Nifah
JF-Expert Member
- Feb 12, 2014
- 34,411
- 82,338
Hadi umenikumbusha story yangu na mimi ya adha ya usafiri wa mabasi, zipo 2 ila hii ilikuwa kali zaidi.Sai Baba, nilikuwa natoka Arusha kwenda Dar. Usiku kabla ya safari nililala late sana, nikayachelewa mabasi ya mapema.
Hapo ndiyo nikakutana na hicho chuma, nikakikwea. Nadhani ndiyo kilikuwa kinatoka body, kilikuwa bomba sana.
Ila kilipoanza kutembea tu, fasta nikagundua kuwa nimeyatimba.
Hiyo ilikuwa ni miaka mingi sana iliyopita, so sijui sasa mabasi yao yakoje, ila tangu wakati huo hayo mabasi sina mpango nayo.
Ova
Ilikuwa safari ya Dar Arusha nikachelewa kidogo kufika Ubungo magari yameshaondoka mengi likawa limebaki Osaka, hapo saa mbili asubuhi. Picha linaanza gari likaondoka pale saa 5, niliteseka sana njiani gari halitembei linasimama kila mahali kuokoteza abiria.
Tulifika Arusha saa 6 usiku, na nilikuwa binti mdogo wa miaka 20 ilibidi mama anisubiri usiku wote huo stendi peke yake.
Tokea hiyo siku mimi na mama tuliapa kutokupanda Osaka maisha yetu yote, ni bora tuahirishe safari.