Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Niliwahi kupanda iringa - Mwanza gari ilkuwa fikoshi au premier(nimesahau).
Ila yote yalikuwa yanaongozana halafu yote miyeyusho.
Sitasahau, nilisimama kutokea iringa mpaka nimefika Singida ndio nikapata siti.
Magari ya Mwanza to Mbeya miyeyusho sana.
 
Mombasa raha ,Mwanza Bukoba...Konda Msukuma Dah! Ongea yake sasaa aaasee ndo ilikua mara yangu ya kwanza kuwasikia wakiongea Hawa watu🤣🤣 Toka Tanga mie.Yaahee! Nilikua Kila aaikiongea na ntizama Wacha animaindiii🤣🤣🤣
 
Kwanini mabasi yenye kunguni Ni ya KIGOMA, BUKOBA, MUSOMA, MWANZA na GEITA TU.
Huku Arusha, TANGA, Moshi huwezi kukuta kunguni hata kwenye ngwalangwala Kama Kilimanjaro express?
Why Kanda ya ziwa tu.
 
Tawakal nilipandia Iringa kuja Dar na mbaya zaidi nilikaa pale next na dereva..yaani pale kitonga miaka hiyo ya 2000 jamaa alikuwa ananyonga kona akiwa na speed ya 80 hadi 90 Nilihama siti nikaenda kukaa number 60. Yule Dereva alikuwa na roho gumu sana
 
Libanika
Katarama wakat bado mpya ilipata ajali pale shelilango wakat inatoka asubuhi ndipo tukaambiwa abiria wa katarama tunapandishwa libanika weeee jamaniii jamaniiii sitasahauu nilifika kesho yake alfajiri mwanza mwili umechoka miguu imevimba Sina hali
 
Kuna basi nilipanda kutoka ifakara to Dodoma, aise gari ndani Lina mifugo mingi kuliko abiria, just imagine mtu anapanda ndan ya bus amebeba mbuzi na kuku ndan ya gari,,kilicho niboa zaid nimelala usingiz kuja kushtuka nashangaa mbuzi ananilamba nywele.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Mbavu zangu
 
Back
Top Bottom