BBC: Tanzania kuingia uchumi mdogo wa kati wajipange, misaada na mikopo nafuu yote itakoma na haitapata misaada kama zamani na upendeleo wa kifedha

Tatizo sio mada bali ni mleta mada na kusudio la kuleta hii mada.
Mkuu kwa upande wangu sijaona tatizo kubwa la mleta mada. Shetani akikuletea ujumbe mzuri, wewe pokea lakini umwache na ushetani wake. Lengo na kusudi la mleta mada hata kama ni ovu bado kuna ujumbe wa taadhari hapo.
Tunataadharishwa hapo kwamba sasa tumekua, siyo watoto wa kubebwa bebwa tena. Mtoto akishakua kuna vitu anakosa kwa mama yake.
Kama nchi tumepanda daraja ambalo kuna vimisaada na mikopo tutakosa, kwa hiyo lazima tujipange kupambana na hiyo hali. Siyo rahisi sana kama tunavyodhani, lakini ndiyo hivyo mtoto akishaweza kutembea habari ya kubebwa inaisha. Kama nchi ni muhimu kujua hayo
 
Vijana Wa Mbowe kwao mafanikio ya JPM na Tanzania kwao.ni sawa kisu kikiingia ndani ya mtima wanaumia kwelikweli yaani we acha tu
 
Return Of Undertaker,
Hamueleweki, mara mnadai bado tuko daraja lile lile mara misaada itapungua, vijana wa mbowe mna shida sana.
Wewe rafiki ndiye huelewi. Hakuna mpinzani aliyekataa tangazo lililochapishwa na WB ila tunasema harakati za kupanda daraja ki-kipato hapa nchini zimechagizwa na awamu zote za uongozi tangu tupate uhuru. Hazijafanywa na awamu ya tano tu kama watu wengi wananyoaminishwa. "Statistical information shows that income growth rate created by the fifth phase government is smaller than that of the previous phase governments". Na huu ndiyo ukweli. Kubali au ukatae. Matokeo haya ni jumla ya mafanikio yaliyofikiwa na awamu zote za uongozi tangu tupate uhuru. Hongera Nyerere, hongera Mkapa, hongera Kikwete, na hongera Magufuli.
 
Kwa furaha tunayofurahia ndio tujipange kwa sababu maumivu yanayokuja kwa kupanda daraja ni makubwa.

1. Misaada iliyokuwa inapata kama nchi maskini itakatwa
2. Mikopo iliyokuwa inasemwa nafuu itakuwa haipo tena.
3. Mikataba yenye unafuu wa kibiashara itakuwa tofauti ile dhana ya kusaidiwa inaondolewa kwa sababu unajiweza.
4. Misaada kama ya madawa mfano HIV inaweza kuondoleaa ikiwemo na baadhi ya chanjo.

Hivyo tujipange.

Pia soma
- Nini maana ya Tanzania kutangazwa kuwa Nchi ya Uchumi wa Kati (MIC) na Benki ya Dunia?
- News Alert: - Benki ya Dunia yaitangaza Tanzania kuingia rasmi katika orodha ya Nchi zilizo katika uchumi wa kati
Hilo la dawa tulikwishapata ucumbuzi bora zaidi, tutapiga nyungu.
 
yote uko sahihi ila kuongezewa muda Magu hapana mkuu pliz acha mawazo ya kichawi kama hayo! acha kuwaza kibinafsi
Ha haha yaani kusema aongezewe muda nimekuwa MLOZI mweka watu VIZUU....
Sasa huo ubinafsi unatoka wapi komredi wangu?!! Waliofikiria kuweka kipengele cha miaka 5 ili uchaguzi ufanyike walipatia ila wale waliofikiri iwe miaka 4 walikosea?!!

Kwangu Mimi hao wote wako sahihi Kama ilivyo sahihi kwa baadhi ya sisi walalahoi ambao tuna mtazamo tofauti....

UPI HUO?

Nilisuuzika Sana na mh.Ally Kessy mbunge wa Nkasi pale alipoonesha kiu yake ya kutaka ifike siku akiwaona WABUNGE wanajadili uwezekano wa kumuongezea muda mh.Magufuli.

SI UBINAFSI WALA SI UCHAWI

Kama si magufuli Kuna mtu alijua watanzania tutajiamini tena na kutembea kifua mbele kizalendo?!!
Taifa hili halikuwa likielekea kuwa km Kenya?!!

SI siri kuwa vijana wengi wa vyuo vikuu na waliomaliza huko walishakuwa na mentalities za SHORTCUTS katika maisha,wengi walishaiga ama kutaka kuiga kuwa km vijana wa NIGERIA...hv ungewaambia nn wakuelewe na maneno yako mepesi ya UZALENDO Koko huku kila kona ya upeo wa macho yao wanaona shuhuda za MAZONGE yafuatayo;

1.EPA
2.IPTL-ESCROW
3.KAGODA
4.DEEP GREEN
5.MEREMETA
6.TANGOLD
7.TWIGA WATOROSHWAO
8.HUJUMA KTK MABWAWA YA KUZALISHA UMEME
9.UPIGAJI BANDARINI
10.TRA MAPATO HAFIFU
11.MADINI YATOROSHWAYO
BILA SERIKALI KUINGIZA KITU
12.MISHAHARA HEWA
13.WAFANYAKAZI HEWA
14.KUSUASUA KWA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU HESLB
15.VYETI BANDIA VYA ELIMU KILA KONA
16.RUSHWA KUBWAKUBWA NA NDOGONDOGO KUWA km SALA MAISHANI MWETU et cetera

Katika NAKAMA hiyo KIMIUJIZA anatokea "MWAMUZI"..
MWAMUZI wa kutung'oa kutoka MSAMBWENI...wa kutubadilisha mentalities zetu zenye UPOGO atutayarishe kwenda KANAANI....

Wallahi namng'ang'ania....bora aendelee tu kitu gani bwana kwani mi nautaka URAIS niseme ananichelewesha kupigiwa saluti na CDF?!!

All and all watanzania tunajijua kwa ufundi wetu wa maneno mengi kuliko vitendo..

Wa vitendo kapatikana.
Wa vitendo tunaye.

Twendeni na magufuli kiunzi cha 2020.

Tafakari ukiwa RELAXED.
 
Kwa furaha tunayofurahia ndio tujipange kwa sababu maumivu yanayokuja kwa kupanda daraja ni makubwa.

1. Misaada iliyokuwa inapata kama nchi maskini itakatwa
2. Mikopo iliyokuwa inasemwa nafuu itakuwa haipo tena.
3. Mikataba yenye unafuu wa kibiashara itakuwa tofauti ile dhana ya kusaidiwa inaondolewa kwa sababu unajiweza.
4. Misaada kama ya madawa mfano HIV inaweza kuondoleaa ikiwemo na baadhi ya chanjo.

Hivyo tujipange.

Pia soma
- Nini maana ya Tanzania kutangazwa kuwa Nchi ya Uchumi wa Kati (MIC) na Benki ya Dunia?
- News Alert: - Benki ya Dunia yaitangaza Tanzania kuingia rasmi katika orodha ya Nchi zilizo katika uchumi wa kati


China refuses to give up ‘developing country’ status at WTO
 
Wewe rafiki ndiye huelewi. Hakuna mpinzani aliyekataa tangazo lililochapishwa na WB ila tunasema harakati za kupanda daraja ki-kipato hapa nchini zimechagizwa na awamu zote za uongozi tangu tupate uhuru. Hazijafanywa na awamu ya tano tu kama watu wengi wananyoaminishwa. "Statistical information shows that income growth rate created by the fifth phase government is smaller than that of the previous phase governments". Na huu ndiyo ukweli. Kubali au ukatae. Matokeo haya ni jumla ya mafanikio yaliyofikiwa na awamu zote za uongozi tangu tupate uhuru. Hongera Nyerere, hongera Mkapa, hongera Kikwete, na hongera Magufuli.
Nakubaliana na wewe 100%.
 
Mi maisha yanazidi kunichapa ngoja niendelee kutazama labda uchumi wa kati utaninunulia Bajaji!!...
 
Tupo pazuri watanzania tujipongeze kwa kuingia uchumi wa kati kabla ya 2025 ambayo ndio ilikuwa lengo letu.
Sasa vilio vinaanza mapema siku 3 nyuma toka kutangazwa kuwa tumeingia nchi zenye uchumi wa kati.Punde tutaimba lugha moja kuwa baba tenda miujiza.
 
Back
Top Bottom