Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Kuna basi nilipanda kutoka ifakara to Dodoma, aise gari ndani Lina mifugo mingi kuliko abiria, just imagine mtu anapanda ndan ya bus amebeba mbuzi na kuku ndan ya gari,,kilicho niboa zaid nimelala usingiz kuja kushtuka nashangaa mbuzi ananilamba nywele.
😂😂😂 Huu ushirikina sasa
 
Sijaona comment kwa Route za Dar TANGA
Dar Arusha
TANGA Arusha
Huku Ni ustaarabu
Thubutu
Nilioanda SIMBA MTOTO
nilitaka Tanga saa 10 jioni
Nikafika UBUNGO saa 1 ASUBUHI
Wenyeji wakaniambia siku nyingine usipande Hilo
Tatizo ndo lilikuwa ndo gari ya mwisho
Ratco ilijaa ilikuwa 2015
 
Chuma moja ya kishamba Kumotco kwenda Iringa, nikachelewa kuboard Begi kwenye buti mafuta yakavujia kwenye nguo sabab ya joto kali 😤😤
 
Kuna kampuni ilikuwa inaitwa spider au taqwa, route yake dar-arusha-nairobi-busia-kampala. Gari zao zilikuwa zote ni Nissan diesel, chuma cha route nzito. Pia zilikuwa na route ya Dar tunduma. Zile chuma zipo slow kama malory, kwenye milima ndio usiseme. Chuma ilikuwa inabeba mizigo nyuma. So kila tukikaribia wanapopima uzito, abiria nusu wanashushwa, nusu wanasogea mbele ili bus libalance uzito maana nyuma kuna mizigo. Ilinyesha mvua, kila upande majanga. Wachache sana hayakuwakuta. Tulitoka dar 12asubuhi, tukaingia Nairobi sa8usiku. Mgongo unawaka moto.
 
Ha

ha haaa. Hili lina mlango wa katikati sio mkuu?.

Niliwahi panda toka Mbeya nikashukia Singida. Wenyeji walinishangaa jinsi nimetumia muda mwingi kufika.

Zile socket kama za nyumbani nahisi unaweza hata nyoa ndevu huku gari linatembea kama una mashine ya umeme.
Yeah mjanja alinipenyezea kuwa ni kampuni ya sumry inajaribu kujikusanya tena.
 
Kuna kipindi nilikuwa babati, hivi yale mabasi ya kwenda dongobesh, hydom huwa yana hali gani maana kwa kulitizama nje tu linatisha mwendo sasa km zombi yani nilikuwa najiuliza vitu vingi sana
 
Sai Baba nilipandia tunduma wakipiga debe kwamba ya mwisho tulipofika uyole saa 4 asubuhi tukafaulishiwa kwenye coaster tukakaa hadi saa 9 alasiri wale jamaa wa hovyo sana.
 
Bwana kuna chuma kinaitwa upendo
Coach

Sijui mmiliki ni msabato siku hiyo dereva na konda wake wakajichanganya wakapiga tukwaya twao kumbe wazee wa kobasi wapo inside the building

Nnachowapendea wana maamuzi magumu wakagombana na dereva na konda mmoja wao akatoa flash akapachika kwenye basi

Tena na basi lilikua bovu mwendo wa kobe ilikua ni mwendo wa kaswida mkipumzika ni mawaidha mkisimama kaswida mkichuchumaa mawaidha mpaka tunafika
Mpaka leo hii mtaani nabishana na watu baadhi ya mafundisho yao kumbe ABC za wazee nilizipata kwenye safari moja tu😂
😅😅😅😅asante nina siku nyingi nimecheka hivi Inasemekana tanzania ni chaneli ya vichekesho inawezekana kweli loh
 
Kunuka samli tena??? Kuna wengine wana panda na mifugo kama Bata, wana waweka chini ya siti, sasa hao Bata wakawa wana mng'ata abiria ambae alikuwa bishoo mmoja kavaa pensi na raba alikuwa siti ya mbele...!
 
Kampuni ya kishenzi sana hii yani Safari kutoka SONGEA mpaka MOSHI lakini hawana USB chargers, dereva wanalala balaa doh!
Kwanza wahudumu wao hasa wadada ni washenzi hatarii, nilicharuana na m1 wakat huo niko advance hatakaa anisahau yulee mbwaaa!! Mxxxxiieeeww!!
 
Back
Top Bottom