Ushauri: Tumia 500,000 kwa mwezi X 12= 6,000,000 kwa Mwaka, Nadhani now una umri 61+15=76
6,000,000 X 15= 90,000,000.
Hiyo pesa utatumia kwa maika 15 bila stress, Ikiisha iyo ndo unaanza kutumia ile iliyokua inaingia mwisho wa mwezi uliyo iacha kwa miaka 15,
Hapo maisha yako yatakua marefu mkuu, umri huo hauhitaji stress, Biashara tuachie sisi coz kilichonikuta mimi kwenye biashara, ingekua wew ungekua ushakufa kwa presha, its more than 10M nimepata loss, hapa najipang upya kuanza tena biashara.
Huo ushauri nikama ushajenga, unausafiri mzuri, nyumbani hakikisha unamifugo rahisi kama kuku, pia unashamba la mazao ya kudumu, na shamba moja la mazao ya chakula, hivyo vitu vitakufanya uwe na kazi kila uamkapo asubuh utapanga ratiba yako uanze na kipi.
NB:Kama hujawai fanya biashara Relax mzee wangu.
Huku Pwani vijijini wazee wanaishi miaka mingi kwa sababu hawaumizi vichwa kuwa na vitu vikubwa ambavyo tunaviona kwenye social media, kila jambo lina muda wake, acha tamaa.
Mwisho kabisa tafuta crue yako baada ya shughuli zako ukipumzika, hapa ni bora uwe na watu wa ibada, kama mkristo kundi hilo lipo kanisani shiriki ibada then rudi home, kama islamic nenda msikitini baada ya swala kula kashata na chai, then rudi home.