Kenya walijipanga kwa kujenga majengo ya vituo vyao vya garimoshi vyenye mvuto na nafasi ya kutosha. Hawana tofauti kubwa katika ujenzi huo ukilinganisha na vituo vyetu vilivyojengwa kwenye reli ya TAZARA na hasa Dar es salaam na Kapirimposhi. Vituo vilivyojengwa kwenye reli ya TAZARA pamoja na uzuri wake na nafasi ya kutosha kwa wakati huo, historia imethibitisha kuwa havikuwahi kutumika kama ilivyotarajiwa. Kama kwenye reli mpya wameona umuhimu wa kujenga vituo kulingana na uhitaji, nadhani ni jambo la heri, kuliko kuweka kituo chenye hadhi kubwa na badaaye kutotumika kikamilifu.