KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,139
[h=3]Mobhare Matinyi: " Huenda Babu Wa Loliondo Alikuwa Mgonjwa Wa Akili"[/h]Submitted by Mjengwa on 1.1.12
Maggid,
Uko sahihi kabisa.
Huyu Babu alikuwa janga kwa taifa letu na anapaswa kulaaniwa vikali na watu wote wenye akili timamu. Uwezekano mkubwa ni kwa Babu wa Loliondo kuwa na tatizo la akili ambalo halikujitokeza kwa namna tuliyozoea - ile kupiga kelele na kuvua nguo. Huyu babu labda ni mgonjwa akili aliyejikita katika imani za kimiungu.
Watanzania, kutokana na ujinga wetu, umaskini wetu, na maradhi yetu, tulimpa fursa ambayo hakustahili. Taifa lenye watu zaidi ya 60% wanaoamini ushirikina, asilimia 40% wasiojua kusoma na kuandika, 35% wanaoishi katika umaskini uliokithiri, na viongozi wengi wanaoshinda kwa waganga, watu wanaofikiri kuwa unene tipwatipwa na ulevi ni afya, ni lazima mtu kama Babu angeonekana shujaa kwetu.
Dawa za Babu zilielezwa na wazee wa Kisonjo kwamba ni za kawaida, na zinatibu magonjwa kadhaa likiwemo kisukari, lakini kwa ujinga wetu watu wakawa wanakunywa kikombe kimoja kwa kudhani imani za kimiujiza zitawasaidia. Wale mababu hawakunywa vikombe vya Babu na bado wanaendelea kuzitumia bila shida kila wakiumwa. Mababu wasiojua kusoma na kuandika wanatushinda akili watu tuliokwenda shule. Dawa zile zimefanyiwa utafiti duniani na zikaonekana kuwa na uwezo wa kufanya kazi fulani, hivyo, ukinywa kikombe kimoja unaweza kupata nafuu lakini hutapona kwa sababu hukunywa kitaalam. Unafuu huu ndio uliowapa wajinga imani kwa Babu anaponya.
Babu hakuwa na utumishi wa uungu wowote wala utabibu wowote. Huenda ni mgonjwa wa akili na ni kweli amekuwa janga la kitaifa. Aibu na fedheha kwa taifa letu.
Mobhare Matinyi.
Maggid,
Uko sahihi kabisa.
Huyu Babu alikuwa janga kwa taifa letu na anapaswa kulaaniwa vikali na watu wote wenye akili timamu. Uwezekano mkubwa ni kwa Babu wa Loliondo kuwa na tatizo la akili ambalo halikujitokeza kwa namna tuliyozoea - ile kupiga kelele na kuvua nguo. Huyu babu labda ni mgonjwa akili aliyejikita katika imani za kimiungu.
Watanzania, kutokana na ujinga wetu, umaskini wetu, na maradhi yetu, tulimpa fursa ambayo hakustahili. Taifa lenye watu zaidi ya 60% wanaoamini ushirikina, asilimia 40% wasiojua kusoma na kuandika, 35% wanaoishi katika umaskini uliokithiri, na viongozi wengi wanaoshinda kwa waganga, watu wanaofikiri kuwa unene tipwatipwa na ulevi ni afya, ni lazima mtu kama Babu angeonekana shujaa kwetu.
Dawa za Babu zilielezwa na wazee wa Kisonjo kwamba ni za kawaida, na zinatibu magonjwa kadhaa likiwemo kisukari, lakini kwa ujinga wetu watu wakawa wanakunywa kikombe kimoja kwa kudhani imani za kimiujiza zitawasaidia. Wale mababu hawakunywa vikombe vya Babu na bado wanaendelea kuzitumia bila shida kila wakiumwa. Mababu wasiojua kusoma na kuandika wanatushinda akili watu tuliokwenda shule. Dawa zile zimefanyiwa utafiti duniani na zikaonekana kuwa na uwezo wa kufanya kazi fulani, hivyo, ukinywa kikombe kimoja unaweza kupata nafuu lakini hutapona kwa sababu hukunywa kitaalam. Unafuu huu ndio uliowapa wajinga imani kwa Babu anaponya.
Babu hakuwa na utumishi wa uungu wowote wala utabibu wowote. Huenda ni mgonjwa wa akili na ni kweli amekuwa janga la kitaifa. Aibu na fedheha kwa taifa letu.
Mobhare Matinyi.