Baada ya TPA kutangaza tenda kuhusu uwekezaji Terminal 2, Bado mnaamini Bandari zote zimeuzwa?

Swali Rahisi kwako:
Kama umeusoma waraka huo Kuna provision yoyote ambayo imeandikwa Kwa muktadha wa kidini au ukiitaka serikali izingatie matakwa ya kidini au kanisa Katoliki?

Kama hujausoma usicoment utadhihirisha ujinga wako.

Baraza la Maaskofu linaundwa nà Maaskofu ambao ni Watanzania, wanaaongoza waumini wa kanisa Katoliki Tanzania. Hivyo logically Maaskofu wanaongoza sehemu ya watanzania, na sio watanzania wote!
Watanzania ni wananchi wa Tanzania wanaostahili haki za kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Maaskofu wametoa waraka kama viongozi wa kanisa Katoliki Tanzania ambapo Kuna watanzania wanaostahili haki za kiuchumi, na katika mkataba wa Bandari Kuna athari za kiuchumi Kwa watanzania bila kujali dini zao au kama hawana dini kabisa!

Kimsingi kisu kimegota mfupani
Kisu gani? Kimegongaje?
 
1. Tanzania shall inform Dubai of any other opportunities relating to ports

2. Tanzania will inform Dubai of any other opportunities relating to ports

3. Tanzania may inform Dubai of any other opportunities relating to ports

Tutafsilie wanazengo tuelewe utofauti wa verb (Shall, Will na May)
Sasa hayo maelezo mbona yako wazi na yanaeleweka, yaani kutangaza vivutio Kwa mwekezaji imekuwa dhambi?
 
Kama mwananchi niliyekuwa nikifuatilia hoja kwenye mitandao ninauliza;
Wanaosemekana kupata pesa toka kwa mwarabu wameshawarudishia pesa yao?.
Mkataba wa IGA umefutwa?(Ili baada ya kushinda zabuni uandikwe wenye maslahi kwa pande zote)
Sijui Tamko la TEC lilieleweka au hoja zimepuuzwa na kutafutiwa mbadala huu?.
Si tulishaambiwa " Hivi mnadhani Watanzania ni wajinga?"


Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Fedheha ni kwamba makanisani waraka ulishapelekwa na hivi sasa tunaishi na gharama za kuitengeneza hiyo chuki kati ya serikali na ukatoliki.

Tulilishwa matango pori kwamba mwarabu anataka kuinunua nchi hivyo ule waraka ulikuwa na ujumbe wa siri wa kukataa kuiuza Tanzania kwa mwarabu haswa muislam.

Leo hii tangazo la TPA linamtaka mwekezaji mwenye uwezo ajitokeze na vigezo vyake vitazamwe kama vinakidhi mahitaji ya uendeshaji wa bandari kisasa, tangazo linasema hata wale wazalendo wenye uwezo wa kuendesha bandari kisasa na wao wanaalikwa pia.

Maana yake ni kwamba hata sisi walei wa kawaida tunaosali makanisani tunaalikwa kufanya biashara na serikali yetu kama vigezo vyetu vinatimia!, hii ni aibu kubwa sana ambayo maaskofu pengine kwa kutokujua walichokifanya waliamua kuitafuta wao wenyewe!.
Hebu walete kwanza hiyo tenda iliyowapa DP world ushindi na toune walishindanishwa na nani.
Kama haupo basi ni dhahiri kuwa hiki wanachofanya ni danganya toto kuzuga baada ya mwizi kufumaniwa.
Tunashindwa kesi kwenye mahakama za usuluhishi kila uchwao na serikali kulipa fidia pesa nyingi za walipa kodi na hili wanalofanya ni kwa gharama yetu wenyewe kulipa fidia huko mbeleni kama ule mkataba walioupitisha bungeni hautaondoshwa.
Mkaidi hafaidi hata siku ya Idd. Ukaidi uliosumumwa na rushwa kwenye uwekezaji ndio unaotugharimu kulipa matrilioni ya shilingi kwa kila kesi inayofunguliwa. Na hakuna mpumbavu yeyote aliyewajibika kwa hizi kesi zote ikimaanisha kuwa kuna ushirika wa genge la watawala kula njama za hizi hujuma.
Kama sii njama kuhusisha ofisi kuu ya nchi inayowajibika kuwawajibisha wahujumu ni nani aliyewajibishwa?
Mikataba iliingiwa na maamuma? Watu wasio onekana?
 
Kwa wachache tuliobarikiwa kuielewa vizuri nchi hii na jamii yake pamoja na siasa zake tunaposimamia jambo kwa maslahi ya taifa naomba tuheshimiwe na tueleweke vizuri.

Kwa miezi 2 sasa kuna kikundi cha wanasiasa na viongozi wa dini, kwa maslahi binafsi na kutumiwa na watu ambao kila siku wamekuwa wakineemeka kwa michezo yao michafu wanayoifanya kwenye njia zetu kuu za uchumi walianzisha maneno kuwa Bandari zote za Maziwa na Bahari ikiwemo Bandari ya Dar es Salaam zimeuzwa kwa waarabu.

Kikundi hichi cha watu kilisambaza maneno haya nchi nzima huku kikisema kuwa Bunge letu limeshurutishwa na Rais Samia kuuza Bandari zetu na hivyo linauza nchi.

Kwa wachache tunaowajua vizuri tulisema kuwa haya maneno ya hawa watu hayana ukweli wowote ule ila ni hila za watu ambao wamekuwa wakineemeka kwa kuifisadi nchi yetu kupitia Bandari ambao wanatunga maneno ili ku sabotage nia nzuri ya Rais katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi kupitia njia zetu kuu za kiuchumi ikiwemo Bandari.

Tuliosimamia ukweli huu na kukataa upotoshaji wa kundi hili la wanasiasa na viongozi wachache wa kidini tuliitwa majina yote eti tumehongwa, mara sisi ni chawa wa Rais Samia.

Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kuwa, ukweli una tabia moja, unatembea taratibu sana ila uzuri wake ni lazima tu ufike mahali pake.

Baada ya Mamlaka ya Bandari kutoa tangazo la kukaribisha maombi ya uwekezaji katika Terminal 2 ya Bandari yetu ya Dar es Salaam sasa nimeamini rasmi maneno ya yule mzee.

Kilichonifurahisha ni kwamba, baada ya tangazo hili la Bandari, Sijasikia maneno yale ya wale wanasiasa pamoja na wale viongozi wa dini hasa TEC kuwa Rais kauza Bandari ya Dar es Salaam au Bandari zote kwa waarabu!


Wale watu waliokuwa wanasema kuwa Bandari zetu zimeuzwa wameufyata kimyaaaaaa na siwasikii wakisema neno lolote lile zaidi ya kuhamisha magoli saivi wameanza kuzungumzia kampuni ya Adani.

Wale waliokuwa wanasema tumeondoa our National Sovereignty kwa kuwapa Bandari yetu Dubai ndo siwasikii kabisa sasa sijui wamelala usingizi wa pono hawajaona hili tangazo la TPA?

Napenda kumaliza kwa kusema
Tanzania kuna kundi maslahi ambalo limekuwa likinufaika kwa ujinga wa Watanzania. Kundi hili ni zito na lina wanasiasa na watu wa dini pia.

Endapo msiposimama na Serikali kuiunga mkono katika kuleta mapinduzi ya kweli ya kiuchumi, nchi yetu itakuwa maskini hadi ukamilifu wa dahali.

Tumsifu Yesu Kristo!

Nakala kwa
The Boss FaizaFoxy GUSSIE
IGA KATI YA DUBAI NA TANZANIA NASEMAJE KUHUSU BANDARI ZETU??

LABDA HIYO TENDA INATANGAZWA KWA NIABA YA DUBAI SISI TUTAJUAJE? SISI TUNAANGALIA IGA INAVYOSEMA, STORI NYINGINE YOYOTE NI NGONJERA
 
Sasa hayo maelezo mbona yako wazi na yanaeleweka, yaani kutangaza vivutio Kwa mwekezaji imekuwa dhambi?
Unajua maana ya neno shall, will na may katika muktadha wa sheria? Kama hujui mtafute mwanasheria akuelimishe. Huu sio mkataba wa kitchen part na Dj . Ni legal agreement!
 
Tundu lissu mkatolic, nauliza hivi chadema walivyompiga risasi lissu Tec walimsaidia nini mkatolic mwenzao?
Two wrongs can never make it right, darkness can never drive away darkness, only light can do!

Attempting murder is not the same as entering stupid contract or agreement! Shule ulienda kufanya nini?

Kwamba kama hukufanya vizuri Jana Leo Usifanye vizuri au kujaribu kufanya vizuri?

Na unaposema chadema walimpiga risasi Tundu lissu Ina maana una uhakika na taarifa zako, Kwa maana tunaamini zimetokana na vyombo vya kidola vya uchunguzi, swali
1. Kwanini mpaka leo chadema hawajakamatwa na Jeshi la polisi

2. Kwanini mpaka leo hawajashtakiwa Kwa kujaribu Kuua na kuharibu Mali?

2. Kwanini mpaka leo hawajashtakiwa Kwa kuondoa ulinzi eneo la makazi ya viongozi hasa speaker ili kutekeleza azma yao ya kumuua Tundu Lisu?

3. Kwanini wasilaumiwe Kwa kumpora ubunge na kuukataa kumpa au kumhudumia matibabu?

Kama huna majibu ya maswali haya wewe ni mbea na ni aibu Kwa familia yako na ukoo wako hasa watoto wako
 
Hapakuwa na sababu ya kumshindanisha na mtu yoyote. Anamiliki meli 400 zinazozunguka dunia nzima, nitajie mshindani wake mwenye wingi wa meli zenye kufikia angalau nusu tu ya hizo 400.

Anaendesha bandari za Uingereza, China na Ulaya nzima, ni mzoefu sana wa end to end logistic chain ambayo kisasa ndio maana mpya ya neno PORT.

Kwa suala la vigezo kawazidi wengi sana. Kanisa limechemka vibaya kuja na waraka wakati walikuwa hawajui kwa kina malengo ya serikali ni yapi.
Uingereza walimpa bandari zao zote?

Mkataba waliosaini uingereza ni sawa na huu tuliosaini sisi wa vipengele vy kipumbavu?

Kuwa na umiliki wa meli nyingi duniani ndio uwe mlango wa kusaini mikaytaba ya kisenge??
 
Fedheha ni kwamba makanisani waraka ulishapelekwa na hivi sasa tunaishi na gharama za kuitengeneza hiyo chuki kati ya serikali na ukatoliki.

Tulilishwa matango pori kwamba mwarabu anataka kuinunua nchi hivyo ule waraka ulikuwa na ujumbe wa siri wa kukataa kuiuza Tanzania kwa mwarabu haswa muislam.

Leo hii tangazo la TPA linamtaka mwekezaji mwenye uwezo ajitokeze na vigezo vyake vitazamwe kama vinakidhi mahitaji ya uendeshaji wa bandari kisasa, tangazo linasema hata wale wazalendo wenye uwezo wa kuendesha bandari kisasa na wao wanaalikwa pia.

Maana yake ni kwamba hata sisi walei wa kawaida tunaosali makanisani tunaalikwa kufanya biashara na serikali yetu kama vigezo vyetu vinatimia!, hii ni aibu kubwa sana ambayo maaskofu pengine kwa kutokujua walichokifanya waliamua kuitafuta wao wenyewe!.
Ninauhakika kabisa wew akili yako ni ndogo sana ukilinganisha na hao jamaa waliotoa huo walaka., pia nina uhakika hujuwi historia na siasa za Taifa hili kwa undani.
 
Ngoja kwanza tuweke akiba ya maneno, inawezekana TPA waliwainfom Dubai kuomba ruksa kwa hili Dubai waliwapa green light 🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom