Yaani nimeshangaa sana mkuu kama vile anatumwa sijui, ili kumpumbaza mama kwamba anafanya kazi vizuri halafu huko baadaye mambo yaharibike akishika tama mwenyewe hawatakuwepo wala kuwa naye, wanataka kumletea stress mama yetu.
Watu wanakwenda ofisini hawashughulikiwi wakiuliza wanaambiwa mpigieni simu Magufuli aje awasaidie si ndiye aliwazoesha hivyo. Sasa unajiuliza ina maana uongozi huu hauogopwi?
Watu wa chini ndio wanajua shida na ndio wengi wanaoumia na ndipo palipo na mtaji wa wapiga kura hata mzee Kinana anaujua umuhimu wake viongozi wa shina na mitaa.
Eti tunalialia humu , kwani viongozi humu hawapiti na kuona au yeye hajui taarifa zinakusanyw vipi mpaka zifike huko juu. Kwamba za kusifia tu ndio zinafika ila zinakosoa hazitakiwi.
Mkuu ngoja tu nyamaze.