Taifa la kibepari hilo wala hawakujali ukombozi wa wenzao. Tanzania ilifadhili Jitihada za ukombozi wa Zimbabwe, Msumbiji, Afrika ya kusini, Namibia na hata comoro juzi tu hapo tulishiriki kuikomboa kwa operation anjouan.
Rais Sam Nujoma wa Namibia wakati anastaafu alikuja Tanzania kushukuru. Hata makao makuu ya ukombozi afrika yalikua Dar es salaam. Hata alipokufa Mandela Tanzania ilipewa nafasi maalumu kumuaga kule kijijini kwao Qunu na kama kawaida yake Kikwete akatoa speech bora kabisa.
Nyerere aliamini kuwa si jambo la kupendeza Sisi kujiona huru wakati ndugu zetu wa kusini bado ukoloni unawasumbua. Ndio maana Tanzania pamoja na kuwa Afrika ya mashariki lakini ni mwanachama wa SADC kama heshima ya ukombozi.
kambi za ukombozi yalikua mengi tu ndani ya Tanzania. Saizi yamegeuka shule,mfano shule ya Samora Machel kule Mbeya. Pia campus moja ya SUA imepewa jina la Solomon Mahlangu.
Algeria na Misri zilikua na mchango mkubwa katika ukombozi wa nchi za kusini kuliko Kenya. Walter Rodney na Che Guevara hawakuja Tanzania kimakosa. Achana nao labda history kwao wanasoma maumau tu. Kiukweli bila zile harakati za ukombozi tungekua mbali sana. Hata soo la Uganda liliturudisha nyuma sana.
Asante ichoboy kwa point muhimu sana.