Ricardo Kaka: Mlokole safi aliezima ndoto na ufalme wa Manuel Rui Costa pale Milan

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
21,838
38,729
Zamani sana Jijini Milan nchini Italia miaka 16 iliopita kulikuwa na jina la Playmaker mmoja mstaarabu mno, muungwana kutoka Mji wa vipaji wa Sao Paulo ni kama vile Morogoro kwa Tanzania, Ricardo Izecson dos Santos Leite maarufu kama 'Kakà'

Nani asiyemkumbuka fundi huyu ambaye anatua uwanja wa ndege wa Malpensa kwenye kitongoji cha Varese pale Italia na biblia yake, Waitaliano wanamtazama Silvio Berlusconi na Carlo Ancelotti, nyie vipi mnatuletea mtoto laini huyu, ataweza kweli soka la Italia, ataweza kweli kupasua Catenacio na Uchawi mweusi kwenye kujilinda?

Maswali yalikuwa mengi ila Kakà alijibu juu ya nyasi za San Siro, aliwapa majibu wale wahafidhina wa Milano, Fossa de Leoni kundi la mashabiki lilofunguliwa mwaka 1968 japo 2005 lilisambaratika, hawa walivua kofia kwa Mbrazil huyu ambaye hakuwa na mambo mengi kwenye kazi yake, but he kept things ticking

Ancelotti aliamini Kaka anafaa kuungana na Andriy Shevchenko na Philpo Pippo Inzaghi kwenye eneo la mwisho, Carlo aliamini miguu ya Manuel Costa na akili yake haiwezi tena kufanya hata nusu ya ubora wa Kakà, fundi huyo alitengeneza hub pale kati kila kitu kilikuwa moto

Kule nchini kwao Brazil ilimlazimu Kocha wa timu ya taifa ajifungie kwenye office za CBF, kufikiria anamtumiaje Ricardo kwenye mfumo wake, Carlos Alberto Pereirra alikuja na 4-2-2-2 ili awe tu na fundi wa Sao Paulo

Una the Mighty Brazil yenye namba 9 ya Ronaldo De Lima, una namba 10 ya Dinho wa Gaucho kisha una straika mwingine mwenye mnuso wa bundi kama Adriano, kazi ya Kakà ilikuwa ni kuunganisha, kupikia na kuwafanya wawe free kule mbele, ikumbukwe hakuwa mchoyo

Kiungo chake kilikuwa sio cha kupiga pass tu, bali kuhakikisha imefika tena kwa mlengwa, kiungo chake hakikuwa cha kuwachezesha tu mastraika bali kuhakikisha amedigest kila kitu, alikuwa mwepesi kwenye kupunguza mabeki, he had flamboyant skills

Unataka tuseme nini kuhusu ucha Mungu wake? Wakati Pato anaenda Milano aliwahi kuulizwa na De Lima, unamfata Kakà au Mimi, yani unataka maisha ya dini au maisha ya bata😂 De Lima alitaka kumpa jarida la Playboy kijana Pato
.
Hii dunia wamepita watu bwana kwenye soka.
FB_IMG_17110563027070845.jpg
FB_IMG_17110574087446777.jpg
FB_IMG_17110574230103924.jpg
 
Kuna game vs arsenal, alikamatwa vibaya mnoo.

Ricardo Ernesto almangungule kaka kibraza. Alikuwa fundi sana.

Lakini kusema kuzima ndoto ya rui costa si kweli, kaka alienda pale kama mrithi wa rui costa, sababu kaka anaenda milan mwaka 2003 rui costa tayari ana miaka 32 kama sikosei, tofauti ya kaka na rui costa kiumri ni kama miaka 10 hivi.
Rui costa tayari alikuwa ukingoni mwa carrer yake ya soka.
 
RUI COSTA alikua ni mchezaji wa aina yake kabisa, KAKA hakuwahi kufika uwezo wa Rui Costa, kilichombeba ni Muda, mabadiliko ya kimchezo, alikua yupo kimodern game zaidi. Licha ya kuwa alikua akimueka bench lakini hakuwa akiweza kumtizama machoni mara mbili.
 
Manchester United alipigwa 3 -0 , Liverpool akapigwa 2-1 fainali ya uefa CL.
Ac Milan wakati huo ilijaa mabingwa Tupu katika wakitawala na Ricardo kaka na andrea pirlo.
Vile vipaji vya zamani vinaenda kuisha kabisa wanabaki watuamia nguvu kina haarland.
 
Daah umenikumbusha mtu aisee AC Milan ndio ilikua Timu yenye vipaji sana huko Italy na walikua wanajua mpira kweli katikati pana Seerdorf, Andrea Pirlow na Gatuso huko mgongoni yupo Nesta kushoto Maldin shavu la kulia Cafu aisee hii Timu ilikua balaa sana hapo Madrid anataabika kutolewa robo kila wakati na Timu ya Ufaransa...
 
Daah umenikumbusha mtu aisee AC Milan ndio ilikua Timu yenye vipaji sana huko Italy na walikua wanajua mpira kweli katikati pana Seerdorf, Andrea Pirlow na Gatuso huko mgongoni yupo Nesta kushoto Maldin shavu la kulia Cafu aisee hii Timu ilikua balaa sana hapo Madrid anataabika kutolewa robo kila wakati na Timu ya Ufaransa...
Manchester United alipigwa 3 -0 , Liverpool akapigwa 2-1 fainali ya uefa CL.
Ac Milan wakati huo ilijaa mabingwa Tupu katika wakitawala na Ricardo kaka na andrea pirlo.
Vile vipaji vya zamani vinaenda kuisha kabisa wanabaki watuamia nguvu kina haarland.

Mnaachaje kumtaja Ambrosini?
 
Kajamaa hako kalikua na uwezo wa kupiga killing passmoja matata sana ya kuvunja mistari miwili ya defenders na ikafika, ukijaribu ku block unakufa ww.
 
Sir Alex Ferguson alikuwa anapenda kumtumia Park Ji Sung kufanya Man marking kwa Ricardo Kaka au Andrea Pirlo “the brain of Milan”
 
Kaka na Rui Costa waliishi Milan zama mbili tofauti kabisa.
RuI alikuwa fundi pia.
 
rekebisha kauli yako, kaka ndio alikuwa fundi pia. Rui alikuwa ni mchawi kabisa
Kusema kweli kwangu Rui alikuwa fundi zaidi ya Kaka, labda kwenye takwimu za G/A ndio watu wanaona Kaka alimzidi Rui.
 
Back
Top Bottom