Beki wa Vijana ataka uraia wa Italia

VUVUZELA

JF-Expert Member
Jun 19, 2010
3,103
786
Beki wa Vijana ataka uraia wa Italia
JACKSON ODOYO
MTANZANIA anayecheza soka Italia, George Mtemahanji amesema ataomba uraia wa Italia. Mtemahaji, ambaye anachezea Modena FC inayocheza Ligi Daraja la Pili nchini Italia, atakuwa anafuata nyayo za Mtanzania mwingine Patrick Mtiliga, ambaye anachezea Malaga ya Hispania, ambaye aliutosa uraia wa baba yake Mtanzania na kuchukua ule wa Denmark, ambako amechezea mara nne timu ya taifa ya nchi hiyo.

Beki huyo aliiambia Mwanaspoti kuwa anataka kutumia mwanya wa Italia kuruhusu mtu kuwa na uraia wa nchi mbili.

Mtemahaji, ambaye kwa sasa yuko katika kambi ya timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chinia ya miaka 23, alisema atalazimika kuomba uraia ili acheze soka huko bila bughudha.

Alisema ataomba mwakani uraia huo kwa kuwa ameishi kwa miaka tisa tu nchini Italia, ambako sheria inaruhusu kuomba uraia baada ya kuishi miaka 10 nchini humo.

�Sijaomba uraia wa Italia kwa sababu sijafikisha miaka kumi huko, huwezi kupewa uraia kama haujamaliza miaka 10 ndani ya nchi hiyo.

"Kwa sasa nina miaka tisa tangu nilipokwenda hivyo ninaimani kwamba mwakani nitachukuwa uraia na wanaruhusu mtu kuwa na uraia wa nchi mbili,� alisema Mtemahaji, ambaye anaishi na wazazi wake huko Italia.

Hata hivyo, kuna serikali ya Tanzania nayo imeandaa mpango wa kuruhusu Watanzania kuwa na uraia wa nchi mbili.

Akizungumzia timu ya taifa ya vijana, Mtemahaji mwenye umri wa miaka 18, alidai hajafurahishwa mazoezi ya timu hiyo.

Beki hiyo, alidai mazoezi anayopewa na makocha Jamhuri Kiwelu `Julio' na msaidizi wake Mohamed Ayoub alifundishwa wakati akiwa na umri wa miaka 12 nchini Italia.

�Sioni kitu kipya katika mafunzo ya walimu wa timu hii kwa sababu hayo wanayofundisha hivi sasa nilishajifunza nikiwa na miaka 12,� alisema Mtemahaji, ambaye ameonyesha umahiri mkubwa katika kulinda lango na kupanda mbele kusaidia mashambulizi.


Mtemahaji alidai anataka mafunzo kama ya huko Ulaya yanayoweka katika mkazo wa namna ya kucheza mpira wa kasi, kutumia akili na nguvu.

Source: Mwanaspoti
 
Modena FC ipi anayochezea Mtemahaji? katika squad list ya wachezaji woote hayumo.
 
nami sijamuona hata nimetafuta sana kwenye hiyo club sijamuona hata jina lake halipo kwenye net uki search
 
nami sijamuona hata nimetafuta sana kwenye hiyo club sijamuona hata jina lake halipo kwenye net uki search

Campionato di vertice anche per gli Allievi Regionali di Mister Gianluca Cavazzuti, sempre tra le prime quattro posizioni della graduatoria ed importante serbatoio per gli Allievi Nazionali. Numerosi ragazzi, nel corso della stagione, si sono meritati più di una convocazione con gli Allievi di Mister Treggia ed hanno acquisito la giusta esperienza per affrontare nel prossimo anno, da protagonisti, il campionato nazionale di categoria. Diversi i record dei ragazzi di Mister Cavazzuti: la vittoria esterna con più gol (1-5 sul campo del Russi), il maggior numero di vittorie stagionali (17), maggior numero di pareggi (12), maggior numero di vittorie esterne (7) e minor numero di sconfitte esterne (3). Nella squadra più prolifica del Settore Giovanile, con 63 gol fatti, 17 su 19 giocatori di movimento sono andati a segno almeno una volta: Stefano Pecora (11 reti), Andrea Bernardo e Pietro Pannullo (9), Facundo Stik e Roberto Ansaloni (5), Andrea Guicciardi, Angelo Piscopo e George Mtemahanji (3), Federico Martinelli, Tommaso Iazzetta, Filippo Manno, Francesco Foresta e Said Mamouni (2), Andrea Di Stasio, Francesco Bosco, Francesco Munaro, Samuele Marchetti e Matteo Montorsi con una rete.

Huyo hapo kwenye red na source yake hii hapa.

Modena Football Club 1912 - Sito Ufficiale - Official Site
 
Campionato di vertice anche per gli Allievi Regionali di Mister Gianluca Cavazzuti, sempre tra le prime quattro posizioni della graduatoria ed importante serbatoio per gli Allievi Nazionali. Numerosi ragazzi, nel corso della stagione, si sono meritati più di una convocazione con gli Allievi di Mister Treggia ed hanno acquisito la giusta esperienza per affrontare nel prossimo anno, da protagonisti, il campionato nazionale di categoria. Diversi i record dei ragazzi di Mister Cavazzuti: la vittoria esterna con più gol (1-5 sul campo del Russi), il maggior numero di vittorie stagionali (17), maggior numero di pareggi (12), maggior numero di vittorie esterne (7) e minor numero di sconfitte esterne (3). Nella squadra più prolifica del Settore Giovanile, con 63 gol fatti, 17 su 19 giocatori di movimento sono andati a segno almeno una volta: Stefano Pecora (11 reti), Andrea Bernardo e Pietro Pannullo (9), Facundo Stik e Roberto Ansaloni (5), Andrea Guicciardi, Angelo Piscopo e George Mtemahanji (3), Federico Martinelli, Tommaso Iazzetta, Filippo Manno, Francesco Foresta e Said Mamouni (2), Andrea Di Stasio, Francesco Bosco, Francesco Munaro, Samuele Marchetti e Matteo Montorsi con una rete.

Huyo hapo kwenye red na source yake hii hapa.

Modena Football Club 1912 - Sito Ufficiale - Official Site

Ahsante kwa kutufahamisha. Kwa hiyo hii club iko Serie B?
 
Huyu dogo nae mzushi nakumbuka alikuwa anahojiwa na Clouds FM akasema hawezi kuukana uraia wa Tanzania
 
<br />
<br />
mkuu haukani uraia wa bongo coz italy inaruhusu uraia wa nchi mbili.

Sasa akibainika amechukua uraia wa Italy basi si itabidi aukane uraia wa kibongo la sivyo itakuwa soo akija bongo kutokana na sheria zetu?
 
Kitu kinachonichekesha kua hayo maneno mimi sijasema kabisa, yule mwandishi wa habari alinihoji baada ya mazoezi pale karume na mimi nikasema maneno mengine kabisa, nimeshangaa kuona kama kwenye gazeti ameandika vingime!!! Mimi niente mtanzania na naipenda inchi yangu suoni shida ya kubadilisha uraia!!!!
 
Huyu dogo nae mzushi nakumbuka alikuwa anahojiwa na Clouds FM akasema hawezi kuukana uraia wa Tanzania

Wewe nae hufahamu alichoongea? kasema Italia wanaruhu Uraia wa nchi mbili, sasa hapo hana sababu ya kuukana Utanzania, labda Utanzania umkane yeye.
 
Wewe nae hufahamu alichoongea? kasema Italia wanaruhu Uraia wa nchi mbili, sasa hapo hana sababu ya kuukana Utanzania, labda Utanzania umkane yeye.
Asante ribosome kua umenielewa, kitu strage ni kua odoyo ameandika alichoelewa yeye sio nilichosema mimi. Mimi narudia tena naipenda sana inchi yangu siwezi kuikataa lakini serekali inabidi ijue kua niente important kuweka possibility ya kuchukua Uraia wa inchi zingine.
 
Back
Top Bottom