Kiungani
JF-Expert Member
- Feb 2, 2007
- 274
- 71
Sishangai Rage na hata wengine kufanya hivyo. Hilo ni suala la muda tu, na wengine wengi sasa watafanya hivyo hivyo pia.
Wakati umiliki wa silaha za moto unaruhusiwa na Mkapa na genge lake akina Mapuri na Mahita, watu walisema sana kuhusu hili. Wenye uwezo wa kumiliki silaha ndiyo hao hao tayari wanalindwa na jamhuri au usalama wao hauko hatarini kama siye wa uswazi.
Wanaishi kwenye maeneo bora, nyumba zao zina nondo hadi madirisha ya chooni, wanazungukwa na kuta za futi 14 zenye nyembe juu, wana walinzi ndani na nje ya kuta hizo, sehemu zao za kazi na biashara pia 'ulinzi' ni wa juu. Pia ni hao hao ndiyo wanaotuambia na kutuimbia kila siku kuwa nchi yetu chini ya CCM na serikali yake, ni nchi ya AMANI na UTULIVU.
Je, ni usalama gani wanautaka kwa kumiliki silaha katika AMANI na UTULIVU wote huo?
Ni wazi kuwa huo usalama wanaoutafuta ni dhidi ya wananchi wao wenyewe. Na ni kwa nini wawaogope wananchi wao, wapiga kura wao, wenye AMANI na UTULIVU ulioletwa na CCM na serikali yake kwa miaka yote hii?
Watu wa Asia ya Mashariki (East Asia) wana msemo kuwa ukitaka kumpika chura usimuweke kwenye maji ya moto, ataruka. Unamweka kwenye maji baridi, unawasha moto chini ya sufuria, na maji yanavyozidi kupata uvuguvugu chura hawezi kuona tofauti na kujua kuwa moto unaongezeka. Taratibu anaiva. Ila wewe mpishi, unajua maji ni ya moto na unafunika mikono yako kabla hujaepua sufuria.
Tanzania tuliwekwa kwenye maji baridi, na kidogo kidogo maji yameishakuwa vuguvugu au ya moto (EPA, Richmond, Meremeta, Kiwira, Barick, Kahama Mines, Dowans, Deep Green, Tangold, Mbolea/Matrekta Kilimo Kwanza, BOT Twin Towers, Rada, Ndege ya Rais. MV Victoria, MV Spice Islander, Mbagala, Gongo La Mboto, n.k.), na waliotufikisha hapa ndiyo hao wanafunika mikono yao (bastola kibindoni, nyumbani au kwenye magari yao) ili wasiungue wakati wanaopoa chura.
Wakati umiliki wa silaha za moto unaruhusiwa na Mkapa na genge lake akina Mapuri na Mahita, watu walisema sana kuhusu hili. Wenye uwezo wa kumiliki silaha ndiyo hao hao tayari wanalindwa na jamhuri au usalama wao hauko hatarini kama siye wa uswazi.
Wanaishi kwenye maeneo bora, nyumba zao zina nondo hadi madirisha ya chooni, wanazungukwa na kuta za futi 14 zenye nyembe juu, wana walinzi ndani na nje ya kuta hizo, sehemu zao za kazi na biashara pia 'ulinzi' ni wa juu. Pia ni hao hao ndiyo wanaotuambia na kutuimbia kila siku kuwa nchi yetu chini ya CCM na serikali yake, ni nchi ya AMANI na UTULIVU.
Je, ni usalama gani wanautaka kwa kumiliki silaha katika AMANI na UTULIVU wote huo?
Ni wazi kuwa huo usalama wanaoutafuta ni dhidi ya wananchi wao wenyewe. Na ni kwa nini wawaogope wananchi wao, wapiga kura wao, wenye AMANI na UTULIVU ulioletwa na CCM na serikali yake kwa miaka yote hii?
Watu wa Asia ya Mashariki (East Asia) wana msemo kuwa ukitaka kumpika chura usimuweke kwenye maji ya moto, ataruka. Unamweka kwenye maji baridi, unawasha moto chini ya sufuria, na maji yanavyozidi kupata uvuguvugu chura hawezi kuona tofauti na kujua kuwa moto unaongezeka. Taratibu anaiva. Ila wewe mpishi, unajua maji ni ya moto na unafunika mikono yako kabla hujaepua sufuria.
Tanzania tuliwekwa kwenye maji baridi, na kidogo kidogo maji yameishakuwa vuguvugu au ya moto (EPA, Richmond, Meremeta, Kiwira, Barick, Kahama Mines, Dowans, Deep Green, Tangold, Mbolea/Matrekta Kilimo Kwanza, BOT Twin Towers, Rada, Ndege ya Rais. MV Victoria, MV Spice Islander, Mbagala, Gongo La Mboto, n.k.), na waliotufikisha hapa ndiyo hao wanafunika mikono yao (bastola kibindoni, nyumbani au kwenye magari yao) ili wasiungue wakati wanaopoa chura.