Ogah Ngojeni niwapatie kioja kingeni cha Mhe Magufuli. hivi sasa Benki ya Dunia inafadhili mradi uitwao Southern Africa Trade and Transport Facilitation Project (SATTFP), mradi huu ndio umetoa fedha za kufanya ukarabati barabara ya Km150 kabla ya kuingia Iringa hadi Iringa, Iringa- Mafinga na sasa Mafinga-Igawa.
Mradi huu lengo lake ni kukuza biashara na sekta usafirishaji katika nchi za kusini mwa Afrika. Nilitegemea mradi kama huu ungeanza na ukarabati wa barabara ya Dar-Chalinze ili kuunganbisha bandari ya Dar es Salaam na nchi hizo. Lakini kwa kuwa Mhe Magufuli alikwisha udangany umma kuwa waliojenga pembezoni mwa barabara ya Morogoro ni wavamizi wa barabara na Benki ya Duni haitaki kusikia poroja za aina hiyo ameishi kutumia fedhaq za mradi huo kujenga mizani ya Vigwaza tu na kuacha barabara ya Dar-Chalizne ikitafutiwa mwekezaji wa Build-Operate-Transfer.
Ni kwanini tuhangaike na BOT ilihali WB ipo tayari kutukopesha? Ni kwa sababu Mhe Magufuli anataka kulinda heshima tu.