Baba mwenye nyumba hataki nifanye biashara ya pombe kali

SONDR

JF-Expert Member
Apr 18, 2019
271
643
Wanajamvi habari za muda huu, poleni na majukumu ya kutafuta ridhiki. Niende kwenye mada moja kwa moja.

Nimepangisha fremu kwenye NYUMBA moja mjini kwa lengo la kufungua biashara ya pombe Kali yaani liquor store.

Nikaingia mkataba na mwenye nyumba wa miezi kumi wakati huo yeye hajui nataka kufanya biashara gani. Nikanza maandalizi ya kufungua biashara yangu Jana nikaleta mzigo wa pombe Kali ambazo nimefungasha kutoka jijini Dar es salaam.

Baada ya kumaliza kushusha na kuingiza mzigo wangu kwenye fremu yangu nikaondoka nikarudi nyumbani kwangu nikisubiri mzigo mwengine ufike ili niaze kufanya biashara mnamo tarehe moja January 2024.

Cha kushangaza asubuhi ya leo Kama saa kumi na mbili na nusu napokea simu ya baba mwenye nyumba akisema amekaa na familiya na wamekubaliana hawaruhusu biashara ya pombe kwenye nyumba yao nilichoka na kukosa cha kumjibu.

Nikamhoji mbona hukuliweka Hilo kwenye mkataba na kwanini hukusema wakati na kodisha akasema Mimi sikumuambia nataka nifanye biashara gani. Nikamueleza wazo la biashara nilangu ww umekodisha fremu ili Mimi nifanye biashara halali ambayo haivunji Sheria za nchi.

Kama unaitikadi zako kuhusu biashara flani ilikupasa uweke kwenye mkataba ili mimi nikisoma naelewa kwakua siwezi kujua itikadi yako Kama hujasema au kuweka wazi.

Wakuu nachanganyikiwa sielewi nimeshatumia pesa ya kutosha alafu mwenye nyumba anakuja na hoja Kama hii naombeni ushauri wenu wakuu.
 
Cha kwanza ulifanya makosa kutokumuweka wazi juu ya biashara unayo taka kuifanya.
Kama anakubali kukurudishia hela yako ya pango basi ondoka hapo utafute sehemu nyingine, maana kila mtu ana uhuru wa kupanga namna ya kuendesha mali yake , nyuma ameijenga kwa nguvu zake na sio kwa msaada wa sheria za nchi.
 
Wanajamvi habari za muda huu, poleni na majukumu ya kutafuta ridhiki.
Niende kwenye mada moja kwa moja
Nimepangisha fremu kwenye NYUMBA moja mjini kwa lengo la kufungua biashara ya pombe Kali yaani liquor store.

Nikaingia mkataba na mwenye nyumba wa miezi kumi wakati huo yeye hajui nataka kufanya biashara gani.
Nikanza maandalizi ya kufungua biashara yangu Jana nikaleta mzigo wa pombe Kali ambazo nimefungasha kutoka jijini Dar es salaam.

Baada ya kumaliza kushusha na kuingiza mzigo wangu kwenye fremu yangu nikaondoka nikarudi nyumbani kwangu nikisubiri mzigo mwengine ufike ili niaze kufanya biashara mnamo tarehe moja January 2024.

Chakushangaza asubuhi ya leo Kama saa kumi na mbili na nusu napokea simu ya baba mwenye nyumba akisema amekaa na familiya na wamekubaliana hawaruhusu biashara ya pombe kwenye Nyumba yao nilichoka na kukosa Cha kumjibu.

Nikamhoji mbona hukuliweka Hilo kwenye mkataba na kwanini hukusema wakati na kodisha akasema Mimi sikumuambia nataka nifanye biashara gani
Nikamueleza wazo la biashara nilangu ww umekodisha fremu ili Mimi nifanye biashara halali ambayo haivunji Sheria za nchi.
Kama unaitikadi zako kuhusu biashara flani ilikupasa uweke kwenye mkataba ili mimi nikisoma naelewa kwakua siwezi kujua itikadi yako Kama hujasema au kuweka wazi.

Wakuu nachanganyikiwa sielewi nimeshatumia pesa ya kutosha alafu mwenye nyumba anakuja na hoja Kama hii naombeni ushauri wenu wakuu.
Mosi,
Pole sana mkuu. Gharama na muda uliotumia kutafuta mpaka kupata hiyo nafasi ya biashara hapo.

PIli, muulize mzee yeye anasemaje? Kama anataka kurudisha pesa ni sawa ila tu alipe na gharama zako zote za kuleta mzigo na usumbufu, na hilo likiwa gumu yeye kulitekeleza omba ushauri kwa wanasheria wakuandikie statment ya msimamo wake maana yeye kwenye mkataba hakusema biashara gani si ruksa kufanya hapo kwake.

Hii ishu nishawahi kutana nayo. Nilienda kwa mwanasheria yule bibi mwenye fremu kuona vile akaniambia mwanangu tuongee tuyamalize.

Asitake kusumbua watu, tena alipe gharama zote
 
Cha kwanza ulifanya makosa kutokumuweka wazi juu ya biashara unayo taka kuifanya.
Kosa ni la kwake yeye kwa kushindwa kuweka bayana kwenye mkataba.

Mzee anaendeshwa na hisia, kuliko akili.

Nimefika kwako nimesoma mkataba hakuna kipengele chochote kinachosema biashara fulani haitakiwi.

Huyo hana pakuchomoka arudishe pesa yote, fidia na gharama za mwanasheria.
 
Cha kwanza ulifanya makosa kutokumuweka wazi juu ya biashara unayo taka kuifanya.
Kama anakubali kukurudishia hela yako ya pango basi ondoka hapo utafute sehemu nyingine, maana kila mtu ana uhuru wa kupanga namna ya kuendesha mali yake , nyuma ameijenga kwa nguvu zake na sio kwa msaada wa sheria za nchi.
Uzi uishie hapa.
 
Cha kwanza ulifanya makosa kutokumuweka wazi juu ya biashara unayo taka kuifanya.
Kama anakubali kukurudishia hela yako ya pango basi ondoka hapo utafute sehemu nyingine, maana kila mtu ana uhuru wa kupanga namna ya kuendesha mali yake , nyuma ameijenga kwa nguvu zake na sio kwa msaada wa sheria za nchi.
Kama hiyo ni fremu kama anavyodai mpangaji, ina maana anaweza kufanya biashara yoyote halali. Hilo ni kosa la mwenye fremu, alitakiwa kabla hajampangisha mtu AMPE na masharti ya biashara Gani hataki zifanyike kwenye fremu yake. Kujaa kimya maana yake "fanya biashara yoyote halali ili mradi unilipe Kodi yangu" .

Sheria za nchi ndizo hizo hizo zilizompa uhalali wa Hilo eneo analoliita la kwake kujenga. Usisahau.
 
Kwaiyo Kaka niweke wazi business idea vp akigoma kunikodisha alafu akafungua yeye
Sasa mkuu hiyo nyumba si mali yake hivyo anaweza kufanya chochote anacho jisikia ili mradi havunji sheria za nchi.
Sema kakuumuza sana kwa kutokuwa wazi tangu mwanzo, mm ninacho kushauri ni akikubali kukurudishia hela yako ya pango hama tu utafute site nyingine usikuze mambo,hii bongo jinsi unavyo kuza mambo ndivyo watu wanazidi kukufanya furusa.
 
Cha kwanza ulifanya makosa kutokumuweka wazi juu ya biashara unayo taka kuifanya.
Kama anakubali kukurudishia hela yako ya pango basi ondoka hapo utafute sehemu nyingine, maana kila mtu ana uhuru wa kupanga namna ya kuendesha mali yake , nyuma ameijenga kwa nguvu zake na sio kwa msaada wa sheria za nchi.
Hakuna kosa alilifanya kama biashara ni halali ya nchi. Hizo imani zake alipaswa yeye mwenye nyumba ndio afanye declaration kwamba mimi hapa biashara flani na flani siruhusu hata ni halali kisheria.
 
Wakuu naombeni ushauri wenu kijana mwenzenu nimechoka nawaza nn chakufanya sielewi
Piga hesabu ya faida ambayo ungetarajia kuipata kwa MIEZI uliyolipia mwambie yy na familia yake wakulipe usepe.otherwise wakuache ama watafute means nyingna na si ishu ya pombe.ishu ya pombe wawaachie watoa leseni na ww
 
Back
Top Bottom