Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Ni mawazo mazuri kabisa.
Sasa nani atakaye badili mfumo huu na kuusuka upya ??

Sisi wananchi ni lazzima tuanzishe midahalo ya makusudi katika kila mikusanyika yetu ya kawaida.
Dar kuna mikutano mingi sana binafsi 95%++++ ni ya Harusi Kitchen Party au aina yeyote ile ya kuselebuka na ujivuni kwamba pochi ipo.
Ni wakati sasa wa kuanza kuwa na mikutano ya kujadili mabadiliko ya kweli jijini Dar.
Sivyo, tusitarajie chochote kutoka kwa wanasiasa wetu. Wengi njaa na choyo nicho kimewapelekea kuwa wanasiasa.

MIMI na WEWE tukikaa pamoja jioni baada ya kuwa kwenye foleni ndefu na kuvinjari jiji chafu tunafanya nini katika kutoa mchango wetu??

Mwenendo mzima wa jiji la Dar ni reflection ya mawazo na vitendo vya wana Dar wenyewe.
Hakuna mwana Dar asiyechangia UOVYO wa JIJI la DAR.

Vurugu ziliziopo Dar es Salaam ni kushindwa kwa mfumo wa uongozi,inabidi kutengeneza mfumo mpya! Dar imeelemewa na foleni za barabarani, uchafu,ujenzi holela,makelele yasiyo ratibiwa kutoka ktk nyumba za Ibada,Bar na Kumbi za Starehe,ujambazi,ukosefu wa maji safi na salama,miundombinu ya majitaka,nk! Lakini kuna watu wengi kuanzia RC,DCs,Wakuregenzi wa Manispaa,Mameya,nk ambao wanalipwa lakini hawana kazi ya maana wanafanya!
 
Wanajenga kwa muda mrefu sana, ingekuwa wachina wangekuwa washamaliza.. Rushwa inaliangamiza TAIFA HILI
 
Pro-Chadema kupinga kila kitu Strabarg wanafanya kazi mazingira yanawasumbua.

Mkuu hii aibu ya huu mradi jijini Dar si suala la kisiasa.
Ni dhahiri kuna avery big failure mahali fulani katika utekelezaji wa mradi.

Actually ni ujinga kufumua barabara za nusu ya jiji bila kuwa na mikakati ya utekelezaji.

Tumeona huko nyuma miradi tuliyosaidiwa kufikiri chini ya msaada wa JICA shirika la maendeleo la Japan.
Kulikuwa na DRIMPI , DRIMPII na kuendelea ambapo barabara za Mwinyi(Bagamoyo),Kawawa ,Morogoro Rd zote zilijengwa kwa awamu bila kuleta usumbufu kwa wakazi wa jiji.

Mshangao wangu na wengi ni hso JIJI kutoelewa somo lile.
 
Vurugu ziliziopo Dar es Salaam ni kushindwa kwa mfumo wa uongozi,inabidi kutengeneza mfumo mpya! Dar imeelemewa na foleni za barabarani, uchafu,ujenzi holela,makelele yasiyo ratibiwa kutoka ktk nyumba za Ibada,Bar na Kumbi za Starehe,ujambazi,ukosefu wa maji safi na salama,miundombinu ya majitaka,nk! Lakini kuna watu wengi kuanzia RC,DCs,Wakuregenzi wa Manispaa,Mameya,nk ambao wanalipwa lakini hawana kazi ya maana wanafanya!

Lini mutahama Dar??? Lini wansiasa watagundua kwamba Tanzania siyo Dar? Tanzania siyo Bagamoyo?
Wakati barabara hiyo inapangwa kujengwa idadi ya watu wa Dar ilikuwa ~4 mil. itakapokwisha dar itakuwa na 5+ mil. Je sababu inajulikana. Je CCM wanaamini iko siku wa-TZ wote tutaishi Dar?

Mimi nina akili timamu na ninaamini kwamba Tanzania ni zaidi ya Dar. Siyo akili hata kidogo kila kitu kujengwa Dar. Tunakopa pesa ili tujenge Dar badala ya kujenga nchi nzima. Barabara-Dar, Hospitali ya rufaa-Dar, bandari-Bagamoyo, vyuo vya kijeshi- Bagamoyo (siyo tena Monduli). Sasa hata mashamba ya maembe na michungwa ni Bagamoyo tu!

Itafikia wakati hata vinyesi vibichi vitazagaa ikulu.
 
When you type fast this thing do happen all the time. Sisi tunaelewa and we dont mind. Tunajali hoja. Sasa wengine hawaoni hoja wanaangalia spelling! Ndiyo tofauti zetu

nimeangalia hoja na spelling, ukumbuke kiandikwacho hapa ni kumbukumbu,usiwe kama wale wanaojificha kwenye kichaka cha MFUMO MBOVU,hata mimi nikikosea nisahihishe na huo ndo uungwana
 
Lini mutahama Dar??? Lini wansiasa watagundua kwamba Tanzania siyo Dar? Tanzania siyo Bagamoyo?
Wakati barabara hiyo inapangwa kujengwa idadi ya watu wa Dar ilikuwa ~4 mil. itakapokwisha dar itakuwa na 5+ mil. Je sababu inajulikana. Je CCM wanaamini iko siku wa-TZ wote tutaishi Dar?

Mimi nina akili timamu na ninaamini kwamba Tanzania ni zaidi ya Dar. Siyo akili hata kidogo kila kitu kujengwa Dar. Tunakopa pesa ili tujenge Dar badala ya kujenga nchi nzima. Barabara-Dar, Hospitali ya rufaa-Dar, bandari-Bagamoyo, vyuo vya kijeshi- Bagamoyo (siyo tena Monduli). Sasa hata mashamba ya maembe na michungwa ni Bagamoyo tu!

Itafikia wakati hata vinyesi vibichi vitazagaa ikulu.

Ni kweli Tanzania ni kubwa sana na wala si Dar kama baadhi ya viongozi/watawala wetu wanachukulia. Lakini kuna ukweli Dar ni kioo cha nchi yetu! Tunazungunzia kufail kufikia viwango kwa project moja kubwa itakayo swinda kiasi kikubwa cha pesa za walipa kodi wa Tanzania.

Mchana wa leo nilikua najiuliza,hivi ktk kipindi tunapowaza kwamba pengine matatizo ya aina hii ni kama laana utawala wa nchi hii kwanini wasiombe ushauri kwa akina Charles Keenja na Makamishina wenzake ktk iliyokuwa Tume ya Jiji ambayo ilifanya kazi kubwa na hata yale yaliyofikiriwa hayawezekani??
 
sure,barabara ya sasa ni nyembamba

nikipitaga najuulizaga kwanini wamejenga hivyo.?
1:ni vipi hayo mabasi yaendayo kasi yatakuwa.?
2: na kama basi hayo yatakuwa zaidi ya 1 vipi yatapishana.?
3:nakama yapo zaidi ya mmoja,vipi mmoja wapo litakapo halibika litawapisha wenzi.?
mmmmmh ngoja nimuombe mungu hatuonyeshe kutakavyokuwa....!?
 
STRABAG wanajua kutoa 10% ndo maana tumewapa tena barabara ya Segera mpaka Same kukarabati. Endeleeni kutoa povu tu. Jinga sana nyie mnataka tukale wapi? Lami lami kwenu kuna lami? Au ndo umeikuta Dar. Pombavu kabisa. Tusibirini 2025 ndo mupaange jinsi ya kujenga zenu.
watu kama wewe, kwa hakika, ni janga!
 
Kwa hakika suala hili halina itikadi na hivyo lijadiliwe kwa busara na sio ushabiki. Ukweli unabakia kuwa tatizo si la Strabag bali la serikali kwa kuwa na watendaji wanaotanguliza maslahi binfsi (10%).

Kwa maoni yangu binafsi barabara ya mabasi haijawahi kuwa sulihisho la msongamano wa magari katika karne ya 21. Magufuli anafahamu hivyo, Prof Tibaijuka anakiri hiyvo na mkuu wao (tuliyempa kazi kusimamia maendeleo) amekubali "bora liende".

Kwa maoni yangu upanuzi wa barabara kuu sambamba ujenzi wa flyovers tano, kwa uchache zingemaliza tatizo la msongamano. Maeneo ya makutano yaliyoko Mapipa, Tazara, ubungo changombe na Moroko ndiyo yangewekewa flyovers na barabara husika kupanuliwa; msongamano Dar ungekuwa umeisha kama si kupunguzwa sana.

Maslahi ya 10% yanazuia maendeleo ya ukweli katika nchi hii. Tunshitsji mabadiliko ya ukweli ili kuleta maendeleo.
 
Back
Top Bottom