Umeulizwa nani ali-engineer mauaji ya Rwanda? jibu swali wacha porojo.
Off topic, tunaongelea mauaji ya Arusha sio ya Rwanda.
Umeulizwa nani ali-engineer mauaji ya Rwanda? jibu swali wacha porojo.
Asante Kikwete kwa Huduma nzuri za afya kila sehemu ya nchi hii.
Fundi mchundo
Kwakweli unayoyasema mengine yana ukweli kwamba lugha kali za kidini zinaweza kupelekea migogoro ndani ya nchi yetu. Ila the Padre Lwambano alivyoitoa hiyo kauli ilikuwa kama anatoa maagizo kwa serikali iwashughulikie waislamu. Na kumbuka Lwambano alitoa hilo tamko tarehe 8 February, 1998 , mapambano yakatokea few days later tarehe 13th February 1998. Rais awamu ile ambaye Mkapa bila kushauriwa vizuri akatoa amri ishughulikiwe hiyo hali. Haya sio maneno yangu ni huyu Aziz kama anavyosema hapa:-
Few people can doubt that Lwambano appears to have been encouraged by the public and official
endorsement the Catholic clergy had received with regard to their grievances against Muslim preaching.
That endorsement had come from a fellow Catholic in the person of the President of Tanzania. On 4
January 1998 at Tabora during celebrations of the Western Diocese of the Moravian Church, President
Mkapa declared war on people who go about distributing cassettes, booklets and convening meetings
where they insulted and ridiculed other religions (Daily News, 5 January 1998). It is relevant that Muslim
preachers are the only people using cassettes and booklets, in addition to public debates, in the propagation
of religion
Na maaskofu wameendelea na tabia yao hii ya kujiona wao ndio wasemaje wa wananchi na wako juu kuliko viongozi wengine wa kiroho. Na hili ndio linalowafanya wajisahau mpaka waingie sasa katika siasa jambo ambalo litawatokea puani. Na jamaa amelitahadharisha kama anavyosema tena hapa:-
It is my considered opinion that the response by the CCM government is religiously biased and prejudiced. Given the fact that the Catholic clergy had failed to prove their charges of blasphemy in a mediation meeting of Bishops and Sheikhs convened by former President Mwinyi in1993, President Mkapas move of unilaterally embarking on using state power to remedy a grievance of his Church leaders without giving Muslims the right of reply suggests nothing but religious bias. Catholics are after all expected to follow whatever the hierarchical church says!
Sasa Pengo should have apologies to muslim for the comments of his fellow member au kama hilo ameshindwa basi kwa kushindwa kukemea matumizi ya nguvu zisizo na msingi kwa raia waliokuwapo pale mwembechai ambao wengi wao hawakuwa katika sehemu ya ule uharamia wa kutaka kuchukua ule msikiti wa mwembechai. But kwakuwa serikali ilikusudia kutoa message kwa waislamu wakaamua kufanya wapendavyo ili kutoa message kwa waislamu wote kuwa hili jambo halikubaliki na maaskofu wakaa kimya kama vile hawaoni na hapa siko pamoja nao kwa hili.
Hili ndio tamko la viongozi wa kiroho kuwa tunalaani mauaji ya raia wasio na hatia na sio kujiingiza katika siasa kusema humtambui meya it does not making any sense.
Bigirta kwanza tuambie hapa ni wapi? Tanzania kweli? Pili sikatai umaskini umezidi Tanzania lakini ndio maana kuna watu wanaitwa wanasiasa na sio viongozi wa kiroho. Wakitaka wavue majoho yao waingie ulingoni venginevyo sikubaliani nao.
Kwa wakristo kutomtka Kikwete, nadhani lina ukweli ndani yake. Tazama hata humu JF, ni wakristo wangapi wanomponda Kikwete ingawa ni wazi kabisa kuwa Kikiwete ni kiongozi mzuri, mchapa kazi na ameifikisha mbali Tanzania katika miaka hii mitano.
MASKOFU NA MASHEHE, KABLA YA WADHIFA WAO KWANZA NI WATANZANIA HIVYO KUKEMEA MAOVU HAKI YAO
Nashangaa sana haufu za udini anazoweza mtu kulazimisha hapa kwa MAASKOFU MJINI ARUSHA nchini ni upi huo hasa? Maana mpaka dakika hii MAASKOFU hawamtambui MEYA WA CCM JIJINI ARUSHA, ambaye naye ni MKRISTO SAWASAWA na hao maaskofu.
Kimsingi MAASKOFU walisema wazi kwamba wanachokipinga kwa meya huyu wa CCM wala si maovu ya kuwa mwana-CCM, si maovu ya UKRISTO wake isipokua MAOVU WANAYOYAKEMEA ni sheria na taratibu za uchaguzi zilivyopindishwa kumuingiza madarakani kupitia mlango wa nyuma.
Sasa viongozi wetu wa kiroho wasipokemea maovu kama haya, ukimya wao juu ya jambo hatari kama hili tafsiri yake ni kwamba wameunga mkono huo uchafu na ubakaji wa DEMOKRASIA, ndivyo watu mnavyotaka????????????????
Kama shida ni kuhusu vifo vya raia wa Tanzania na hata yule wa nchi rafiki na jirani Kenya, nadhani mtu asijaribu kuziba wengine midomo. Mauaji ya pemba 2001 vingozi wa dini walipiga kelele sana na kuikemea serikali ya Mhe Mkapa wakisema nguvu nyingi kupita kiasi imetumika dhidi ya wananchi. Katika kundi hilo kulikwepo Mashehe, Maaskofu, Mapadri na Wachungaji kwa mchanganyiko wake.
Hivyo kutokana na ukweli huu ambao iko mikononi mwao waandishi wa habari mpaka leo hii, ni matumaini yangu kwamba hauna maana yoyote kutaka kutuambia ya kwamba kama kilio cha Watanzania hakikusikilizwa tulipoipigia kelele mauaji ya Pemba basi leo hii raia tunapouaua tusiseme kwa sababu kule hatukusilizwa vile vile.
Pia, sitaki niaminishwe ya kwamba mweka hoja hii anajaribu kutuambia kwamba MAUAJI YA KINYAMA ARUSHA kwa vyovyote vile yalitekelezwa na MTU AU WATU anaowajua yeye ILI KUSAIDIA KUMLIPIA KISASI CHA MAUAJI YA PEMBA leo hii hivyo anaona hadi sasa ngoma ni droo na wala kusilalamike mtu?
Mwisho, imekuaje mtoa mada umekwepa kujiuliza maswali yote ya msingi hapa; Je, MASHEHE NA MAIMAMU kukaa kimya bila kukemea mauaji ya kinyama Arusha hadi kujitokeza tu kutetea Mhe kwa sura nyingine ya ajabu ajabu tu inamaana wanayo agenda gani?????????