CHADEMA wafungua upya kesi dhidi ya Polisi

CHADEMA wafungua upya kesi dhidi ya Polisi

Hiyo kesi ni muhimu sana kipindi hiki ambacho serikali ya awamu ya 5 inaonyesha dhahiri ina lengo la kuurejesha mfumo wa Chama kimoja.

Ushahidi wa wazi ni tukio la jana huko jijini Mwanza ambako wafuasi wa CCM waliruhusiwa kuandamana na baadaye kuhutubiwa na viongozi wao wa Chama wa mkoa.

Hiyo ni double standard ya waziwazi inayofanywa na Policcm ambao siku chache zilizopita walidiriki hadi kuwakamata viongozi wa Chadema, akiwemo Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe, aliyekuwa akipita kwenye matawi mbalimbali ya Chadema akiwasalimia viongozi hao wa matawi, kwa madai ya kukiuka amri waliyoiita ya halali ya zuio la kufanya mikutano yoyote ya kisiasa.

Hata hivyo alipoulizwa RPC wa Mwanza, Ahmed Msangi, sababu za kuruhusu maandamano na mikutano wa CCM akadai kuwa hakuwa na taarifa kama kulikuwa na kitu kama hicho!!

Kumbe intelejensia ya Jeshi letu la Polisi, huwa inaishia katika kubaini matukio yatakayofanywa na vyama vya siasa vya upinzani pekee!!!!!
Huyo kamanda kama alijibu hivyo ni kuonyesha kuwa hawajibiki
 
HAWA POLISI WETU WANAJIDHALILISHA SANA KWA KUPOKEA KILA MAAGIZO YA CCM MWISHO WA SIKU WAO NDIYO WANAISHIA KUHANGAIKA NA KESI,KAMA WALIWARUHUSU CCM WAKAANDAMANA NA NA BAADAYE KUFANYA MKUTANO NA POLISI KULINDA HUO MKUTANO JE TUELEWE HAWA CCM NA POLISI LAO MOJA AU? HUU NI UKANDAMIZAJI WA WAZI KABISA
Ccm wanaruhusiwa na hawatakiwi kubughuziwa
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimefungua upya kesi dhidi ya amri ya polisi ya kupiga marufuku maandamano na mikutano ya kisiasa baada ya kuifanyia marekebisho hati ya awali ya mashtaka kwa kuwaondoa baadhi ya washtakiwa.

Mawakili wa Chadema Gasper Mwanaliela, John Mallya na Paul Kipeja waliwasilisha mahakamani hati mpya ya madai kwa kuondoa wadaiwa wawili ili kukidhi mahitaji ya kisheria.

Wadaiwa katika hati mpya ya mashtaka iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Geita na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Awali, washtakiwa wengine walikuwa ni wakuu wa polisi Wilaya za Kahama, Maswa na Kamishina wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi, Nsato Mssanzya

Chanzo:Mwananchi online
Hiyo kesi wameifungua masjala gani muda huu! Machadema kwa kujifurahisha bana!
 
Hujielewi, hata ukishinda mahakamani, polisi watapiga marufuku mikutano yenu tena, sijui mtakimbilia wapi. Huwezi kushindana na DOLA
Unaijua amri ya mahakama wewe au una bweka tu?
 
Unaijua amri ya mahakama wewe au una bweka tu?
Unajua katiba na sheria ya vyama vya siasa wewe? Hata mkipewa ruhusa, OCD ana mamlaka ya kuzuia akiona kuna hali ya sintofahamu! Potezeni muda tu.
 
Ccm wanaruhusiwa na hawatakiwi kubughuziwa
Kama ungeyaona maandamano yao ni lazima ungeshangaa sana ! Ni tukio liloambatana na kujidhalilisha , Mibaba mizima na wa mama eti wanamlilia Meya ambaye yuko hai ! Niliona aibu sana ! Zipo tetesi kwamba kabla ya kuandamana kila mmoja wao alipewa sahani 1 ya wali na Fanta orange 1 take away .
 
Kama ungeyaona maandamano yao ni lazima ungeshangaa sana ! Ni tukio liloambatana na kujidhalilisha , Mibaba mizima na wa mama eti wanamlilia Meya ambaye yuko hai ! Niliona aibu sana ! Zipo tetesi kwamba kabla ya kuandamana kila mmoja wao alipewa sahani 1 ya wali na Fanta orange 1 take away .
Daaaaa wana ccm kwa wali ni sawa na samaki na maji
1466019892955.jpg
 
Back
Top Bottom