Nimeshangaa hbr clouds TV kuwa ombaomba wameshindikana kuondolewa dsm.
Mtaa wa Libya mwandishi anaonyesha wamama, wabibi na wazee wamejaa kwenye mavaranda wamepumzika usiku baada ya kazi nzito ya kupambana na hali zao kwa njia ya kutuomba pesa (kazi ya kuomba pesa)
Pia watoto kibao wamezagaa utadhani kuna chekechea ya kata mitaa hiyo.
Mkuu
Shindwa madawa
Shindwa usafi
Shindwa viwanda
Shindwa elimu
Shindwa kuonyesha resatislipu
Shindwa kupeleka yard za magari kigamboni
Ila hawa jamaa kuwarudisha dodoma (wengi wamesema wanatokea huko hasa bahi ) nakushauri utumie mbinu za mtaka RC kukimbiza mwizi kimyakimya sisi wapitanjia tufaidi matokeo tu hata tusipokuona na kukukusikia tutajua ni wewe maana tulikusikia uliposema hutaki kuwaona jijini kwako.