Hichi ndio kinawakuta wastaafu wengi. Nguvu zimeisha, akili imechoka alafu uanze moja na biashara. Sector ambayo imejaa kila aina ya horror unayoifikiria. Kama ni biashara basi ilitakiwa ufanye wakati uko kazini ili hata ukistaafu ni kitendo cha kuendelea tu. Sababu mara nyingi kuanza biashara yoyote ile kupoteza kila kitu ni lazima ili kujifunza na wastaafu wengi huishia wakavu namna hiyo.
Nisikutishe bure mzee, kama una mwanao mkubwa anayejitambua na unayemuamini, mpe robo ya hizo pesa afanye biashara physical(kununua na kuuza) wewe uwe msimamizi au watakuchanganya wakuibie, pesa nyingine iweke kama backup. Alafu kuwa makini na kuomba ushauri mitandaoni, wengi wanaandika tu bila kufikiria na wala sio wafanya biashara, wengi matapeli, ushauri wa biashara omba wafanya biashara unaowajua. Pia kuwa makini na biashara za kuwekeza, mitaani na hasa mitandaoni, matapeli wamejaa kila kona.
Kuna daktari amestaafu kutoka muhimbili nilimkuta anauza mayai kwenye kiduka-genge. Hivyo usitegemee vikubwa sana.