mutayaona yatakayo waumiza kiuchumi
 
Mi ntamkumbuka zaidi ndugu yangu,****** mwenzagu alhaj alfan jmk, kwa kuniletea machungu ya maisha na kuufanya ubongo wangu ufikirie kama kesho itafika! Namshukuru mkapa kwa kunipa mazingira tulivu na ktk kipind chake nliweza kupiga miayo kijanja na si kama siku izi ambapo tumbo na mgongo viko zero distance kwa kukosa kitenganishi(mkate/chakula ). Jk ntakukumbuka daima kwa kuifanya akili yangu iwaze itaishije leo na si kuwaza ntafanyeje ili taifa letu listawi!
 
Ilikua rahisi kwa Raisi wa tatu kutabiri kinachokuja kwani alimfahamu ajaye nyuma yake(raisi wa nne) anauwezo gani kiutendaji kwani aliufahamu utendaji wake kwa miaka kumi aliyofanya kazi chini yake kama waziri wa mambo ya nchi za nje. Kama asingelazimishwa na nguvu ya 'Mtandao' iliyokuwepo kuna kila dalili ya kuamini kwamba 'kijiti' kingekwenda kwa mtu mwingine kabisa.

Kwanini Mkapa hakusimama ahesabiwe akiwa na msimamo wake? nashindwa amini unajimu wake mbali na kuwa alikuwa anatuambia kuwa tunamwona yeye ni mchafu ila ajaye tutakoma! je hapo alitutakia mazuri?
 
Mimi nitamkumbuka Mkapa kwa kujenga Uwanja wa mpira wa kisasa, na pia nitamkumbuka Kikwete kwa kujenga chuo kikuu cha Dodoma(UDOM)
 
Jamani "Mkweeeri" toka lini??? Babu wa taifa alishaliona mapeeema, mtu ana experience ya kucheza ngoma na utawala wapi na wapi......c makosa yake. Makosa ni ya wadanganyika waliomchagua kwa kuuza kura (maendeleo yao) kwa ku-exchange na kanga na kofia.
 
Back
Top Bottom