Nimesoma yote nimebaki nasikitika.
Ni lazima chama kiwaite wote waliotajwa kwani kuna ukweli kwa zaidi ya asilimia 85.
Swala la kusubiri eti kuletewa madai halisaidii.
Zitto Zuberi, Ben Saanane, Dr kitila mkumbo, habibu mchange, Juliana Shoza, Exaudi Mamuya, majina mengine ni ya badnia sijui ni akina nani ila najua hao wakiitwa watatajana.
Hatuwezi kuendelea kufanya kazi kwenye mazingira kama haya, lazima viongozi wa juu waelewe wazi kuwa chama sio hawa watu wachache inabidi wahojiwe na tupewe maelezo.
Kukaa kimya kwenye mambo kama haya kwa kutegemea natural course does not show leadership. Lazima viongozi wakubali kupamabana na haya mambo leo. Ufa uliopo ni mkubwa na wengine tunajua mengi sana hatutaki tu kuwa madomokaya.
Kuna watu ni wasomi lakini sio viongozi, tusichanganye degree , masters phd na uongozi. Uongozi ni karama, hekima, busara, utulivu , ushauri , uwajibikaji na kuweza kuhakikisha unalinda ulichoapa kukitumikia. Hawa wote waliotajwa wamevunja katiba ya chama na ikithibitika waliotajwa nayo ni ya kweli lazima adhabu stahiki ziwafuate. Nitashangaa sana kama tunaweza kuwahoji na kuwafukuza madiwani chama kikashindwa kutumia kipimo hicho hicho kwa hawa watu. Toxic.
Mwaka 2015 sio mbali tuyamalize haya matatizo leo ili mwenye maumivu yamuume sasa tufike 2015 na team safi yenye nia thabiti ya kumkomboa mtanzania.
Tamaa ya madaraka ya hawa wanaojiita vijana wasomi ndio inawaponza. Hawana shukrani wala hawana vision. Hawajui maana ya chama cha siasa. Mjumuiko huu wa watu wengi wenye fikra, akili, uwezo, nia na malengo tofauti hayahitaji ilmradi kiongozi bali yanahitaji kiongozi wa kweli mwenye record safi.
Nafurahi kwani itabidi wengine wasifike nchi ya ahadi kama Musa.
Chief Mkwawa wa kalenga.
Makundi ya vijana walafi yasiposhughulikiwa leo yatatuponza baadaye.