Bei ya sukari nchini yashuka kwa Sh,1500

Bei ya sukari nchini yashuka kwa Sh,1500

Acha unafki,we umenunua sukari 1500,au Unakula home hujui hata bei ya chupi?
Nipo home kweli mwezi uliopita nilipotumwa na mzee dukani kununua sukari nilinunua kg 1 kwa Tsh.5000 wiki iliyopita nimenunua kg 1 kwa tsh 2400
 
kwa hiyo 5000-1500=3500/=

Hapa hakuna unafuu wowote.
kama ukiwa na Tsh.5000 mwezi uliopita ulikuwa unaweza kupata kg 1 tu leo ukiwa na Tsh.5000 utapata kg ngapi?? kwamba hapo hamna utofauti mkuu
 
Mnatengeneza matatizo wenyewe halafu mnawalaumu ukawa, sijui huwa mnawaza kwa kutumia makalio.
lilikuwa ni tatizo ambalo watu walizani wanaweza kuiteteresha serikali MUNGU amekuwa mkubwa, kuwa awamu hii si ya kutetemeka
 
Mkuu hesabu uliacha darasa la ngapi? yani wastani wa 2,500 na 5,000 iwe 1,500?
nimeweka bei ya miezi iliyopita
bei ya sukari imepungua kwa Tsh 900 hadi 1500 ikilinganishwa na bei ya sukari kwa miezi 2 iliyopita katika maeneo tofauti
 
Walijua itabaki juu kama majani mtini sasa imeshuka wanaumia as if wanafurahi watanzania kutokunywa chai
 
Hahahaha magazeti bwana yaani wameandika mahesabu yao ili watuvuruge tu tusielewe ukisoma fasta fasta utafikiri wamesema kilo ni 1500 kumbe sio
Na wamevuruga watu kweli kweli [emoji12] [emoji12] [emoji12]

Kaka ...
 
1500 per kg iyo sukari labda imetoka China na imetengenezwa kutokana na chupa za maji zilizotumika
Kaanzia sh 900_1500 nadhani mleta mada kasahau hii ni Tanzania labda habari ni ya Kenya [emoji2] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hakuna sukari ya sh 900 aisee
 
Sasa hiyo bei ya 2500 ndo tuliokuwa tukinunua kabla ya kupanda na kufikia 3500 hebu kuwa serious bana. Kwa kifupi sukari bado ni ghali
 
Imepungua kwa wastani wa kati ya 900 - 1500 kutoka bei iliokuwapo awali ya 3500.
 

Attachments

  • upload_2016-8-11_20-59-5.png
    upload_2016-8-11_20-59-5.png
    50.9 KB · Views: 28
Kaanzia sh 900_1500 nadhani mleta mada kasahau hii ni Tanzania labda habari ni ya Kenya [emoji2] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hakuna sukari ya sh 900 aisee
We unaonekana ni mzito kweli kwenye hesabu hasa za mafumbo, yani kama hesabu ndogo tu ya mtoa post inakushinda kuielewa kweli tuna safari ndefu!
 
Bei ya Sukari nchini imeanza kutengamaa baada ya kushuka kwa wastani wa sh 900 hadi 1,500 kwa kilo kutokana na viwanda kuanza uzalishaji pamoja Serikali kuingiza takribani tani 70,000 kutoka nje ya nchi kufidia upungufu uliyokuwepo.

Utafiti mdogo uliofanywa na gazeti la Mwananchi jijini Dar es Salaam na mikoani unaonesha kiwa sehemu kubwa sukari inauzwa kwa wastani wa sh.2400 kutoka zaidi ya sh.3,500 iliyokuwepo miezi miwili iliyopita.

Kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo kunatoa ahuweni kwa Wananchi wengi waliolazimika kutoboa mifuko yao ili kumudu bidhaa hiyo muhimu katika uandaaji wa vyakula mbalimbali pamoja na chai.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi.

Mkuu una akili zinazofanana na avatar yako. Tueleze kilichopandisha bei ya sukari ghafla toka tshs 1800 mwezi november 2015 hadi 2400/= unayodai ni unafuu ninini?
 
Wapi umeambiwa sukari 1500, kuelewa kazi sana.. Umeambiwa upungufu wa bei ni wastani 1500
Mimi nachoelewa ni kwamba hapo awali tulikuwa tukinunua sukari shilingi 2000 kwa kilo. Baada ya matamko bei imepanda hadi 2300. Vipi hapo, bado sina akili?
 
Back
Top Bottom