Bwana huyu alinunuliwa na ahadi ya kupewa Uwaziri. Leo anarudi CCM kwa sababu (anasema mwenyewe): "sitaki shughuli zangu na za washirika wangu zikwamishwe na Serikali... ". Kwa lugha nyepesi anataka kuinunua Serikali kwa kadi ya CCM. Nimuulize Mheshimiwa Col Kinana, tukitumia lugha ya kijeshi tukasema mtu huyu ni mamluki tutakosea? Na kama hivyo ndivyo ilivyo, kuna haja yoyote kumpokea katika Chama. Hamwoni huyu mtu ndiyo kundi la mchwa uliyokuwa unakipekecha Chama ndani kwa ndani kisha wakakaa pembeni na kutuambia Chama kimeoza? Haya, mwenye macho na masikio aone na kusikia.