Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Hivi fedha za kufadhili huu mradi wa barabara za mabasi yaendayo kasi (DART) zinatoka wapi?
 
Huu mradi hauko chini ya Wizara ya Ujenzi, mradi huu ni maalumu uko Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Je, ni another Richmond?

Jamani huu ndio ukweli, na msimamizi ni DART jamani mwacheni Magufuli wa watu!

Hivi waziri wa TAMISEMI nae yupo ktk ile list ya Nape na Kinana?
 
Nimeona mradi wa DART uko chini ya TAMISEMI. But nadhani kwa kuwa una programs nyingi (za ujenzi, uchukuzi nk), program ya ujenzi inasimamiwa na Magufuli, nadhani ndio maana siku ya uzinduzi (mwka juzi?) na mara kadhaa yeye ndyie ameonekana akifuatilia ujenzi.

You are right mkuu
 
Kwanza barabara ya morogoro road ni nyembamba sana, hata kuna muda ukiwa unataka kulipita gari kubwa mfano lorry, kama ukiwa ubavuni na mumefika kwenye corner inabidi mwenye gari dogo utulie maana ukiendelea unawezatolewa kwenye njia...

Pia barabara haina emergency exist mfano gari likikuharibikia mitaa ya rombo itabidi ulisukume mpaka ubungo ndio lihame njia.....

Alaf ujenzi ni wakusuasua sana, maana njia ambayo ipo busy dar nzima kama hiyo ilitakiwa ujenzi wake huwe waakili ya hali ya juu.....wafanye kazi usiku na mchana, sasa wenyewe usiku wanalala

Hapo ndio mtaelewa kwanini walifukuzwa kenya, hawa strabag wangebaki kenya zile flyover na thika road (highway) wangevisikia kwenye bomba

Kweli mkuu hawa jamaa usiku wanalala kazi wanaanza kufanya saa tatu asubuhu hadi saa kumi, nwisho wa mwaka walienda kutanua mbugani wiki 2 kazi ilisimama! Msimu wa mvua ndo huo ama kweli tanzania ni zaidi ya uijuavyo, tunaitaka tanganyika yetu
 
Mkuu mimi ni ccm damu ila ukweli ni lazima tukubali ,strabag hawafai hata kidogo

Vipofu kama kina Ritz ambao hawasikii wala hawaoni hawawezi kukuelewa. Nachukia sana jitu lisiloweza kuwa objective japo kwa siku moja. wanadhani wanaijenga CCM kumbe ni kinyume chake. wametusababisha wengine tuichukie CCM. Huwezi kuwa na akili timamu ukaunga mkono utendaji wa hawa punguani wanaoitwa Strabag. Ni Tanzania tu ndo unaweza kufanya haya wayafanyayo hapa ukaachwa. ONLY IN TANZANIA.
 
Last edited by a moderator:
sio strambag uongozi wa kikwete ni janga. Hakuna plan. kila cku kiongozi anaamua lake. No vision
 
Vipofu kama kina Ritz ambao hawasikii wala hawaoni hawawezi kukuelewa. Nachukia sana jitu lisiloweza kuwa objective japo kwa siku moja. wanadhani wanaijenga CCM kumbe ni kinyume chake. wametusababisha wengine tuichukie CCM. Huwezi kuwa na akili timamu ukaunga mkono utendaji wa hawa punguani wanaoitwa Strabag. Ni Tanzania tu ndo unaweza kufanya haya wayafanyayo hapa ukaachwa. ONLY IN TANZANIA.

Mbonyi monoama
 
Last edited by a moderator:
sio strambag uongozi wa kikwete ni janga. Hakuna plan. kila cku kiongozi anaamua lake. No vision

Tuambie wewe una vision gani zaidi ya kushinda humu jamvini na kwenye facebook?
 
Itachukua miaka kadhaa kuona impact ya hii project. Ni hadi hapo mtandao wake utakapogusa njia zote kuu za jiji kama Kilwa road, Nyerere road, New Bwagamoyo road, n.k. Lakini katika miaka 2 hadi 5 ijayo ni ngumu kuona foleni zikipungua mjini.

Lakini naamini itafika wakati juu ya barabara hizi tutafunga mataluma ya reli na ku-operate usafiri wa treni ndipo ukombozi utakapokuwa umekamilika
 
Barabara inayotoka akiba mpaka kimara nakuendelea kwenda bara

Hujamuelewa Nicas Mtei anachohoji, au kwa makusudi unakwepa. Kama ni barabara ya Morogoro, neno road linaongeza tija gani?...unapaswa kusema Morogoro Road au Barabara ya Morogoro na sio Barabara ya Morogoro Road!!!!
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lako mleta thread una stress nyingi kichwani mwako,nipe jiji duniani ambalo halina foleni,nipe jiji duniani ambalo miundombinu yake haipanuliwi,mradi wa mabasi yaendayo kasi,ni wa historia ya tangu rais wa kwanza,michoro yake na kila kitu vilikuwepo,serikali ya awamu ya nne imekuja katika utekelezaji tu wa kile ambacho awamu tatu hazikufanya,ni sawa na daraja la kigamboni,michoro yake ipo toka jk.nyerere akiwa rais,kikwete kaja kutekeleza,punguza stress,soma vitu uvijue,na sii thread za kuandika ukiwa kwenye foleni.
 
Back
Top Bottom