Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

nkosikazi

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2010
Posts
361
Reaction score
337
Nipo barabarani kutokea kimara kuelekea mjini. Njiani ni balaa tupu kwa sababu kuna michepuko ya barabara isiyo na alama yoyote. Nimeingia barabara moja nikaenda kama kilometa 3 nikakuta kizuizi. Ikabidi nirudi tena nilikotoka. Kilometa 3! Nikatafuta sehemu nyingine ya kuingilia na baada ya muda nikagundua nimepotea tena. Tupo wengi tunaopotea; kwani hakuna alama yoyote kuonyesha mwelekeo ni upi.

Nimechukua masaa mawili kufika maeneo ya Ubungo. Hapo nimekuta chaos! chaos! chaos! Haijulikani magari yanaelekea mwelekeo upi! Magari na malori yamekutana uso kwa uso kila mahali na kuzifunga barabara. Huwezi kuamini kuwa hii ni nchi ya kistaarabu hata kidogo. Hakuna mataa na hakuna askari wa kuyaongoza magari yanayopita ovyo na mwishowe kuyabana magari mengine. Sote tumesimama.

Najiuliza: hivi hawa wakubwa wana habari jinsi nchi inavyosulubiwa? Wana habari kuwa tumegeuzwa vichekesho? Je wana habari kuwa huko Ujerumani inakotoka kampuni haiwezekani kufanyika kitu kama hiki na wakapona? Wana habari kuwa viongozi wote waliohusika kuleta upuuzi huu wanaweza kufutwa kazi immediately? Na Uchina viongozi na watendaji waliofanya hii kandarasi ya kiwendawazimu wangenyongwa? Lakini kwetu ni business as usual. Kila kitu kiko sawa tu. Hakuna anayejali. Badala yake vinaonyeshwa vipindi vya tv kusifia huu upuuzi!

Na kinachoudhi zaidi ni kwamba huu mradi ni wa ulaji tu. Hakuna kitakachosaidia kupunguza foleni kwa kujenga barabara maalum ya mabasi yaendayo kasi. Wakubwa wetu hawajui kuwa wanaopanda magari yao binafsi hawatasubstitute magari yao kwa kupanda mabasi yanayonuka. No. Wataendelea kuendesha magari yao na foleni itaongezeka pia.

Wakati wenzetu wanajenga miundombinu ya karne ya 22 sisi tunajenga barabara maalumu ya mabasi! Mungu tusaidie! Kwani hawa wenzetu wakienda kutembea huko nje kila siku hawaoni kinachoendelea huko au alimradi wapate chao mfukoni kwa kuleta miradi aghali na ya kipuuzi isiyo na tija kwetu? Hata wao wanajua huu mradi ni danganya toto tu na ndio maana hata Prof. Tibaijuka alisema huu mradi hauwezi kuondoa foleni!

Sasa kama hata yeye anajua hivo huu mradi ni kwa faida ya nani? Kwa nini tutaabike hivi kwa mradi ambao we know for sure it is useless? Nawaonea huruma watu wangu!
 
Kwanza barabara ya morogoro road ni nyembamba sana, hata kuna muda ukiwa unataka kulipita gari kubwa mfano lorry, kama ukiwa ubavuni na mumefika kwenye corner inabidi mwenye gari dogo utulie maana ukiendelea unawezatolewa kwenye njia...

Pia barabara haina emergency exist mfano gari likikuharibikia mitaa ya rombo itabidi ulisukume mpaka ubungo ndio lihame njia.....

Alaf ujenzi ni wakusuasua sana, maana njia ambayo ipo busy dar nzima kama hiyo ilitakiwa ujenzi wake huwe waakili ya hali ya juu.....wafanye kazi usiku na mchana, sasa wenyewe usiku wanalala

Hapo ndio mtaelewa kwanini walifukuzwa kenya, hawa strabag wangebaki kenya zile flyover na thika road (highway) wangevisikia kwenye bomba
 
Ni muhimu sana kubadili mfumo wa kupata viongozi wa mikoa, wilaya n.k. Tuachane na mfumo wa kupeana uongozi mezani. wapigiwe kura na wananchi.

Chaos iliyopo Dar ni kwa sababu mkuu wa mkoa, mayor na wenziwe wamekuwa ni watu wa kufungulia milango wanasiasa.


Hivi kama mayor wa dar hajifunzi kutoka nchi nyingine? Jiji la biashara kama dar hata alama za barabarani zimewashinda?
 
Ni muhimu sana kubadili mfumo wa kupata viongozi wa mikoa, wilaya n.k. Tuachane na mfumo wa kupeana uongozi mezani. wapigiwe kura na wananchi.

Chaos iliyopo Dar ni kwa sababu mkuu wa mkoa, mayor na wenziwe wamekuwa ni watu wa kufungulia milango wanasiasa.


Hivi kama mayor wa dar hajifunzi kutoka nchi nyingine? Jiji la biashara kama dar hata alama za barabarani zimewashinda?

Vurugu ziliziopo Dar es Salaam ni kushindwa kwa mfumo wa uongozi,inabidi kutengeneza mfumo mpya! Dar imeelemewa na foleni za barabarani, uchafu,ujenzi holela,makelele yasiyo ratibiwa kutoka ktk nyumba za Ibada,Bar na Kumbi za Starehe,ujambazi,ukosefu wa maji safi na salama,miundombinu ya majitaka,nk! Lakini kuna watu wengi kuanzia RC,DCs,Wakuregenzi wa Manispaa,Mameya,nk ambao wanalipwa lakini hawana kazi ya maana wanafanya!
 
Nipo barabarani kutokea kimara kuelekea mjini. Njiani ni balaa tupu kwa sababu kuna michepuko ya barabara isiyo na alama yoyote. Nimeingia barabara moja nikaenda kama kilometa 3 nikakuta kizuizi. Ikabidi nirudi tena nilikotoka. Kilometa 3! Nikatafuta sehemu nyingine ya kuingilia na baada ya muda nikagundua nimepotea tena. Tupo wengi
tunaopotea; kwani hakuna alama yoyote kuonyesha mwelekeo ni upi.
Nimechukua masaa mawili kufika maeneo ya ubungo. Hapo nimekuta chaos! chaos! chaos! Haijulikani magari yanaelekea mwelekeo upi! Magari na malori yamekutana uso kwa uso kila mahali na kuzifunga barabara. Huwezi kuamini kuwa hii ni nchi ya kistaarabu hata kidogo. Hakuna mataa na hakuna askari wa kuyaongoza magari yanayopita ovyo na mwishowe kuyabana magari mengine. Sote tumesimama.
Najiuliza: hivi hawa wakubwa wana habari jinsi nchi inavyosulubiwa? Wana habari kuwa tumegeuzwa vichekesho? Je wana habari kuwa huko Ujerumani inakotoka kampuni haiwezekani kufanyika kitu kama hiki na wakapona? Wana habari kuwa viongozi wote waliohusika kuleta upuuzi huu wanaweza kufutwa kazi immediately? Na Uchina viongozi na watendaji waliofanya hii kandarasi ya kiwendawazimu wangenyongwa?
Lakini kwetu ni business as usual. Kila kitu kiko sawa tu. Hakuna anayejali. Badala yake vinaonyeshwa vipindi vya tv kusifia huu upuuzi!
Na kinachoudhi zaidi ni kwamba huu mradi ni wa ulaji tu. Hakuna kitakachosaidia kupunguza foleni kwa kujenga barabara maalum ya mabasi yaendayo kasi. Wakubwa wetu hawajui kuwa wanaopanda magari yao binafsi hawatasubstitute magari yao kwa kupanda mabasi yanayonuka. No. Wataendelea kuendesha magari yao na foleni itaongezeka pia. Wakati wenzetu wanajenga miundombinu ya karne ya 22 sisi tunajenga barabara maalumu ya mabasi! Mungu tusaidie! Kwani hawa wenzetu wakienda kutembea huko nje kila siku hawaoni kinachoendelea huko au alimradi wapate chao mfukoni kwa kuleta miradi aghali na ya kipuuzi isiyo na tija kwetu? Hata wao wanajua huu mradi ni danganya toto tu na ndio maana hata Prof. Tibaijuka alisema huu mradi hauwezi kuondoa foleni! Sasa kama hata yeye anajua hivo huu mradi ni kwa faida ya nani? Kwa nini tutaabike hivi kwa mradi ambao we know for sure it is useless? Nawaonea huruma watu wangu!

Mkuu pole sana. Samahani nataka kufahamu kwani malori nayo sio magari?

Umenikumbusha ubishi wa trekta ni gari au mashine?
 
Mwenye akili hasifii ujinga.kuna wehu wengne wanacfu sn kazi ya hyu babu hao completly ni wapanda daladal na ht ndoto za gari kw fikra zao potofu naona waendelee kulala huenda wakamalizia kuota.mkuu hamna cku nlokacrika km nilivyotoka cnza najua naingia mabibo sokoni one tme afu naendelea na mambo mengne nikajikuta turn yangu ni kituo kabla ya usalama imagne km c umaskin wa fikra ni nn vp km ingekuw ni mgonjwa anatok one way kuelekea pengne?ilichukua miezi na miezi kufungua hko kanjia still ni worse.
 
Pro-Chadema kupinga kila kitu Strabarg wanafanya kazi mazingira yanawasumbua.
 
STRABAG wanajua kutoa 10% ndo maana tumewapa tena barabara ya Segera mpaka Same kukarabati. Endeleeni kutoa povu tu. Jinga sana nyie mnataka tukale wapi? Lami lami kwenu kuna lami? Au ndo umeikuta Dar. Pombavu kabisa. Tusibirini 2025 ndo mupaange jinsi ya kujenga zenu.
 
Really? !!!
Makubwa

Naona wewe ni kama Thomaso, mpaka uone!!! Soma kwanza maelezo haya:

DART is an acronym for Dar Rapid Transit Agency.The Dar Rapid Transit (DART) Agency, came fully into force on 16th June 2008, established by GN.120 of 25th May, 2007, under the Executive Agencies Act, No.30 of 1997. It was established to achieve the following objectives:
Establish and operate Bus Rapid transit in Dar Es Salaam
Ensure smooth mobility on urban streets and roads, and
Ensure effective Management of DART Agency

Baada ya hapo, ebu tembelea hii website hii hapa


Background
 
Naona wewe ni kama Thomaso, mpaka uone!!! Soma kwanza maelezo haya:

DART is an acronym for Dar Rapid Transit Agency.The Dar Rapid Transit (DART) Agency, came fully into force on 16th June 2008, established by GN.120 of 25th May, 2007, under the Executive Agencies Act, No.30 of 1997. It was established to achieve the following objectives:
Establish and operate Bus Rapid transit in Dar Es Salaam
Ensure smooth mobility on urban streets and roads, and
Ensure effective Management of DART Agency

Baada ya hapo, ebu tembelea hii website hii hapa


Background

Nimeona mradi wa DART uko chini ya TAMISEMI. But nadhani kwa kuwa una programs nyingi (za ujenzi, uchukuzi nk), program ya ujenzi inasimamiwa na Magufuli, nadhani ndio maana siku ya uzinduzi (mwka juzi?) na mara kadhaa yeye ndyie ameonekana akifuatilia ujenzi.
 
Strabag ni janga

Fedha zinazojenga hiyo barabara zingetosha kujenga fly overs Ubungo, Magomeni, Mwenge, Moroko, Buguruni, na Tazara, na hiyo ingepunguza zaidi ya 50% ya adha ya msongamano Dar
 
Back
Top Bottom