It appears kile kikosi kilichoshutumiwa na Ben, kimekwenda kukaa pamoja na kuandika hii makala ndefu ya kujisafisha na kumsafisha Zitto. Lakini katika jambo lililonishangaza sana ni kwamba
Mchange anasema alikuwa anajua mission yote ya Ben, lakini aliendelea kwenda na kushiriki kwenye mikakati yote ya kukihujumu chama. Na zaidi sana anasema hata wenzake akina
Juliana Shonza alikuwa anawajulisha. Sasa najiuliza:
- Ni nini kilichokuwa kinawatuma kuendelea kushiriki katika hivyo vikao na mikutano ya kukichafua chama na kukisambaratisha huku wakijua kwamba wanafanya kitu kibaya? Hapa tutauelewa vema unafiki wa mchange!
- Ni kwanini kundi la akina Mchange, Juliana, Gwakisa, Taswira na hiyo MP7 kwa ujumla wake lilijitolea na kujipambanua kwenye mitandao kumkashifu na kumchafua Dr. Slaa na si Zitto au kiongozi mwingine yeyote wa chama? Walitumwa na nani? Kwa maslahi ya nani? Je ni Ben aliyewatuma kufanya mliyokuwa mnayafanya? Je hamkujifunza ni kwanini Ben mwenyewe hakuwa akishirikiana nanyi kuwachafua viongozi wa chama?
- Kwa kukubali kutumiwa, tutakuwa tumekosea tukiwaita nyie mataahira? Maana mlishindwa kutumia akili zanu binafsi kuchambua na kutambua kwamba mnayoyafanya ni ya kihuni? Sasa mwaonaje tukisema wewe Mchange na wenzako wote mliokuwa mnaandika maneno ya hovyo kwenye facebook dhidi ya viongozi wa chadema ni watu wenye mtindio wa ubongo?
- Kama mlijua kuwa Ben, ni mnafiki na kwamba ni shushushu, kwanini hamkuwa wa kwanza kujitokeza na kuanika uovu wa Ben kwenye mitandao badala yake mliandika ya Dr. Slaa? Iweje msubiri hadi Ben ajitokeze na kuanika ya kwenu ndipo mje mbele yetu na kuanza kujisafisha? Tunao ushahidi kwamba nyie ndiyo mliokuwa mnakihujumu chama kutokana na maneno yenu mliyokuwa mnayaandika kwenye mitandao na magazetini? Je mnaweza kuwasilisha ushahidi wowote wa maandishi au wa mdomo unaoonyesha kwamba Ben saanane alikuwa pamoja nanyi kuhujumu chama?
- Mwisho napenda kujua yale yote ambayo akina Mchange, Tuntemeke, Taswira, Juliana na wapuuzi wasaliti wengine wa chama walikuwa wanayafanya, yalikuwa ni kwa faida ya nani? Kwa kuwa hili kundi lote linamuunga mkono Zitto, ni kwa namna gani mtatuaminisha kwamba hamkuwa mnatumwa na Zitto kufanya haya? Na kwanini Zitto alikuwa hawaonyi (hasa wewe Mchange) kila unapotoa tuhuma nzito na za hatari kwa mstakabali wa chama ilihali wewe ni mtu wake wa karibu?
Ninapenda kuwashauri nyie akina Mchange,
Ben Saanane,
Zitto na wengine wote kwamba mmeshasema mengi, unafiki wenu umeshajulikana kwetu hivi sasa. Kilichobaki rudini kwenye vikao vya chama mkatubu, na mrudi kwenye mstari wa kuendelea kukijenga chama.
Zitto acha tamaa ya madaraka. Huwezi kupata madaraka kama chama chenyewe unachotegemea kikubebe kuelekea Ikulu kitakuwa kimekufa.
Zitafakarini njia zenu!