Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Basi gani la mkoani ulipanda ukajutia?

Gari zote tu ambazo safari zake zina wasukuma,wamangati, wamasai , watu wa tabora , kahama ,shinyanga ,dodoma kwenda kondoa......aisee hizi gari ni hazifai kunguni, chawa, mende ustaarabu zero usiombe ukabahatika kukaa siti moja na wale wavaa mashuka wananuka samli tu muda wote wanalamba ugoro. Kuna bibi mmoja alitema kohozi nje likarudi ndani siti ya nyuma yake likamnata jamaa sikioni.

Hiyo moja kioo cha dirisha hakikuepo makonda walishikilia boks kuziba upepo mwanzo mwisho.

Hizo tripu popote kambi
 
Gari zote tu ambazo safari zake zina wasukuma,wamangati, wamasai , watu wa tabora , kahama ,shinyanga ,dodoma kwenda kondoa......aisee hizi gari ni hazifai kunguni, chawa, mende ustaarabu zero usiombe ukabahatika kukaa siti moja na wale wavaa mashuka wananuka samli tu muda wote wanalamba ugoro. Kuna bibi mmoja alitema kohozi nje likarudi ndani siti ya nyuma yake likamnata jamaa sikioni.

Hiyo moja kioo cha dirisha hakikuepo makonda walishikilia boks kuziba upepo mwanzo mwisho.

Hizo tripu popot
Kunuka samli tena??? Kuna wengine wana panda na mifugo kama Bata, wana waweka chini ya siti, sasa hao Bata wakawa wana mng'ata abiria ambae alikuwa bishoo mmoja kavaa pensi na raba alikuwa siti ya mbele...!🤣🤣🤣
 
Ni basi gani umewahi kupanda ukajuta kabisa ukasema sitakaa nipande tena hii gari?
Nilikata tiketi saa 12 (tukiaminishwa linaondoka saa22.30) kwenda Arusha basi likaondoka saa 5 likiwa na abiria wachache, bwana we njia zima lina simama kusanya sanya. Mbaya zaidi mbele kidogo ya Same likaharibika,tukafika Arusha saa 11 asubuhi wakati mabasi ya kurudi Dar yameshaanza kuondoka.
Ni Tokyo Express 😡
 
Kipindi hicho nilipanda MJ safari, gari watu wanakula muda wote, sio mayai ya kuchemsha wala mahindi ya kuchoma, hawachagui hawabagui. Mmoja tunafika Morogoro akajinyea kwenye bus, harufu yake mule ndani haifai. Nilikoma kabisa siku hio.
Hii ya kujinyea niliwahi kutana nayo kwenye safari flani hivi huyo kaka nilimuhurumia sana
 
Islam => Mbeya to Dar (gari imechoka zaidi ya kuchoka). Tulitoka Mbeya saa 12:00 asubuhi tukafika Mikumi saa tatu usiku. Tukaletewa gari nyingine.


Upendo Express => Mbeya to Mwanza (gari imechoka zaidi ya kuchoka). Tulitoka Mbeya saa 12:00 asubuhi tukafika Iringa saa 12 jioni. Likatengenezwa na Kisha kuendelea na safari. Kabla ya kufika Mtela gari ikaharibika. Tulisubiria masaa sita kuletewa gari nyingine.

Mungu tu ndiye husaidia kufika salama.
 
Back
Top Bottom