Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Enzi hizo bus linaitwa Sawaya kutoka Dar to Arusha, lilikuwa miyeyusho sana pamoja na nguguye Kilimanjaro truck ambayo kwa sasa hivi ndo hii kampuni Kilimanjaro Express (nina imani sasa hivi ni kampuni bomba aka imejipata)
 
Majinja enzi hizo from mbeya to dar aisee sitasahau. Mvua kubwa ilianza kunyesha morogoro mikumi pale gari zima linavuja abiria tunaloa hakuna pa kujificha Tunashuka ubungo pale watu tumeloa chapa watu wanatushangaa mpaka mabegi yameloa. Ni moja ya tukio baya nililowahi kumbana nalo maishani sitawasahau wale washenzi eti wanomba radhi aisee nilitamani nilipue lile bus
 
Majinja enzi hizo from mbeya to dar aisee sitasahau. Mvua kubwa ilianza kunyesha morogoro mikumi pale gari zima linavuja abiria tunaloa hakuna pa kujificha Tunashuka ubungo pale watu tumeloa chapa watu wanatushangaa mpaka mabegi yameloa. Ni moja ya tukio baya nililowahi kumbana nalo maishani sitawasahau wale washenzi eti wanomba radhi aisee nilitamani nilipue lile bus
 
Siku moja nilipanda klm Arusha kwenda Dar Kwa ajili usaili ndio kipindi magari ya luxury yameingia na bei kuliko ya kawaida, tulipofika machame mzee mmoja na wife wake akaingia alionekana anamkwara Sana na anamfahamu mmiliki na hata anaweza kumpigia..alikuwa anawapigia mkwara Sana wale wahudumu
Sasa muda si muda akaingia chooni na akarudi naye mke wake akaenda mara ooh watu wanaanza kulalamika harufu Kali kumbe Yule mama anashusha kubwa chooni aisee gari ilikuwa inanuka hatari AC ni kama zinasambaza Tu harufu Ndani Ile harufu ilikuwa Kali sijui ni nn alikuwa amekula safari ilikuwa mbaya Sana madirisha yakafunguliwa yote ni upepo mpaka dar
 
Nilikomaa, nilivyofikaa nilimchamba mwenyeji wangu!!
Nkamuambia afanye ahame kulee, bus lina kungunii lile sijawahi ona kabisaa wallah. Lol
We nawe utakua ulipenda bei kitonga😂
 
Premier ya mwanza mbeya, ile takataka imesababisha niwe na kituo dodoma kama naenda mwanza. Napanda shabiby hadi dom nalala asubuhi napanda satco.
 
Bus ya kuitwa Shukurani Dar - Dom hata kama imebaki yenyewe sipandi.
Bus ya kuitwa Fikoshi sipandi bora niahirshe safari.
Fikoshi nimepanda juzi sina hamu nalo,nilitoka mwanza kwenda njombe nikashukia makambako, yaani sina hamu hata liwe limebaki peke yake duniani bora nikaahirisha safari nimekoma mno. Mbaya zaidi nilisafiri na watoto siti imeharibika unafanya kuinyanyia acha tuu
 
Jina nimesahau ila ni route ya Dar to Musoma, jamanii lile bus ni chakavu afu lina kungunii balaaa. Asee niliteseka hatariii sirudii tenaa.

Ilikua 2017
Mjukuu ulikwenda Musoma kufanya nini? Halafu ukanipita hapa Lamadi hata bila kunisalimia kha! Safari nyingine usifanye hivyo! Na pole kwa masaibu yaliyokupata!
 
Premier ya mwanza mbeya, ile takataka imesababisha niwe na kituo dodoma kama naenda mwanza. Napanda shabiby hadi dom nalala asubuhi napanda satco.
Kwa hiyo route Premier ndio mbabe.
 
  1. Nyehunge kero ni kelele ya muziki usiku wa safari nzima huwezi kuongea na simu, huwezi kusikiliza redio yako
  2. Al Saidy wamefunga maspika ya disco ndani ya mabasi yao huwezi kuongea na simu, huwezi kusikiliza redio yako
 
Kilimanjaro express ya Dar- Tunduma sjui kama bado wanaenda hii route.
 
Back
Top Bottom