Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

Ni posho gani walichukuwa:-

Posho ya vikao sitting allowance

au

Posho ya kujikimu

au

Ni posho zote
 
mnampongeza Zitto kwa lipi na kuwaponda wabunge wengne wa cdm?
Wana Jf sheria za bunge znasema usipoudhuria ktk vikao vya bunge mara tatu mfululizo kuna adhabu itachukuliwa. Zitto hajasaini kitabu cha maudhuria ila mpaka bunge linaisha tarehe 26 hakuchukuliwa hatua. Je ni kweli Zitto hajasaini?
Mbona wauliza swali baada ya kujijibu mwenyewe?
 
Hichi si chama kwa mtazamo wangu ni kuwa kimejaa wanafiki na huyu mzinzi anayewadanganya wa tz hamna chochote kama wapo serious waache kuzichukua na walipe kodi pia kama wanauchungu na nchi
wamejaa porojo tu
 
Mwenyekiti wa CDM alisema wabunge wamekuwa wakilipwa mishahara kwa mwezi pamoja na fedha za kujikimu (per diem) wanapokuwa nje ya majimbo yao yao kikazi na kwamba wanachopinga ni "posho za vikao" (sitting allowance) ambazo ni kikwazo cha utekelezaji wa kazi za serikali na majukumu mengine katika ofisi za umma.

Kwa mfano, mimi ni mjumbe wa kamati ya uongozi (ya bunge), nasaini sitting allowance katika kikao cha bunge, nikiitwa katika kikao cha kamati ya uongozi nasaini tena sitting allowance na hata kama kutakua na kikao kingine jioni naweza kulipwa, sasa kama huo siyo wizi ni nini?


Hauwezi ukaongea maneno haya alafu ukaendelea kuzichukua pesa unazoamini ni za wizi, hapa naungana na Mh. Sitta kuwa hapa Mbowe na Wabunge wenzalke wanaochukua hizo posho ni wanafiki..
 
Mnafiki ni yule ambaye akiongea husema uongo,akiweka miadi hatimizi,na akiaminiwa hufanya hiyana.hawa chadema wanasema uongo kuwa hawapokei posho huku wakiziweka kibindoni?.wanafanyia hiyana wananchi.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
<br />
Mnafiki zaidi ni nani kati ya Chadema ambapo kunatoka Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (alirudisha shangingi), na naibu wake (amekataa posho) au wabunge wa CCM walalao bungeni na kuunga hoja asilimia mia moja? Katibu mkuu Jairo anatoka Chadema? Kahonga wabunge wapitishe bajeti ya wizi.<br />
CCM unafiki mtupu!
<br />
<br />
 
&quot;Katika ilani ya uchaguzi ya chadema ya mwaka 2010,chadema kilikataa posho.Kikawaelekeza wabunge wake wazipinge bungeni.Hatuwezi kuungana na wenzetu wanoziunga mkono&quot;.Alisema Marando.<br />
<br />
Hata hivyo taarifa kutoka ofisi za bunge hadi jana zionasema ni Zito Kabwe pekee ndiye mbunge wa chadema ambayea aliacha kusaini posho huku wengine wote wakitia kibindoni. source Mwananchi.-29/08/2011 page 4 <br />
<br />
UTAWATAMBUA KWA MATENDOOOO..MATENDOO
<br />
<br />
naona Cdm inakuwasha hadi kwenye masaburi mzee!?
 
Jasusi;2423506]Hata ukiangalia ofisi ya bunge imefanya mchezo wa kisiasa kutoa taarifa hii. Ilitaka Chadema waonekane kuwa wanafiki wakati wabunge wengi wa CCM wanapinga kuondolewa kwa posho za wabunge. That should be the issue na wala si unafiki wa Chadema. Sasa suala limegeuka kuwa Chadema badala ya kujiuliza ni kwa nini CCM inashikilia wapewe posho na kwamba hizo posho hazitoshi, ziongezwe
Jasusi;2423506]Hata ukiangalia ofisi ya bunge imefanya mchezo wa kisiasa kutoa taarifa hii. Ilitaka Chadema waonekane kuwa wanafiki wakati wabunge wengi wa CCM wanapinga kuondolewa kwa posho za wabunge. That should be the issue na wala si unafiki wa Chadema. Sasa suala limegeuka kuwa Chadema badala ya kujiuliza ni kwa nini CCM inashikilia wapewe posho na kwamba hizo posho hazitoshi, ziongezwe
Wakuu, Tatizo ninaloliona na mchezo wa siasa unaochezwa na serikali vizuri sana.

Tunakumbuka bunge liliwahi kutoa taarifa kuwa masilahi ya bunge ni siri yao. Inapotoka taarifa kuwa wabunge wote isipokuwa Zitto ni kutoa siri zile zile walizokataa kutueleza kwa kisingizio cha siri za wabunge. Sasa Kwanini taarifa hii imetoka leo?

Tunakumbuka wiki nzima imegubikwa na suala la Jairo hasa jinsi serikali ilivyomkingia kifua na kumdhalilisha Waziri mkuu. Joto ndani ya bunge limekuwa kubwa ingawa makosa yalifanywa na wabunge wenyewe kukasimu kazi zao kwa seriakali na kukataa matokeo.

Hata hivyo jamii imeonekana kuguswa sana na jambo hili na kumweka Rais na Katibu mkuu kiongozi katika wakati mgumu sana wakipingwa na kila kada, wanataaluma,viongozi wa jamii, wastaafu n.k.

Serikali ikachomeka suala la mh Zitto kuchukua rushwa CHC. Zitto akaweka wazi na masharti yaliyomweka Mkulo pagumu. Hoja ikafa.
Wiki hii hii serikali ikashauri suala la Arusha lijadiliwe, CCM kwa kupitia Nape na Mkama wakaligeuza kama tatizo la Chadema.
Sasa wamekuja na hili la posho.

Hii yote ni kutaka ku 'divert' attention ya public kutoka kwa aibu ya Jairo ili mjadala upotee kwa kuchomeka mijadala isiyo na uhusiano.
Tunavyozidi kulijadili kwao ni mafanikio. Let us stick to our guns. Ikulu, PS and Katibu mkuu wamendhalilisha PM. Rais na Katibu mkuu kiongozi wamebofoa! Waseme ukweli waache mambo ya CHC, Posho n.k hayo tunayajua, tunalotaka maelezo ni hili la 'best friend wao Jairo'
 
Wakuu posho ni janga la kitaifa na hakika suala la posho lisipoangaliwa vizuri litaimega CHADEMA. Lakini naona wametumia busara na kuamua kunyamaza na kuzichukua posho kimyakimya. Lakini kwa unafiki wanataka eti kumshughulikia Shibuda kwa kuwa amesema hadharani kwamba yeyey anataka posho kinyume na wenzake ambao wanajifanya hawazitaki huku wanazimung'unya. Hapa kuna unafiki usiomithilika! Kwa hili sitasita kusema kwa kinywa kipana kwamba CHADEMA WAMEKUWA WANAFIKI KUHUSU SUALA LA POSHO. Nipigeni tu mawe lakini nasema.
 
Jamani mtoa mada amesema source ni Mwananchi tarehe 29/08/2011 page 4, lakini hakuna taarifa kama hiyo unless page 4 ziko 2


Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi ni kwamba CHADEMA walishatoa maelezo ya kile wanachopinga. Ni mfumo sio particular transation. Na ilivyo sasa, uki-sign daftari la mahudhurio basi hela zinalipwa moja kwa moja kwenye account yako. Pia nadhani kuna madhara kama wabunge wote wa CHADEMA wangegomea kuto-sign mahudhurio (mwenye uelewa zaidi asaidie hapa tafadhali). Kwa hiyo ili kuondoa tatizo lote walishauri KUNG'OA MTI NA SIO KUKATA MATAWI. Na bunge ndio chombo sahihi cha kutunga sheria.

Nadhani ccm wanaweza kujaribu ku-spin hii lakini kwa kumbukumbu zangu CHADEMA walijaribu sana kupaza sauti za kubalisha hii sheria inayoruhusu posho lakini hawakufanikiwa. Wasiwasi wangu ccm wanaweza kupoteza umuhimu wa huu mjadala kwa kusema kuwa hawa CHADEMA nao wamepokea lakini cha msingi hapa tukumbuke kama hatutajikita kwenye kujadilikubalisha mfumo tutapotea tatizo la msingi.[/QUOTE]
 
kama kweli wabunge wa CDM wamechukua hizo sitting allowance then iam done with politics...kama shibuda amechukua posho zote sina tatizo nalo sababu shibuda ni ccm,..inawezekana hii gutter politics,..ingechukua vichwa vya habari vya magazeti yote..
 
For some reason I just think Zitto is not serious or sincere with this and he is just trying to score some political popularity points.
hata kama zitto anatafuta popularity sisi inatuhusu nini? sisi la mhimu ni kodi zetu zitumike vizuri. Lakini sishengai kwani michango yako yote kwa zitto ni negative siku zote. kwa hiyo thread kama hii ungeachia tu ipite usingepoteza chochote kuliko kuandika utumbo wako hapa. Laslty kwenye politics is always popularity and not otherwise.
 
Siungi mkono Suala la Posho za Wabunge, lakini nafikili hata Zito alipaswa kuchukua hiyo posho, kwa sababu hizo alizoacha zitaenda wapi? nafikili ni vema hizo pesa angechukua na kuzipeleka katika mfuko wa maendeleo kule Mwandiga, kitu ambacho nazani hata waheshimiwa wabunge wa CDM wengine watakifanya. Cha msingi ni kukazania kuhakikisha posho zinaondolewa kisheria.
 
Waitwao ni wengi ila wateule ni wa chache....... (Wameitwa wengi bungeni ila kabaki Zitto peke yake) sasa kama mpaka Mwenyekiti naye???? Ila katika haya bado jamvi hili litumike kulisaidia Taifa na si kutetea maslahi ya vyama manake wanayo yaonesha ndiyo yatakayokuwa watakaposhika nchi hii. Siasa ni upuuzi mtu japo kila kitu na katika maisha ya kila siku lazma ukutane na siasa...... Na bado kuna mengi makubwa tuyatarajie mbeleni miaka mitano ni mingi sana.
 
Watu wengi wamjuao zito watakubaliana nami kwamba..huyu jamaaa ni mpiganaji na mjenga hoja mzuri sana lkn pia anapenda sana umaarufu, kujipendekeza kwa magamba sometimes, na uchu sana na madaraka. In short is a kind of a guy who can change his colors anytime kufanikisha kile anachokitaka huku akijitahidi sana kumaintain his reputation kwa jamii. Kwanza, kuna mwanaJF 1 amesema gazeti la mwananchi limewahi kuandika habari nyingi za kumpamba Zito, anyway sijawhi kufatilia hili. Lkn wakati wa mjadala wa bunge wa bajeti ya EAC zito alikuwa akiilalamikia sana serikali kuhusu kukataa kumpa work permit extension CEO wa gazeti hili mpaka mm nikahisi kuna some sort of interest btn mwananchi na bwana Kabwe. Secondly, wakati akiwasilisha bajeti ya wizara ya fedha ya kambi ya upinzani, Zito alimsifia Makinda kwa kuliendesha bunge vizuri huku akijua wazi wananchi, wanazuoni, wabunge wa upinzani wengi hasa wa CDM, na wa CCM wasio wanafiki wamekuwa wakiponda jinsi mama huyo na wasaidizi wake wanavoendesha bunge hilo.Sasa, just bada ya bunge kuisha..gazeti hili linakuja na habari hii ambayo to some extent in maslahi kwa CCM, inamjenga Zito na inaiponda CDM. Katika mazingira haya niliyohighlight mtu mwenye akili unaweza ukaona kuna mambo mengi and syndicate iliyojificha nyuma ya hii habari.Nikija kwenye issue ya posho..CDM walishaonyesha msimamo kwamba sera yao inakataa posho, lkn kotokana na kanuni maslahi binafsi na kandamizi za bunge kwamba..once you have signed the attendance book lazima utaingiziwa hiyo pesa, na usiposign unachukuliwa kama ni mtoro na hivo kupelekea kupata adhabu ikiwemo kufukuzwa, wabunge wa CDM had a little option but kusign sababu tunahitaji uwakilishi wao. Nataka niwaambie CDM kwa nia nzuri kabisa..mojawapo ya vitu viliovyowapa point ktk bunge lililopita ni swala la posho, lkn ikija kuthibtiika mmechukua hizo posho kimyakimya bila kutoa ufafanuzi wowote kwa wananchi kwamba kwann, ktk misingi gani mlilazimika kuchukua posho na mna mpango gani na hizo pesa ambazo nyie pamoja na ss wananchi wengi wazalendo tunaamini ni haramu, mtakuwa mmetuangusha, mtapoteza imani yenu kwa wanachama wenu na watanzania wanyonge na mtawapa magamba cha kusema kwenye kampeni za IGUNGA. Ninachoomba mm..which I believe watu wengi wenye kuitakia mema nchi hii watakubalina nami: Viongozi waandamizi wa CHADEMA waitishe press conference maramoja kulitolea ufafanuzi jambo hili.
 
Kabla cjajibu hii hoja ya chama chetu au chama changu nisaidieni huyu mleta hoja ninani kama cyo masaburi ninauwakika na wabunge wangu cyo vilazi kama ccm kwanza msipende kuwachafua akina mbowe lema wenje mnyika lissu halima mdee msigwa n.k wewe mleta hoja acha siasa za maji taka hicho chanzo chako kitakuwa cha jeiro na nape na nakitakuwa kina tumia masaburi
 
Back
Top Bottom