Bei ya sukari nchini yashuka kwa Sh,1500

Bei ya sukari nchini yashuka kwa Sh,1500

UKAWA watakua wamenuna huko waliko.. Wanatamani watanzania wapate shida ili wao wapate kura 2020
Tusiweke siasa kwenye kila kitu...Kwani huko unapoishi wewe ni kweli sukari inauzwa 1500?
 
View attachment 379442
Bei ya Sukari nchini imeanza kutengamaa baada ya kushuka kwa wastani wa sh 900 hadi 1,500 kwa kilo kutokana na viwanda kuanza uzalishaji pamoja Serikali kuingiza takribani tani 70,000 kutoka nje ya nchi kufidia upungufu uliyokuwepo.
Utafiti mdogo uliofanywa na gazeti la Mwananchi jijini Dar es Salaam na mikoani unaonesha kiwa sehemu kubwa sukari inauzwa kwa wastani wa sh.2400 kutoka zaidi ya sh.3,500 iliyokuwepo miezi miwili iliyopita.
Kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo kunatoa ahuweni kwa Wananchi wengi waliolazimika kutoboa mifuko yao ili kumudu bidhaa hiyo muhimu katika uandaaji wa vyakula mbalimbali pamoja na chai.
Source: Gazeti la Mwananchi.
WACHA WEE MWANDISHI
 
we mbona huelewi..umeambiwa bei imeshuka toka zaidi ya shs 3000 na sasa wastani wa bei shs 2400. hiyo bei yako ni sawa. au ulitaka bure? teh teh.
Soma tena bwege wee imeshuka Lumumba tena kwenye keyboard
 
we mbona huelewi..umeambiwa bei imeshuka toka zaidi ya shs 3000 na sasa wastani wa bei shs 2400. hiyo bei yako ni sawa. au ulitaka bure? teh teh.
Acha mambo ya wastani wewe hesabu zisizo na hualisia,sema hiyo ya 1500 inapatikana wapi mi nikanunue kilo 10 fastafasta
 
Tuwe tunasoma na kuelewa, miezi 2 iliyopita kuna sehemu walinunua sukari hadi kwa tsh.5000 kwa 1kg hiyo 1500 ni wastani wa kupungua kwa bei toka bei ya miezi 2 iliyopita
Mkuu hesabu uliacha darasa la ngapi? yani wastani wa 2,500 na 5,000 iwe 1,500?
 
Wanywa chai mna kelele kweli, bei ya sukari kupanda kiduchu makelelelelelel, mbona sie wapiga pombe bei zinapanda kila siku na hatulalamiki tena hata bajeti ya nchi inatutegemea sisi kuongeza pato!
 
Sukari ipi? ile inayofunikwa na vile vifuniko vya sukari vinavyouzwa kariakoo?
 
Wanywa chai mna kelele kweli, bei ya sukari kupanda kiduchu makelelelelelel, mbona sie wapiga pombe bei zinapanda kila siku na hatulalamiki tena hata bajeti ya nchi inatutegemea sisi kuongeza pato!
Chai wanakunywa wengi ikiwemo wewe na familia yako, pombe wanakunywa wachache hasa wasiomcha Mungu!!
 
Sukari inatakiwa irudi bei yake ya awali,sh 2000 kwa kg mtaani,kisha ndo tuanze kuishusha mpaka 1500,
vinginevyo ni usanii tu
 
Achana na story za magazeti,mwandishi anandika tu Wakati hata bei halisia ya sukari haifahamu

Ovaa
wameambiwa waandike habari za kumfurahisha mkulu, jana kigogo kawatangazia kuwafungia kwa uchochezi ikiwa wataandika habari za kuwakosoa wakuu.
 
Jumapili nilinunua bei kwa Mwanza bado iko juu Tshs. 3,000/=
 
Hutudanganyi kizembe hivyo mana hata sisi wenyewe ni wanunuaji wazuri wa sukari hivyo tunajua bei halisi..wambie hi kiki itaishia Ubungo
 
Back
Top Bottom