Ya Bomba la mafuta limewahepa.
Wakati Magufuli anaingia madarakani alikuta Kikwete ametengeneza makubaliano na Wachina ya Kujenga SGR yote Dar hadi hadi Kigoma, na pia kutoka Uvinza kwenda mgodi wa Musongati wa Burundi na kufika Kaliua. Ilikua iende na Mwanza nadhani, kwa mkopo wa $7.6 Bilioni kupitia benki ya China ya EXIM na Kampuni ya Ujenzi ya Reli za serikali ya China. Magufuli aliitupia hii dili nje kwa madai kuwa ilikuwa na harufu ya ufisadi na kwamba tutajenga SGR kwa fedha zetu za ndani.
Sasa leo hii, zaidi ya fedha ambazo tayari tumezamisha kwenye SGR kipande cha Dar hadi Dodoma tu, tumekopa tena $ 1.46 Bilioni ili kukamilisha ujenzi wa SGR toka Dar hadi Makutopola. Hili linafanyika wakati TRC wanasema hadi sasa kipande kilichojengwa kimeshakula $1.3 Bilioni. Hii inamaanisha kwamba tunakopa $ 1.46 Bilioni kukamilisha sehemu ambayo tayari imekula $1.2 Bilioni. Kwa hiyo basi, hadi sasa kuanzia Dar hadi Makutopola gharama inaweza kufikia zaidi ya $3 Bilioni, ambayo ni karibu nusu (50%) ya mkataba ambao Kikwete na Wachina walikuwa watie sahihi kama gharama ya kujenga SGR yote, na Raisi Magufuli akatuaminisha Watanzania kwamba ule mkataba ulikuwa na harufu ya ufisadi.