Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Katika Siasa Hakuna Rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu....Lolote Lawezekana..
 
kwa hili la mwapachu ni full aibu. ningelikuwa mimi ndo katibu mkuu wa ccm nisingeruhusu kupokea wachumia tumbo kama hawa kamwe.....
 
Zipo taarifa za chini kwa chini zinazodai kuwa Balozi Juma Mwapachu ana mpango wa kurejea CCM. Mpaka sasa bado haijafahamika ni sababu zipi hasa zilizompelekea kufikia uamuzi huo.

Itakumbukwa kwamba wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka jana, Balozi Mwapachu alirudisha kadi za TANU na CCM na kutangaza kumuunga mkono aliyekuwa mgombea Urais wa CHADEMA, Edward Lowassa.

=======

UPDATES:

Hatimaye imekuwa kweli. Balozi Mwapachu ametangaza rasmi kurejea CCM

Wa Kwanza huyo... hesabu inaendelea
 
Sitawashangaa kwa propaganda zenu hizi. kwani mlianza wakati wa kampeni kuwa LOWASA endapo akishindwa kupata uraisi atarudi CCM kwani kule CDM amefuata cheo na siyo uanachama wa CDM.

Mkapatwa na aibu kubwa sana baada ya kuona kuwa mh. Lowasa bado yupo ngangari ndani ya CDM pamoja na UKAWA bado inadunda tu.

Mlipatwa na AIBU KUBWA SANA majuzi mlipomuona Mh. Lowasa akiwa katika mkutano mkuu wa CHADEMA pale jijini MWANZA.

Mlipata aibu kubwa majuzi mliposhuhudia mama Regina Lowasa akiwa na BAWACHA pale hospitali ya Morogoro wakifanya usafi pamoja na kutoa misaada katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani.

NI AIBU YENU MILELE.

BADO MTASEMA MENGI. View attachment 330172
MBONA HAVAI YALE MAVAZI YETU??


Sitawashangaa kwa propaganda zenu hizi. kwani mlianza wakati wa kampeni kuwa LOWASA endapo akishindwa kupata uraisi atarudi CCM kwani kule CDM amefuata cheo na siyo uanachama wa CDM.

Mkapatwa na aibu kubwa sana baada ya kuona kuwa mh. Lowasa bado yupo ngangari ndani ya CDM pamoja na UKAWA bado inadunda tu.

Mlipatwa na AIBU KUBWA SANA majuzi mlipomuona Mh. Lowasa akiwa katika mkutano mkuu wa CHADEMA pale jijini MWANZA.

Mlipata aibu kubwa majuzi mliposhuhudia mama Regina Lowasa akiwa na BAWACHA pale hospitali ya Morogoro wakifanya usafi pamoja na kutoa misaada katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani.

NI AIBU YENU MILELE.

BADO MTASEMA MENGI. View attachment 330172
 
Lowassa alikwishapanga baraza la mawaziri, wakuu wa mikoa, wilaya na mabalozi. Poleni sana kwa wote mlionunuliwa kwa madaraka. Lowassa alitoa rushwa kwa baathi ya watu kwa kuwahaidi madaraka na tenda akiwa rais. Lowassa alikwisha uza nchi ya tanzania kabla ajachaguliwa kuwa rais.
 
SI WAKAE PEMBENI TU KAMA SISI KWANI LAZIMA UCHUKUE KADI
 
Kwahiyo Magufuli anashughulika na wapinzani wa CCM tu? Ndio maana majipu mengine yaliyomfikisha hapo hayagusi?

Kweli mabadiliko si lelemama!!!
 
Tuseme hii habari ni ya kweli....

Kwani hawezi kuishi bila ya kuwa CCM?

Yaani baada ya kuondoka kwa drama vile sasa anaamua kurudi tena?
Itakua aliomba mwenyewe kurudi CCM,lakini wale vijana pale Lumumba wakampa masharti magumu,mojawapo ni hili la kumchafulia jina kwa kumwandikia risala kama hii aisome au aitume mbele ya media.
 
Hana madhara huyo kwani hakuwa mwanachama wa chama chochote cha Ukawa..
 
Hii misumari ya Magufuri ni kiboko,watu wanarudi wenyewe. Kweli ngosha kaamua. Huko chama cha kuzungusha mikono hakukaliki kabisa.Jamaa kila akiamka ni nyundo tu.
 
Itakuwa inawaonea sana kama CCM itaanza kuwaona wale walioikimbia huko nyuma na sasa wameamua kujirudisha wenyewe kama ni maadui ama wabaya wao.

Bila kudanganyana, ilikokuwa inatupeleka serikali ya Kikwete ilifikia mahali kwa kiongozi mwadilifu kabisa, kuendelea kuwa mwanaCCM au kuwa ndani ya serikali ilikuwa sawa na kujitia najisi, hapakufaa kukaa mtu msafi.

Binafsi naona baadhi ya wana CCM waliochepuka ni wazuri kuliko baadhi ya wale waliong'ang'ania kubaki lakini wakiifilisi nchi, waliobaki kutokana na manufaa na maslahi binafsi waliyokuwa wakiyapata kwa kuwa kwao serikalini.

Mleta mada nadhani unakosea sana kudhani kwamba hao wanaorudi CCM wanakosea, hapana, kurudi kwao ni ishara nzuri kwamba mhe Magufuli ameziridhisha hata nyoyo za waliokuwa wamekatishwa tamaa.

Ya Mungu mengi, huwezi kujua hata Magufuli mwenyewe kwa misimamo aliyonayo na jinsi CCM ilivyokuwa imeoza anaweza kushindwa kuinyoosha na akaamua kuachana nayo akiwa bado Rais.

Tusione Kikwete naye akijibaragua kujidai anakikarabati chama hicho eti naye anaanza kuwafukuza wenzie, nakuhakikishia kwa dhati ya moyo wangu kwamba Kikwete asingekuwa na ubavu wa kufanya hayo ila ni kwa kujivunia nguvu na kujiamini anakoonyesha Magufuli katika uongozi wake.
 
Keshapoteza hata ile heshima kidogo aliyokuwa nayo. Hata huko ugambani hawatamwamini tena.
 
Pamoja na kurudi kwao hizo wanazoziita biashara za jamaa zao ziendelee kubanwa tena kisawa sawa maanake kwa sasa hawaaminiki popote na wala hawana ubavu wakurudi walikotoka.

Yaani miezi tu nje ya system tayari njaa imekolea mpaka mahaba waliyolewa yameyeyuka!!!

Kama utu uzima kweli ni dawa basi,wengine ni dawa ya bawasili.
 
Wakati umefika chama kuwa na msimamo wa kusimamia sheria na taratibu na miiko ya chama kuheshimiwa,kwan si busara kwa mtu kuhama chama na kumpokea bila kutafakari hii inafanya siasa zetu kutokuwa na nguvu na mvuto ktk ulimwengu,na kufanya kuyumba kwa chama kutokana na maslai yao binafsi.je alikotoka wanamtafakari vp? Tubadilike tusimamie misimamo yetu ktk siasa.
 
Mtu mzima, tena msomi na mwandishi wa kitabu cha Uongozi/Utawala, na zaidi ya yote mwanadiplomasia, anapokosa kuwa na msimamo tunamwiitaje!? Tukisema ni kibaraka waungwana watamshangaa, na ukimwiita mnafiki marafiki zake watamwogopa kama ukoma. Sasa tumwiiteje. Nadhani inatosha kusema ni mmoja wenye akili finyu zisizoweza kufanya uchambuzi wa mambo, ambaye kama mkristo, Yesu angemwambia hajui atendalo. Hata hivyo, mimi simshangai maana hata wakati wa siasa ya Ujamaa alikuwa critic wa mfumo ule; lakini leo anamfananisha Rais JP Magufuli na Nyerere, mw,asisi na mtetezi wa mfumo huo wa Ujamaa. Linalonisikitisha ni kwamba Taifa lilipoteza raslimali zake kumsomesha mtu ambaye hakuweza kuelimika japo alipitia elimu ya juu! Chama kiwe na tahadhari naye.serikali"Aibu iliyoje!! Bado najiuliza hivi kabla ya kutoa tamko hili alipata wasaa wa kushauriana japo na familia yake? Ni fedheha kubwa Mzee kama huyu kujidhalilisha kiasi hiki"eti shughuli zake na washirika wake zisikwamishwe na serikali"
 
Kwa hiyo ule waraka wa mwanzo ulikuwa uzushi sio?
 
Keshapoteza hata ile heshima kidogo aliyokuwa nayo. Hata huko ugambani hawatamwamini tena.


Sasa kubwa kuliko linakuja nalo ni la fisadi Lowasa, subiri uone sasa hivi ranchi yetu Handeni iliyoporwa na fisadi Lowasa inarudishwa mikononi mwa Wananchi na hapo ndiyo mtajua kwamba Wanasiasa wa kibongo wote wezi tu!
 
maCCM ni vigeugeu wa kutupwa. hili jitu la kimagamba ni linafiki kuliko maelezo.
 
Back
Top Bottom