Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Abood Tunduma-Dar.
Niliambiwa SEAT ipo nikapanda Mbeya.
Ndani nikakabidhiwa kindoo nikalie,ngoma mpela mpela mpaka moro wakapaki gereji kwao masaa mawili.
Ndani ya bus nilikaa mikao yote inayojulikana.
Nashkuru tulifika salama.
SIPANDI TENA.
 
Kipindi hicho nilipanda MJ safari, gari watu wanakula muda wote, sio mayai ya kuchemsha wala mahindi ya kuchoma, hawachagui hawabagui. Mmoja tunafika Morogoro akajinyea kwenye bus, harufu yake mule ndani haifai. Nilikoma kabisa siku hio.
 
Kuna basi la Mwanza ~ Mbeya (jina kapuni) nilikata ticket ya kukaa upande wa dirishani, siku ya safari nikakuta dirisha la kwenye siti yangu halina kioo...! Yani nilipigwa na upepo Mwanza hadi Iringa...! Ndo mtu akashuka. Sintakaa kusahau...Na konda anasema hajui maana walikuja na basi lingine jana yake wameliacha service wakachukua basi lingine ambalo lilikuwa safi na limesha fanyiwa service.
Ila pia kilicho ni shangaza kuhusu hili basi halikuwa na USB port bali socket kama za nyumbani
 
Kuna basi la Mwanza ~ Mbeya (jina kapuni) nilikata ticket ya kukaa upande wa dirishani, siku ya safari nikakuta dirisha la kwenye siti yangu halina kioo...! Yani nilipigwa na upepo Mwanza hadi Iringa...! Ndo mtu akashuka. Sintakaa kusahau...Na konda anasema hajui maana walikuja na basi lingine jana yake wameliacha service wakachukua basi lingine ambalo lilikuwa safi na limesha fanyiwa service.
Ila pia kilicho ni shangaza kuhusu hili basi halikuwa na USB port bali socket kama za nyumbani
😂😂😂 socket zinafanya kazi?
 
Ni basi gani umewahi kupanda ukajuta kabisa ukasema sitakaa nipande tena hii gari?
Sai Baba, nilikuwa natoka Arusha kwenda Dar. Usiku kabla ya safari nililala late sana, nikayachelewa mabasi ya mapema.

Hapo ndiyo nikakutana na hicho chuma, nikakikwea. Nadhani ndiyo kilikuwa kinatoka body, kilikuwa bomba sana.

Ila kilipoanza kutembea tu, fasta nikagundua kuwa nimeyatimba.

Hiyo ilikuwa ni miaka mingi sana iliyopita, so sijui sasa mabasi yao yakoje, ila tangu wakati huo hayo mabasi sina mpango nayo.

Ova
 
Back
Top Bottom