Bei ya sukari nchini yashuka kwa Sh,1500

Bei ya sukari nchini yashuka kwa Sh,1500

Tuwe tunasoma na kuelewa, miezi 2 iliyopita kuna sehemu walinunua sukari hadi kwa tsh.5000 kwa 1kg hiyo 1500 ni wastani wa kupungua kwa bei toka bei ya miezi 2 iliyopita
kwa hiyo 5000-1500=3500/=

Hapa hakuna unafuu wowote.
 
Pye kume imeagizwa sasa mlikua mmekomaa nini kuwabania watu nonesense
 
Upo sahihi kabisa, Habari inasema bei ya SUKARI imeshuka kwa wastan wa sh 900 mpaka 1500 lakini ****** walio wengi wameelewa ndivyo sivyo kwamba bei ya sukari ni sh 1500 [emoji1]
Dah...halafu wakiambiwa masomo ya sayansi ni lazima hadi kidato cha nne wanaanza kulialia hapa🙂🙂
 
We huo utafiti unefanyika wapi mimi nipo kimara kg ni 2500
 
Jamhuri ya watu wa lumumba ndo mmeshushiwa bei
 
Weee umetusahau? Si tunavuma kwa UNAFKI na KUJISHEBEDUA! Kabla sijapiga kura nilikuwa nakunywa chai kwa sukari ya Tshs 1800, leo sukari 2500, tena nipo hapa Mbezi, sijui Bi Mkubwa kule Tambi anauziwa Tshs ngapi, lkn bado wataalamu wa Maths wanasema imeshuka!
Hiyo sukari imeshuka lini? Wapi?
 
Waandishi wetu yaani hawana weledi kabsa na kazi yao.kuandika uongo tuuh.ovyo kabsa.
 
Huyo mwandishi na mhariri wake wamepewa bahasha hao!!. Huo utafiti wameufanya eneo gani au kwa familia za wafanyakazi wa viwanda hivyo!.

**vinginevyo mtoa mada utakuwa ume_take chance "kuwa wa kwanza ku_post" wkt dip wameeleza eneo la utafiti.
Wakiwa upende wenu wanakua fea ila wakiwa upande mwngn bas wamepewa bahasha
 
Vipi bado unanunua kwa 3500?? Maana Nyumbu wanabisha huku kwamba sukari haijashuka..

Nini 2400!
Kwetu sukari 3500 kwa kilo moja.
Waliotoa bei elekezi wametoweka pia,
Hapa kazi Tu
 
Bei ya Sukari nchini imeanza kutengamaa baada ya kushuka kwa wastani wa sh 900 hadi 1,500 kwa kilo

Utafiti mdogo uliofanywa na gazeti la Mwananchi jijini Dar es Salaam na mikoani unaonesha kiwa sehemu kubwa sukari inauzwa kwa wastani wa sh.2400 kutoka zaidi ya sh.3,500 iliyokuwepo miezi miwili iliyopita.
Mkuu hesabu uliacha darasa la ngapi? yani wastani wa 2,500 na 5,000 iwe 1,500?
Kumbe 3500-2400 ni sawa na 1500????
Sasa 3500 mpaka 2400 ni 900 au 1100??
Dah...Mungu ibariki Tanzania 🙄🙄
 
Back
Top Bottom