Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,395
- 39,531
Kwa: Katibu Mkuu
Chama cha Mapinduzi
Yah: Uamuzi wa Spika wa Bunge kuhusu suala la
Mheshimiwa, Malima (Mb) na Bwana Mengi Mwenyekiti wa
IPP
Suala lilitajwa hapa juu la husika
Mheshimiwa Katibu Mkuu, siku ya tarehe 8 Februari
2007, Mheshimiwa Samwel Sitta (Mb) Spika wa Bunge
aliwasilisha kwenye Bunge uamuzi wake kuhusu suala
hhili lililotajwa hapa juu. katika shauri hilo Spika
wa Bunge alifikia uamuzi kwamba nimeliongopea Bunge
kwa mujibu wa kanuni na 50 ya Kanuni za Bunge. Aidha
amefikia uamuzi kwamba kwa makusudi nililenga
kamuathiri Mengi kwa kumchhonganisha na viongozi wa
kitaifa. Mwisho, katika kukutafuta ufumbuzi wa suala
hili Spika wa Bunge, ameamua kutukutanisha mimi na
Bwana Mengi ili kutafuta suluhu baina yetu kwa
manufaa ya jamii.
Pamoja na kutambua wajibu wangu kama Mbunge kwa Bunge
lenyewe, Spika na Chama changu ninashindwa kuafikiana
na maamuzi haya na utekelezaji wake kw akuwa naona
hayalingani na ukweli wa matamshi yangu Bungeni ya
tarehe 2 Agosti 2006, uamuzi huo haukunitendea haki
kama Mbunge na ulilenga kwa dhahiri kumpendelea Bwana
Mengi, na katika kuufikia ninaamini kwamba haukupatiwa
taratibu za kuufikia ambazo zisingezingatia manufaa ya
Chama, kuliko ulivyo sasa hivi.
Aidha naomba niseme kwamba Spika alipeleka suala hili
mbele ya Kamati ya Bunge ya Kinga, Maadili na Madaraka
ya Bunge, ili apatiwe ushauri. Kwa kauli yake mwenyewe
amekiri kwamba kamati haikuniona na kosa lolote,
sikusema uongo na nilikuwa sahihi katika mchango
wangu.
Katika uamuzi wa Spika anasema :
1.1.11 Kabla sijatoa maamuzi yangu, napenda
kuwashukuru kwa dhati Mheshimiwa Mwenyekiti Juma S.
Nhunga na Waheshimiwa wajumbe wote wa Kamati ya Haki,
maadili na madaraka ya Bunge kwa umakini wao na kwa
kutumia utaratibu wa haki katika kuchunguza na
hatimaye kukamilisha kazi yao na kutoa ushauri wao
kwangu. Muda waliotumia na gharama zake visingwezea
kuepukwa.
6.0 TAARIFA NA USHAURI WA KAMATI YA KINGA, MAADILI NA
MADARAKA YA BUNGE
6.1 Baada ya Kamati ya Kinga, Maadili na Madaraka ya
Bunge kukamilisha uchunguzi wake, iliwasilisha taarifa
yake kwangu pamoja na taarifa ya maoni tofauti
(dissenting views) ya wajumbe wake wawili.
6.2 Katika taarifa hiyo, kamati ya kinga, maadili na
maadili na madaraka ya Bunge kamati iliridhika kuwa
Mhe. Adam K. A. Malima (Mb), hakusema uongo ndani ya
Bunge, na kwamba hakukuwa na uthibitisho wowote kuwa
ana maslahi binafsi na kile laichokisema Bungeni.
6.3 Kwa matokeo hayo, kamati ilishauri Bw. Reginald
Mengi aarifiwe kuhusu matokeo hayo ya uchunguzi wa
kamati, na pia Mengi ashauriwe kuwa makini katika
matumizi ya vyombo vya habari, hasa vile
anavyovimiliki.
6.4. Aidha, kamati ilishauri kuwa, Mhe. Malima ajibiwe
maombi yake ya Mwongozo wa Spika kuwa, alipokuwa
anachangia Bungeni tarehe 2 Agosti, 2006, alikuwa
sahihi kulingana na misingi ya Katiba, Sheria na
Kanuni za Bunge, na kwamba, akipenda afuate taratibu
zaidi za kisheria, kwa kuwa, kushambulia mchango wa
mbunge mmoja mmoja wakati anatekeleza majukumu yake ya
kikatiba si halali na mhusika wa kutenda kosa hilo
anaweza kushtakiwa mahakamani.
Baadae katika Uamuzi huo huo anasema;
7.2.7 Matokeo hayo ya uchunguzi wa kamati hiyo ya
Bunge yanaonesha wazi kuwa matamshi ya Mhe. Malima
hayakutimiza masharti niliyoyataja kwenye aya ya
5.4.2.1 hapo juu, yaani kwamba, yamevunja na kukiuka
masharti na matakwa ya Kanuni ya 50 (1) ya kanuni za
Bunge (Toleo la 2004) ambayo, pamoja na mambo mengine
inapiga marufuku Mbunge yeyote kusema uwongo Bungeni.
7.2.8 Kwa uelewe mzuri, kanuni hiyo inatamka kwamba:-
Ni marufuku kabisa kusema uwongo Bungeni. Kwa sababu
hiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni,
atawajibika kuwa na hakika kwamba, maelezo anayoyatoa
ni sahihi, na siyo mambo ya kubuni au ya kubahatisha
tu; 17
mheshimiwa Katibu Mkuu hapa utaona wazi kwamba pana
mgongano wa matamshi. Kwanza spika anasema kamati
imefanya kazi makini iliyozingatia taratibu, pili
anasema kamati ambayo inafanya maamuzi yake kwa mujibu
wa taratibu imeamua kwa wingi yaani consensus kwamba
sikufanya kosa lolote, tatu, kwenye 7.2.7 anasema tena
uchunguzi wa kamati hiyo hiyo, unaonyesha wazi kwamba
matamshi yangu yamekiuka kanuni na (50). Kwa maana hii
licha ya kazi ya makini ya gharama kubwa ya kamati ya
haki, maadili na madaraka Spika ameona maoni na
maamuzi ya kamati hayakao sahihi, isipokuwa kauli za
ushauri tofauti za Mheshimiwa Ole Sendeka ambaye
alikuwa kwenye kamati na alipata nafasi ya kuniuliza
maswali yake yote aliyekusudia, na Anne Kilango
Malecela ambaye amewasilisha pia ushauri tofauti wa
kamati hali ya kwamba yeye hakuhudhuria kabisa vikao
vya kamati hata siku moja kwa muda wa wote ambao mimi
na mashahidi wengine wote tulihudhuria na kuhojiwa na
kamati na hivyo nashindwa kuelewa Spika amepokea vipi
ushauri tofauti wa mjumbe ambaye hakuwepo kabisa.
Mheshimiwa Katibu Mkuu, hivyo basi kwa kuzingatia haya
niliyoeleza hapa juu naomba nisema yafuatayo;
(i) Sikubaliani na uamuzi huo wa Spika wa Bunge wa
kufikia maamuzi kwa tafsiri ya taathira
(interpretation by implication of statement) hali ya
kwamba matamshi yangu Bungeni yako wazi na hayahitaji
kupewa tafsiri ya taathira, na pia sikubaliani na
uamuzi huo ambao umefanywa kwa msingi wa vilelezo au
vigezo ambavyo sivyo vilivyotumika kwenye kamati na
wala havikuzingatia msingi wa hoja.
(ii) Spika ametumia Kanuni na 4(2) kufanya maamuzi
yake. Lakini kanuni ya Bunge 88 (1), (3), (5), (6),
(7), (9), na (11) zinaweka utaratibu wa uwazi wa
kupokea taarifa ya kamati ya kudumu na kuiwasilisha
kwa Bunge ili ijadiliwe na iridhiwe na Bunge. Spika
kwa sababu ambazo hakuoainisha hakuona umuhimu wa
kuruhusu mjadala wa Wabunge kwa suala lenye uzito wa
namna hii na badalå yake akaona busara yake pekee yake
itatosha kuamua masuala nyeti ya kinga na haki za
wabunge. Hivyo sielewi kwanini hakutumia utaratibu wa
utawala bora na demokrasia ya kibunge (good
governance and parlmentary democracy) unaotuamulia
masuala mengine yote ya kamati na ya Bunge kila siku.
(iii) Sheria ya haki, kinga na madaraka ya Bunge, 1988
haisemi kwamba sisi kama Wabunge ni bora kuliko
wananchi, na tuko juu ya sheria. Bunge lenyewe ndilo
lililotunga sheria hiyo na sisi Wabunge ndiyo
tunawajibika mwanzo kuiheshimu. Ama kwa upande wangu
sikusema hivyo wala sikusema jambo lolote ambalo kwa
taathira linaweza likatafsiriwa hivyo, na hivyo sielei
kwanini Spika ametumia mifano ya kuonyesha kwamba
matamshi yangu yamevukia mipaka ya kinga kama
kumsingizia Padri ujambazi wakati wa kulinganisha
suala hili.
(iv) Suluhu ni muafaka unaotafutwa kwa kuridhia pande
mbili baada ya kubainika tofauti zao na chanzo cha
tofauti hizo, na ambayo (suluhu hiyo) inalenga
kuepusha hatari ya pande hizo mbili kuendelea kugombea
na kuleta athari kwa wengine wasiokuwa wao au hata
pamoja na wao. Mimi sina ugomvi na Mengi na nimelisema
hilo na nimelirudia kwenye kamati mara kadhaa.
Nilikuwana tatizo na makadiro ya wizara na kama ni
ugomvi basi itakuwa baina yangu na Waziri, Mhesh.
Muhammad Seif Khatib kwa kuwa nilikuwa nimekusudia
kuzuia mshahara wake. Baada ya kupata maelezo na
kutosheka kama ulikuwa ugomvi basi huo ulishamalizika
bila ya kuhitaji kupatanisha. Ugomvi wa Mengi labda ni
wake kwangu mimi.
(v) Ni imani yangu kwamba kama kwa mujibu wa Spika
suala hili lilikuwa linashamirisha makundi
yaliyochomoza ambayo yameonekana kuibua masuala ya
udini, rangi na tofauti za kipato katika jamii, na
kwa kuwa mimi sikuona ushahidi wowote wa kuunga mkono
suala hili la makundi ndani ya kamati, ndani ya Bunge
na kwa kuwa mimi ni Mbunge wa jimbo wa Chama ambacho
hakikubaliani na matabaka ya aina yoyote yale, na
mwanajamii ndani ya jamii ya watanzania, siridhiki na
maelezo hayo yaliotumika kama kigezo cha kutafuta
suluhu.
(vi) Kwa kiasi kikubwa haya yote yanahusu Wabunge wa
CCM kwani ndio tulio wengi ndani ya Bunge (asilimia
85), na kamati ya Maadili ina wabunge 13 wa Chama
chetu kati ya jumla ya wabunge 15. Kwamba Wabunge
wawili na Spika mwenyewe hawakuona sababu ya kuleta
jambo hili linalotuanika hadharani, kwenye utaratibu
mzuri ambao ndio unajenga mshikamano na umoja miongoni
mwetu, ni j ambo la kushangaza na ambalo linanipa
mashaka makubwa. Kwa kuwa sijaona taarifa ya kamati
kwa Spika, ya ushauri tofauti (dissenting views) za
Waheshimiwa Ole Sendeka na Anne Malecela, siko tiyari
kuukubali uamuzi wa Spika ambao kama alivyosema msingi
wake ni dissenting views hizo.
Mheshimiwa nawasilisha uamuzi wangu wa kuukataa uamuzi
Spika wa kuhudhuria kikao cha usuluhisho na Mengi.
Badala yake, na kwa kuwa suala hili sas linahusu
viongozi wawili, mmoja mjumbe wa kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama, na mwingine Mbunge
wa CCM nawasilisha suala hili kwako ili lipatiwe
ufumbuzi ndani ya taratibu za uongozi wa Chama cha
Mapinduzi, ambao ninaamini uongozi una busara pana ya
viongozi wenye ujuzi na uzoefu wa kufanya maamuzi
yenye kuzingatia maslahi ya Chama chenyewe na Taifa
kwa ujumla.
Mheshimiwa Katibu Mkuu, ninaambatanisha taarifa yangu
yenye vielelezo ya matokeo ya ndani ya Kamati ambayo
ndiyo Waheshimiwa Ole Sendeka na Anne Malecela
walitumia wakati wanawasilisha maoni yao kwa Spika.
Ninaamini yataonyesha bila ya kuhitaji tafsiri za
taathira kwamb mijadala ndani ya kamati ilikuwa ya
uwazi na ambayo ilizingatia taratibu zote, na hivyo
kulikuwa hakuna haja ya Spika kupuuzia ushauri
aliyepewa na wengi na kuchukua maamuzi ya wachaçhe
ambayo yanaonekana yametawaliwa na misingi ya ubinafsi
kinyume na maadili, heshima na nidhamu ya wabunge wa
Chama cha Mapinduzi.
Kanuni za Kamati ya Wabunge wa CCM;
9(a). Kila mjumbe binafsi wa kamati ya Chama anapaswa
wakati wote ule ambapo anakuwa Mbunge, ahakikishe
kwamba tabia yake na mwenendo wa maisha yake kwa
ujumla haukiletei aibu na fedheha au kukipaka Chama
matope.
Mheshimiwa Katibu Mkuu, nawasilisha nasubiri muongozo
wa Chama.
Naomba kuwasilisha,
Kidumu Chama cha Mapinduzi
Nakala kwa
Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi
Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa, Mb
Mweyekiti wa Kamati ya Wabunge wa CCM Waziri Mkuu
Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni
Mheshimiwa Ali Ameir Mahommed, Mb
Katibu
Kamati ya Wabunge wa CCM.
Mwisho.
Chama cha Mapinduzi
Yah: Uamuzi wa Spika wa Bunge kuhusu suala la
Mheshimiwa, Malima (Mb) na Bwana Mengi Mwenyekiti wa
IPP
Suala lilitajwa hapa juu la husika
Mheshimiwa Katibu Mkuu, siku ya tarehe 8 Februari
2007, Mheshimiwa Samwel Sitta (Mb) Spika wa Bunge
aliwasilisha kwenye Bunge uamuzi wake kuhusu suala
hhili lililotajwa hapa juu. katika shauri hilo Spika
wa Bunge alifikia uamuzi kwamba nimeliongopea Bunge
kwa mujibu wa kanuni na 50 ya Kanuni za Bunge. Aidha
amefikia uamuzi kwamba kwa makusudi nililenga
kamuathiri Mengi kwa kumchhonganisha na viongozi wa
kitaifa. Mwisho, katika kukutafuta ufumbuzi wa suala
hili Spika wa Bunge, ameamua kutukutanisha mimi na
Bwana Mengi ili kutafuta suluhu baina yetu kwa
manufaa ya jamii.
Pamoja na kutambua wajibu wangu kama Mbunge kwa Bunge
lenyewe, Spika na Chama changu ninashindwa kuafikiana
na maamuzi haya na utekelezaji wake kw akuwa naona
hayalingani na ukweli wa matamshi yangu Bungeni ya
tarehe 2 Agosti 2006, uamuzi huo haukunitendea haki
kama Mbunge na ulilenga kwa dhahiri kumpendelea Bwana
Mengi, na katika kuufikia ninaamini kwamba haukupatiwa
taratibu za kuufikia ambazo zisingezingatia manufaa ya
Chama, kuliko ulivyo sasa hivi.
Aidha naomba niseme kwamba Spika alipeleka suala hili
mbele ya Kamati ya Bunge ya Kinga, Maadili na Madaraka
ya Bunge, ili apatiwe ushauri. Kwa kauli yake mwenyewe
amekiri kwamba kamati haikuniona na kosa lolote,
sikusema uongo na nilikuwa sahihi katika mchango
wangu.
Katika uamuzi wa Spika anasema :
1.1.11 Kabla sijatoa maamuzi yangu, napenda
kuwashukuru kwa dhati Mheshimiwa Mwenyekiti Juma S.
Nhunga na Waheshimiwa wajumbe wote wa Kamati ya Haki,
maadili na madaraka ya Bunge kwa umakini wao na kwa
kutumia utaratibu wa haki katika kuchunguza na
hatimaye kukamilisha kazi yao na kutoa ushauri wao
kwangu. Muda waliotumia na gharama zake visingwezea
kuepukwa.
6.0 TAARIFA NA USHAURI WA KAMATI YA KINGA, MAADILI NA
MADARAKA YA BUNGE
6.1 Baada ya Kamati ya Kinga, Maadili na Madaraka ya
Bunge kukamilisha uchunguzi wake, iliwasilisha taarifa
yake kwangu pamoja na taarifa ya maoni tofauti
(dissenting views) ya wajumbe wake wawili.
6.2 Katika taarifa hiyo, kamati ya kinga, maadili na
maadili na madaraka ya Bunge kamati iliridhika kuwa
Mhe. Adam K. A. Malima (Mb), hakusema uongo ndani ya
Bunge, na kwamba hakukuwa na uthibitisho wowote kuwa
ana maslahi binafsi na kile laichokisema Bungeni.
6.3 Kwa matokeo hayo, kamati ilishauri Bw. Reginald
Mengi aarifiwe kuhusu matokeo hayo ya uchunguzi wa
kamati, na pia Mengi ashauriwe kuwa makini katika
matumizi ya vyombo vya habari, hasa vile
anavyovimiliki.
6.4. Aidha, kamati ilishauri kuwa, Mhe. Malima ajibiwe
maombi yake ya Mwongozo wa Spika kuwa, alipokuwa
anachangia Bungeni tarehe 2 Agosti, 2006, alikuwa
sahihi kulingana na misingi ya Katiba, Sheria na
Kanuni za Bunge, na kwamba, akipenda afuate taratibu
zaidi za kisheria, kwa kuwa, kushambulia mchango wa
mbunge mmoja mmoja wakati anatekeleza majukumu yake ya
kikatiba si halali na mhusika wa kutenda kosa hilo
anaweza kushtakiwa mahakamani.
Baadae katika Uamuzi huo huo anasema;
7.2.7 Matokeo hayo ya uchunguzi wa kamati hiyo ya
Bunge yanaonesha wazi kuwa matamshi ya Mhe. Malima
hayakutimiza masharti niliyoyataja kwenye aya ya
5.4.2.1 hapo juu, yaani kwamba, yamevunja na kukiuka
masharti na matakwa ya Kanuni ya 50 (1) ya kanuni za
Bunge (Toleo la 2004) ambayo, pamoja na mambo mengine
inapiga marufuku Mbunge yeyote kusema uwongo Bungeni.
7.2.8 Kwa uelewe mzuri, kanuni hiyo inatamka kwamba:-
Ni marufuku kabisa kusema uwongo Bungeni. Kwa sababu
hiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni,
atawajibika kuwa na hakika kwamba, maelezo anayoyatoa
ni sahihi, na siyo mambo ya kubuni au ya kubahatisha
tu; 17
mheshimiwa Katibu Mkuu hapa utaona wazi kwamba pana
mgongano wa matamshi. Kwanza spika anasema kamati
imefanya kazi makini iliyozingatia taratibu, pili
anasema kamati ambayo inafanya maamuzi yake kwa mujibu
wa taratibu imeamua kwa wingi yaani consensus kwamba
sikufanya kosa lolote, tatu, kwenye 7.2.7 anasema tena
uchunguzi wa kamati hiyo hiyo, unaonyesha wazi kwamba
matamshi yangu yamekiuka kanuni na (50). Kwa maana hii
licha ya kazi ya makini ya gharama kubwa ya kamati ya
haki, maadili na madaraka Spika ameona maoni na
maamuzi ya kamati hayakao sahihi, isipokuwa kauli za
ushauri tofauti za Mheshimiwa Ole Sendeka ambaye
alikuwa kwenye kamati na alipata nafasi ya kuniuliza
maswali yake yote aliyekusudia, na Anne Kilango
Malecela ambaye amewasilisha pia ushauri tofauti wa
kamati hali ya kwamba yeye hakuhudhuria kabisa vikao
vya kamati hata siku moja kwa muda wa wote ambao mimi
na mashahidi wengine wote tulihudhuria na kuhojiwa na
kamati na hivyo nashindwa kuelewa Spika amepokea vipi
ushauri tofauti wa mjumbe ambaye hakuwepo kabisa.
Mheshimiwa Katibu Mkuu, hivyo basi kwa kuzingatia haya
niliyoeleza hapa juu naomba nisema yafuatayo;
(i) Sikubaliani na uamuzi huo wa Spika wa Bunge wa
kufikia maamuzi kwa tafsiri ya taathira
(interpretation by implication of statement) hali ya
kwamba matamshi yangu Bungeni yako wazi na hayahitaji
kupewa tafsiri ya taathira, na pia sikubaliani na
uamuzi huo ambao umefanywa kwa msingi wa vilelezo au
vigezo ambavyo sivyo vilivyotumika kwenye kamati na
wala havikuzingatia msingi wa hoja.
(ii) Spika ametumia Kanuni na 4(2) kufanya maamuzi
yake. Lakini kanuni ya Bunge 88 (1), (3), (5), (6),
(7), (9), na (11) zinaweka utaratibu wa uwazi wa
kupokea taarifa ya kamati ya kudumu na kuiwasilisha
kwa Bunge ili ijadiliwe na iridhiwe na Bunge. Spika
kwa sababu ambazo hakuoainisha hakuona umuhimu wa
kuruhusu mjadala wa Wabunge kwa suala lenye uzito wa
namna hii na badalå yake akaona busara yake pekee yake
itatosha kuamua masuala nyeti ya kinga na haki za
wabunge. Hivyo sielewi kwanini hakutumia utaratibu wa
utawala bora na demokrasia ya kibunge (good
governance and parlmentary democracy) unaotuamulia
masuala mengine yote ya kamati na ya Bunge kila siku.
(iii) Sheria ya haki, kinga na madaraka ya Bunge, 1988
haisemi kwamba sisi kama Wabunge ni bora kuliko
wananchi, na tuko juu ya sheria. Bunge lenyewe ndilo
lililotunga sheria hiyo na sisi Wabunge ndiyo
tunawajibika mwanzo kuiheshimu. Ama kwa upande wangu
sikusema hivyo wala sikusema jambo lolote ambalo kwa
taathira linaweza likatafsiriwa hivyo, na hivyo sielei
kwanini Spika ametumia mifano ya kuonyesha kwamba
matamshi yangu yamevukia mipaka ya kinga kama
kumsingizia Padri ujambazi wakati wa kulinganisha
suala hili.
(iv) Suluhu ni muafaka unaotafutwa kwa kuridhia pande
mbili baada ya kubainika tofauti zao na chanzo cha
tofauti hizo, na ambayo (suluhu hiyo) inalenga
kuepusha hatari ya pande hizo mbili kuendelea kugombea
na kuleta athari kwa wengine wasiokuwa wao au hata
pamoja na wao. Mimi sina ugomvi na Mengi na nimelisema
hilo na nimelirudia kwenye kamati mara kadhaa.
Nilikuwana tatizo na makadiro ya wizara na kama ni
ugomvi basi itakuwa baina yangu na Waziri, Mhesh.
Muhammad Seif Khatib kwa kuwa nilikuwa nimekusudia
kuzuia mshahara wake. Baada ya kupata maelezo na
kutosheka kama ulikuwa ugomvi basi huo ulishamalizika
bila ya kuhitaji kupatanisha. Ugomvi wa Mengi labda ni
wake kwangu mimi.
(v) Ni imani yangu kwamba kama kwa mujibu wa Spika
suala hili lilikuwa linashamirisha makundi
yaliyochomoza ambayo yameonekana kuibua masuala ya
udini, rangi na tofauti za kipato katika jamii, na
kwa kuwa mimi sikuona ushahidi wowote wa kuunga mkono
suala hili la makundi ndani ya kamati, ndani ya Bunge
na kwa kuwa mimi ni Mbunge wa jimbo wa Chama ambacho
hakikubaliani na matabaka ya aina yoyote yale, na
mwanajamii ndani ya jamii ya watanzania, siridhiki na
maelezo hayo yaliotumika kama kigezo cha kutafuta
suluhu.
(vi) Kwa kiasi kikubwa haya yote yanahusu Wabunge wa
CCM kwani ndio tulio wengi ndani ya Bunge (asilimia
85), na kamati ya Maadili ina wabunge 13 wa Chama
chetu kati ya jumla ya wabunge 15. Kwamba Wabunge
wawili na Spika mwenyewe hawakuona sababu ya kuleta
jambo hili linalotuanika hadharani, kwenye utaratibu
mzuri ambao ndio unajenga mshikamano na umoja miongoni
mwetu, ni j ambo la kushangaza na ambalo linanipa
mashaka makubwa. Kwa kuwa sijaona taarifa ya kamati
kwa Spika, ya ushauri tofauti (dissenting views) za
Waheshimiwa Ole Sendeka na Anne Malecela, siko tiyari
kuukubali uamuzi wa Spika ambao kama alivyosema msingi
wake ni dissenting views hizo.
Mheshimiwa nawasilisha uamuzi wangu wa kuukataa uamuzi
Spika wa kuhudhuria kikao cha usuluhisho na Mengi.
Badala yake, na kwa kuwa suala hili sas linahusu
viongozi wawili, mmoja mjumbe wa kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama, na mwingine Mbunge
wa CCM nawasilisha suala hili kwako ili lipatiwe
ufumbuzi ndani ya taratibu za uongozi wa Chama cha
Mapinduzi, ambao ninaamini uongozi una busara pana ya
viongozi wenye ujuzi na uzoefu wa kufanya maamuzi
yenye kuzingatia maslahi ya Chama chenyewe na Taifa
kwa ujumla.
Mheshimiwa Katibu Mkuu, ninaambatanisha taarifa yangu
yenye vielelezo ya matokeo ya ndani ya Kamati ambayo
ndiyo Waheshimiwa Ole Sendeka na Anne Malecela
walitumia wakati wanawasilisha maoni yao kwa Spika.
Ninaamini yataonyesha bila ya kuhitaji tafsiri za
taathira kwamb mijadala ndani ya kamati ilikuwa ya
uwazi na ambayo ilizingatia taratibu zote, na hivyo
kulikuwa hakuna haja ya Spika kupuuzia ushauri
aliyepewa na wengi na kuchukua maamuzi ya wachaçhe
ambayo yanaonekana yametawaliwa na misingi ya ubinafsi
kinyume na maadili, heshima na nidhamu ya wabunge wa
Chama cha Mapinduzi.
Kanuni za Kamati ya Wabunge wa CCM;
9(a). Kila mjumbe binafsi wa kamati ya Chama anapaswa
wakati wote ule ambapo anakuwa Mbunge, ahakikishe
kwamba tabia yake na mwenendo wa maisha yake kwa
ujumla haukiletei aibu na fedheha au kukipaka Chama
matope.
Mheshimiwa Katibu Mkuu, nawasilisha nasubiri muongozo
wa Chama.
Naomba kuwasilisha,
Kidumu Chama cha Mapinduzi
Nakala kwa
Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi
Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa, Mb
Mweyekiti wa Kamati ya Wabunge wa CCM Waziri Mkuu
Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni
Mheshimiwa Ali Ameir Mahommed, Mb
Katibu
Kamati ya Wabunge wa CCM.
Mwisho.