Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 255
GEITA: Mtoto Dickson Elias (5) mkazi wa Chikobe, Kata ya Butundwe, Wilaya ya Geita mwenye ulemavu wa viungo, ameuawa na baba yake mzazi kisha kuzikwa porini kwa madai ya kushindwa kuendelea kumlea baada ya mama mzazi wa mtoto huyo kurudi kwao.
Kufuatia mauaji hayo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, linamshikilia Elias Bukumie (32) ambaye ni baba mzazi wa mtoto huyo kwa tuhuma za mauaji.
Akielezea tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Safia Jongo, amesema mwili wa mtoto huyo ulionekana porini na wasamaria wema.
“Wasamaria wema wakiwa porini, waliona mwili wa mtoto wa miaka mitano. Taarifa za awali zilisema amechunwa ngozi na kukatwa ulimi. Timu yetu ya upelelezi ilikwenda hadi Kijiji cha Chikobe na kuukuta mwili wa mtoto ambaye inaonekana alikuwa mlemavu wa viungo,” amesema Kamanda Jongo.
CHANZO: Mwananchi
Kufuatia mauaji hayo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, linamshikilia Elias Bukumie (32) ambaye ni baba mzazi wa mtoto huyo kwa tuhuma za mauaji.
Akielezea tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Geita, Safia Jongo, amesema mwili wa mtoto huyo ulionekana porini na wasamaria wema.
“Wasamaria wema wakiwa porini, waliona mwili wa mtoto wa miaka mitano. Taarifa za awali zilisema amechunwa ngozi na kukatwa ulimi. Timu yetu ya upelelezi ilikwenda hadi Kijiji cha Chikobe na kuukuta mwili wa mtoto ambaye inaonekana alikuwa mlemavu wa viungo,” amesema Kamanda Jongo.
CHANZO: Mwananchi