TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,870
- 5,755
Bei ya Sukari nchini imeanza kutengamaa baada ya kushuka kwa wastani wa sh 900 hadi 1,500 kwa kilo kutokana na viwanda kuanza uzalishaji pamoja Serikali kuingiza takribani tani 70,000 kutoka nje ya nchi kufidia upungufu uliyokuwepo.
Utafiti mdogo uliofanywa na gazeti la Mwananchi jijini Dar es Salaam na mikoani unaonesha kiwa sehemu kubwa sukari inauzwa kwa wastani wa sh.2400 kutoka zaidi ya sh.3,500 iliyokuwepo miezi miwili iliyopita.
Kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo kunatoa ahuweni kwa Wananchi wengi waliolazimika kutoboa mifuko yao ili kumudu bidhaa hiyo muhimu katika uandaaji wa vyakula mbalimbali pamoja na chai.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi.
Utafiti mdogo uliofanywa na gazeti la Mwananchi jijini Dar es Salaam na mikoani unaonesha kiwa sehemu kubwa sukari inauzwa kwa wastani wa sh.2400 kutoka zaidi ya sh.3,500 iliyokuwepo miezi miwili iliyopita.
Kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo kunatoa ahuweni kwa Wananchi wengi waliolazimika kutoboa mifuko yao ili kumudu bidhaa hiyo muhimu katika uandaaji wa vyakula mbalimbali pamoja na chai.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi.