Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Huu mradi mimi mwenyewe siuelewi, ujenzi gani miaka kadhaa hauishi, nchi inaongozwa na watu wasio fikiri, huo mradi hauna maana kwa sasa, kwani suala la foleni litabaki palepale.
 
nimeangalia hoja na spelling, ukumbuke kiandikwacho hapa ni kumbukumbu,usiwe kama wale wanaojificha kwenye kichaka cha MFUMO MBOVU,hata mimi nikikosea nisahihishe na huo ndo uungwana

Mkuu aliyeelewa contribution yangu, ameielewa hata bila masahihisho.
Kwa wenye ugumu wa kuelewa ,post imesahihishwa mahsusi kwa faida yako.
Tujadili basi content.
 
Ukienda nairobi kuna barabara moja inaitwa 'thika road' imejengwa na inapitisha magari 10 yaani 10 lane,matano kila upande.ukienda dar inakuta wameweka unused area katikati ya barabara yenye usezo wa kuchukua magari 4 ila eneo hilo limepandwa ukoka,unapanda ukoka katikati ya barabara??? stupidness
 
hadi 2015 ifike kimara mtauza magari yenu chezea strabag wewe..
 
Hii nchi ni kama haina mwenyewe.sijui kama viongozi wetu hawaoni haya?mi pia imenikuta leo hii unatumia saa moja na nusu kutoka mbezi ubungomfano mzuri pale Kimara mwisho kuna kona hatari sana.sijui akina Magufuli na kelele zao hawaoni au wanasubiri waseme wakati wa kukabidhiwa barabara hii.maana zile kona tayari inasemekana watu washakufa.

Pili hii ni highway.kufungua line moja pale kimara ni adhabu kwa wananchi.hata hiyo line ina mahandaki makubwa na kuzidisha kero. Swali langu kwa wahusika hamuoni hili kwa sababu huwa mnakuwa na escorts ya police au sababu mnapita angani? Its not fair kwanza leo ni weekend kwa nini watufungie barabara?
 
Ritz hii haina itikadi?kwani so called ccm wanapita wapi?ungekuwa kwenye hii foleni leo nadhani usingesema hivyo
 
Ritz hii haina itikadi?kwani so called ccm wanapita wapi?ungekuwa kwenye hii foleni leo nadhani usingesema hivyo

Katika hili Ritz si uongo yuko offline.
Barabara hizi za Brt/Dart we ita upendavyo, mamlaka husika zimechemsha,utafikiri shule zote walizoenda hazina maana.
 
Katika hili Ritz si uongo yuko offline.
Barabara hizi za Brt/Dart we ita upendavyo, mamlaka husika zimechemsha,utafikiri shule zote walizoenda hazina maana.

Ukweli Mamlaka husika zimechemka tusonge mbele vipi? Kwa kiwango kikubwa makosa haya yatahamia ktk barabara nyingine kadri awamu za mradi huu zinavyo tekelezwa!
 
Keeping all your eggs in one busket!!!! Mtawapaje miradi mingi hivyo wakati hakuna hata mmoja waliomaliza kwa ufanisi. Ubora haupo angalia ujenzi wao tu. Tutaimba.
 
Ni kweli Tanzania ni kubwa sana na wala si Dar kama baadhi ya viongozi/watawala wetu wanachukulia. Lakini kuna ukweli Dar ni kioo cha nchi yetu! Tunazungunzia kufail kufikia viwango kwa project moja kubwa itakayo swinda kiasi kikubwa cha pesa za walipa kodi wa Tanzania.

Mchana wa leo nilikua najiuliza,hivi ktk kipindi tunapowaza kwamba pengine matatizo ya aina hii ni kama laana utawala wa nchi hii kwanini wasiombe ushauri kwa akina Charles Keenja na Makamishina wenzake ktk iliyokuwa Tume ya Jiji ambayo ilifanya kazi kubwa na hata yale yaliyofikiriwa hayawezekani??

Mkuu Dar haiwezi kuwa kioo cha nchi. hili ni jiji linalokuwa kwa ustaarabu wa kijijini. wengi wanatoka vijijini na kuhamia wakiwa na kuku, mbuzi, ngombe, choo cha shimo, ndala, n.k. jiji gani duniani watu wanaamshwa na jogoo anayewika?

Ukiona kiongozi anaomba ushauri, fahamu huyo ana akili timamu. Nchi zilizoendelea ni lazima rais awatumie washauri. Sisi ni kama akipenda na bahati mbaya hawapendi.

uonavyo kuna dalili ya kiongozi mwenye akili. Hiyo hali ya kuweka hata vibaka maofisini ukawaita mawaziri inaleta picha gani? Mtu anashindwa hata kugundua nani anaweza kumpa msaada wa maamuzi ktk wizara fulani, na hapo ni baada ya kutumia mwezi mzima akiwa kimya, sisi tukidhani anafikiria kupata watu makini!
 
Huu mradi wa dart ni majanga.

Nadhani wanadarisalama tu wavumilivu sana. Usumbufu wanaoleta hawa jamaa, ilibidi wapigwe faini ya kufa mtu watie akili.
 
Subiri mradi ukamilike ndipo uweke lawama zako,nani alikumbia mradi huu ni wa kupunguza foleni?foleni zitapungUa kwa kitu kinaitwa multiplier effect ambayo siyo guarantee ya moja kwa moja.kuwepo kwa njia maalum ya mabasi manake watu watasafiri kwa haraka zaidi kufika wanakoenda kwa kuwa mabasi yatapita njia maalum.foleni inaweza kupungua kwa kuzingatia kuwa mradi wa mabasi utaondoa madaladala njiani ambayo kwa sasa idadi yake ni kubwa.na watu wengine watapaki magari yao na kutumia public transport.kifupi unachotakiwa kuargue ni kama baada ya mradi huu kukamilika mtu akitoka kimara kuja posta ataendelea kutumia masaa matatu?njia za kupunguza msongano ambazo ziko ambazo nnazojua mimi ni kujenga fly overs ubungo na tazara na tayari serikali ya japani imeshakubali kugharamia.ujenzi wa feeder roads kama ile ya goba mbezi hadi kinyerezi,kimara hadi chuo kikuu.,ujenzi wa pantoni toka mjini kuelekea bagamoyo ambapo kutakua na vituo vinne mpaka bagamoyo ujenzi wake unakamilika katikati ya mwaka huu,daraja la kigamboni nk.tusikatishe tamaa wale wanaojaribu kwa sababu binafsi au za kiasiasa!
 
Huu mradi wa dart ni majanga.

Nadhani wanadarisalama tu wavumilivu sana. Usumbufu wanaoleta hawa jamaa, ilibidi wapigwe faini ya kufa mtu watie akili.
Uwezekano ni mkubwa kuwa hawana kosa lolote ila makosa yako kwenye serikali yetu. Watu wengi hawajui au kutambua; lakini mradi huu umetudhalilisha sana sana sana! Tunaonekana kama wendawazimu fulani. Magufuli kafanya nini na makelele yake? Nothing! Wakubwa wetu hawapiti barabara hizi: wao wanapita selander bridge tu na kuingia oysterbay wakitumia V8 tulizozilipia kwa jasho na damu yetu!
 
Kibaya zaidi jamaa wanafanya kazi with minimum supervision, hayo yote ni makosa ya msimamizi wa mradi (consultant) ambae ni smec international maana yeye ndo kazi yake kumsimamia mkandarasi
 
.......

Mradi kama huo wa DART una wadau lukuki wakiwemo:-
  • Serikali ya Tanznaia (Client) wajibu wake ni kuonyesha ardhi na kuandaa mazingira ya kutekeleza mradi kwa mujibu wa mikataba na sheria za kimataifa na sio tunavyotaka sisi watanzania.
  • Benki ya Dunia (Financier) mtoa fedha, anayetoa fedha kwa masharti yaliyomo ndani ya mikataba.
  • Consultant wajibu wake kutayarisha mchoro wa ujenzi, gharama za mradi, kutangaza tenda ili kupata wakandarasi mbali mbali.
  • Strabag Contactor mjenzi kazi yake ni kujenga kilichomo katika michoro tu.

Hivyo masahibu yote yanayotukuta si wajibu wa Mjenzi bali ni wajibu wa Serikali yenu ambayo imeshindwa kuandaa mazingira mazuri ya utekelezaji wa mradi huo. Ni dhahiri kuwa kuandaa mazingira ya utekelezaji wa mradi huo huchukua muda mrefu sana.

Waziri Kawambwa alipokuwa Waziri wa Ujenzi alikuwa akitekeleza mradi huo kwa mujibu wa sheria za kimataifa na hivyo kuandaa mazingira mazuri ya utekelezaji wake kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Lakini alipoletwa Mhe Magufuli kuwa Waziri wa Ujenzi akataka kumuonyesha kuwa mwenzie hajui kazi akamachukua Mkandasarasi yaani Strabag na kumuingiza site kichwa kichwa pasipo kuilipa Tanesco na DAWASA fidia ili waondoe nguzu na umeme na mabomba ya maji.

Matokeo yake ni mkandarasi kuanza kazi na kukuta kuwa hawezi kutengeneza diversion kwa sababu nguzu za umeme na mabomba ya maji havikuondolewa. Nani wa kumluamu? Ni Strabag au sisi wenyewe kwa utendaji wetu wa kibabe?.

Jana Kibonde alikuwa anahoji kwanini Strabag hafanyi kazi usiku? Haya mambo hayaendeshwi kienyeji. Wakati wa kujaza tendi ndipo mkandarasi anaoanisha gharama zake na muda wa kumaliza kazi kwa mujibu wa sheria za ajira za kimataifa na nchi husika. Hivyo kuwafanyisha wafanyakazi kazi usiku lazima kuna cost implications zake za kuwalipa wafanyakazi overtime, gharama za umeme mafuta ya generator n.k ambavyo mkandarasi hakitarajia wakati anajaza tenda na kushinda kwa kuwa alijua atafanya kazi katika mazingira ya kila mdau kutimiza wajibu wake ikiwemo Serikali kuilipa fidia Tanesco na Dawasa fidia ili waondoe mabomba nguzo za umeme ili babarabara za diversion zoiweze kutengenezwa na kila kitu kwenda kama kilivyotarajiwa.Ni mara ngapi tumesikia Mhe Magufuli akilumabana msemaji wa Tanesco Nd Badra Masudi kuhusu TaNESCO KULIPWA FIDIA ILI WAONDOE NGUZO ZA UMEME?

Asante Mkuu kwa maelezo yako......

..........Mradi kama huo wa DART una wadau lukuki wakiwemo:-
  • Serikali ya Tanznaia (Client) wajibu wake ni kuonyesha ardhi na kuandaa mazingira ya kutekeleza mradi kwa mujibu wa mikataba na sheria za kimataifa na sio tunavyotaka sisi watanzania.
  • Benki ya Dunia (Financier) mtoa fedha, anayetoa fedha kwa masharti yaliyomo ndani ya mikataba.
  • Consultant wajibu wake kutayarisha mchoro wa ujenzi, gharama za mradi, kutangaza tenda ili kupata wakandarasi mbali mbali.
  • Strabag Contactor mjenzi kazi yake ni kujenga kilichomo katika michoro tu.

...Unaweza kuongezea Supervising Consultant, Utility Companies, Government Office responsible for Acquisition and Compensation (kwa sababu hili suala laweza kuwa likiendelea wakati mradi unaendelea).......

............Hivyo masahibu yote yanayotukuta si wajibu wa Mjenzi bali ni wajibu wa Serikali yenu ambayo imeshindwa kuandaa mazingira mazuri ya utekelezaji wa mradi huo. Ni dhahiri kuwa kuandaa mazingira ya utekelezaji wa mradi huo huchukua muda mrefu sana.....

...Wajibu wa Ujenzi na consequences zake zinahusu wahusika wote....labda kama kuna specifics responsibilities........ambazo huwa defined either at design stage of before starting of the project (i.e. during negotiations)......pia wakati mwingine haya maswaibu yanaweza kutatuliwa following regular site meetings.....


.........Waziri Kawambwa alipokuwa Waziri wa Ujenzi alikuwa akitekeleza mradi huo kwa mujibu wa sheria za kimataifa na hivyo kuandaa mazingira mazuri ya utekelezaji wake kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Lakini alipoletwa Mhe Magufuli kuwa Waziri wa Ujenzi akataka kumuonyesha kuwa mwenzie hajui kazi akamachukua Mkandasarasi yaani Strabag na kumuingiza site kichwa kichwa pasipo kuilipa Tanesco na DAWASA fidia ili waondoe nguzu na umeme na mabomba ya maji.....

Miradi ya Ujenzi Mikubwa kama hii....kwa kawaida kunakuwepo na ofisi inaitwa Project Execution/Implementation Unit.....mara yingi miradi inayofadhiliwa na World Bank, IMF, EU, AfDB, UN etc hizi unit huwa ni loan contract requirement......unit hizi (ambazo kwa kawaida hutakiwa kusheheni wataalamu wa kada mbali mbali za ujenzi) hu-coordinate mambo yote yahusuyo mradi on behalf of Client.......Kama kweli Magufuli aliingilia kazi ya hii Unit (kama ipo) na alifanya hivyo ulivyosema.....pamoja na mambo mengine.......huyu jamaa ni too "risky" kuwepo Ujenzi.....ni rahis sana kuingizia hasara serikali na kumpa ulaji Mkandarsi kwa maamuzi kama hayo......

nimezimamia sana hizi PEU/PIU mbali mbali katika nchi mbali mbali nikiwa kama Team Leader nikiwakilisha baadhi ya MFIs.....hivyo naelewa challenges zinazoelezewa hapa....na hasa kwenye urban and sub-urban environment kama ilivyo DSM......



..........Jana Kibonde alikuwa anahoji kwanini Strabag hafanyi kazi usiku? Haya mambo hayaendeshwi kienyeji. Wakati wa kujaza tendi ndipo mkandarasi anaoanisha gharama zake na muda wa kumaliza kazi kwa mujibu wa sheria za ajira za kimataifa na nchi husika. Hivyo kuwafanyisha wafanyakazi kazi usiku lazima kuna cost implications zake za kuwalipa wafanyakazi overtime, gharama za umeme mafuta ya generator n.k ambavyo mkandarasi hakitarajia wakati anajaza tenda na kushinda kwa kuwa alijua atafanya kazi katika mazingira ya kila mdau kutimiza wajibu wake ikiwemo Serikali kuilipa fidia Tanesco na Dawasa fidia ili waondoe mabomba nguzo za umeme ili babarabara za diversion zoiweze kutengenezwa na kila kitu kwenda kama kilivyotarajiwa.Ni mara ngapi tumesikia Mhe Magufuli akilumabana msemaji wa Tanesco Nd Badra Masudi kuhusu TaNESCO KULIPWA FIDIA ILI WAONDOE NGUZO ZA UMEME?

......Very TRUE.....Very TRUE!!!!
 
Acha kutetea upumbavu.... Umeshasikia majiji kama London, New York, Paris na Munich watu wanatumia masaa zaidi ya mawili kufika makazini,,,,, yaan watanzania wengine n makondoo ambayo yanaswagwa hata hayajui yanapelekwa wapi? Hiyo barabara ni kichekesho na hakuna sehem yoyote duniani mabasi hayo eti yaendayo kasi yakatengenezewa barabara yake,,, Hilo bus lililoonyeshwa ni sawa na yanayotumka ulaya na yanatumia barabara moja kama magari mengine.... Ni upuuzi mtupu

Tembea uone .... China yanatumia barabara yake ...

Usitoe conclusion as if umetembea dunia nzima
 
....... mamlaka husika zimechemsha,utafikiri shule zote walizoenda hazina maana.

Mkuu....kwa kweli inanishangaza sana sana......kwani wale watu niliofanya nao kazi wengi wao ni wataalamu wazuri sana sana i.e. first world class engineers (e.g Mfugale, Mujwahuzi, Mar Mujungi (RIP), Dr. Mlinga etc)..... ambayo yamenisaidia sana kwenye international organizations nilizofanyia/ninazofanyia kama mshauri.....

.....Nikiwa kwneye mbali mbali kuna kitu kimoja nimekishuhudia.....i.e. Communication and Public Relations katika miradi kama hii......kila wakati Wananchi walikuwa wna kuwa briefed through Information meetings, Radio/TV Presentations.....njia hizo hizo zinatumika sana kutoa taarifa za TRAFFIC MANAGEMENT.......in one country....seven days notice to the public prior ya kuanza kazi sehmu husika na traffic managemeny ni LAZIMA....vinginevyo hakuna kuanza kazi......Mkandarasi analifahamu hilo well in advance (ipo kwenye CoC and Specs) na hivyo hana excuse ya aina yeyote ile ya kuchelewesha mradi.....
 
Acha kutetea upumbavu.... Umeshasikia majiji kama London, New York, Paris na Munich watu wanatumia masaa zaidi ya mawili kufika makazini,,,,, yaan watanzania wengine n makondoo ambayo yanaswagwa hata hayajui yanapelekwa wapi? Hiyo barabara ni kichekesho na hakuna sehem yoyote duniani mabasi hayo eti yaendayo kasi yakatengenezewa barabara yake,,, Hilo bus lililoonyeshwa ni sawa na yanayotumka ulaya na yanatumia barabara moja kama magari mengine.... Ni upuuzi mtupu

Mkuu inaelekea.....hayo majiji uliyoyataja huyafahamu vizuri...labda kama ulipita tu.....i.e..on transit.......na hiyo sentensi yako "highlighted blue".....SIO SAHIHI.......
 
Back
Top Bottom