Baada ya Dr. Slaa kuzungumza, Mbowe kufunguka

Baada ya Dr. Slaa kuzungumza, Mbowe kufunguka

Dr slaa hawezi kuwa amejivunjia heshima
Dr kanyoosha maelezo vizuri the kama mbowe, lisu na Luwasa. Wana lolote la kuongea waite press conference wajibu hoja kwa mantiki na sio kwa jazba
Watu wanapigwa na wake zao na inabaki kama story yakusadikika itakiwa kulala kwenye gari jibuni hoja sio kashfa
 
Dr slaa kiukweli ameongea kwa uchungu na hisia kali, watanzania tuitendee haki nchi yetu, tumpe kura magufuli, hana kashfa nzito kama za lowassa, nawaomba sana tusiikomoe nchi yetu, walibya leo hii wanajuta, walidanganywa hivihivi, utajiri na amani yao yote imetoweka, wanamkumbuka gadafi wao and it is too late

Kwa nini tusimpe mama Anna ambaye hana kashfa kabisa?
 
Dr slaa kiukweli ameongea kwa uchungu na hisia kali, watanzania tuitendee haki nchi yetu, tumpe kura magufuli, hana kashfa nzito kama za lowassa, nawaomba sana tusiikomoe nchi yetu, walibya leo hii wanajuta, walidanganywa hivihivi, utajiri na amani yao yote imetoweka, wanamkumbuka gadafi wao and it is too late
Wanasiasa hawaamiki hivyo bandika bandua inawahusu,sio sawa kuongozwa na chama kimoja kwa muda mrefu kiasi matokeo yake wanabweta na kuifanya nchi yao HAKUNA NAMNA!
 
Dr slaa kiukweli ameongea kwa uchungu na hisia kali, watanzania tuitendee haki nchi yetu, tumpe kura magufuli, hana kashfa nzito kama za lowassa, nawaomba sana tusiikomoe nchi yetu, walibya leo hii wanajuta, walidanganywa hivihivi, utajiri na amani yao yote imetoweka, wanamkumbuka gadafi wao and it is too late

Watu ka nyie mnaudhi sana basi tu
 
Alinda naomba nitafute posta kuna sehemu wanauza mihogo na maharage tule tupate nguvu tukalikomboe taifa.

11924909_988851627823597_4450057012622236879_n.jpg
 
Tulimwona Lipumba, aliuza magazeti kwa siku moja akapotea, Jana tumemwona Slaa naye atapita. Inaonekana bado hajajua kiwa wananchi hawana ugomvi na mtu bali wana ugomvi ccm kwa hiyo yeyote atakayekuja kuiondoa ccm madarakani lazima awe rafiki yetu tu.
Viva Lowassa
Viva Ukawa
Lowassa tutaendelea kukuombea ili wafitini wako wote waamini kiwa nchi hii sio ya ccm peke yake. Si wametuita sisi ni malofa ma wapumbavu, basi watajua lofa ni nani.

sema Ukawa usitusemee watanzania wote!sisi wengine tunayafikiria maisha baada ya uchaguzi pia yatakuwaje,kwa hiyo tunataka mabadiliko bora na sio bora mabadiliko.
 
Mnaulizwa mnashindwa kujibu. Mnataka kuing'oa CCM ili iweje? Sote tunajua matatizo hebu tupeni suluhisho. Hamna! Mnasema Lowassa. Kisha mnazidi kukatisha tamaa kudai hata akiwa fisadi, mchafu, mgonjwa na spana mkononi si tunataka mabadiliko. Nauliza tena kumwingiza Lowassa Ikulu maisha yako yatabadilika kivipi? Jibu huna. Watakaopata mabadiliko ni Lowassa na ex-CCM buddies na labda akina Chenge atawakumbuka! Wewe utaendelea na matatizo yako kama si kuzidi. Huyu hafai kabisa!
Kwa hiyo ccm ikiendelea madarakani ndio maisha yangu yatakuwa bora!?? Lazima kuwepo mabadiliko siwezi baki na ccm miaka nenda rudi
 
Nini kipya kimezungumzwa na Slaa? kimaantiki alimkubali Mh Lowasa.. eti masharti yke hayajatekelezwa. sasa kama yangetekelezwa maana yake hayo anayosema yasingekuwepo.. masharti hayo hayakuhusu richmond, yanahusu kwamaba aje na watu kutoka ccm aliyotaka yeye na ataje majina yao (Slaa). Na kwa kuwa hakutekeleza hayo masharti basi slaa amekimbia. Kumbe ugomvi na Lowassa mpaka anajichimbia nuymbani kwako ilikuwa ni hayo masharti sasa hayo mengine yameongezwa na akina Mwakyembe. .. Sidhani kama kuna mashika hapa watanzania tukianza kutafutana hivyo hakuna atakayestahili.... Hivi Mangufuli akichambuliwa kwa hasara alizoleta kwenye taifa hili atatosha kweli?

Ndio tunataka Magufuri na yeye achambuliwe kwa hoja zenye ushahidi ili watu wenye akili timamu tusioongozwa na mihemko tuwapime kwa madhambi yao na mazuri yao.
Tuletewe maasi ya Magufuri na ya Lowassa ili tuone wapi uzito umezidi
 
Slaa alikuwa Mgombea 2010...alikuwa na Nondo ya kumshughulikia Lowassa na JK kwa nguvu zote ETI akaamua kukaa kimya !!!!???.. Dr Slaa amekuja kutoka SA na Ndege ya Kukodi, nani kamkodia hiyo ndege? Millioni 500 alizohongwa eti aka kata ilikuwaje akakaa kimya kwa muda wote hadi jana? Kukaa kwake kimya hakuvunja sharia za nchi? Kuwatuhumu Maaskofu bila Ushahidi ni sawa kisheria?
Maaskofu wakane tuhuma ili Dr aje na ushahidi wake. Bora alivyoongea sababu watanzania tulitaka kumsikia
 
Nini kipya kimezungumzwa na Slaa? kimaantiki alimkubali Mh Lowasa.. eti masharti yke hayajatekelezwa. sasa kama yangetekelezwa maana yake hayo anayosema yasingekuwepo.. masharti hayo hayakuhusu richmond, yanahusu kwamaba aje na watu kutoka ccm aliyotaka yeye na ataje majina yao (Slaa). Na kwa kuwa hakutekeleza hayo masharti basi slaa amekimbia. Kumbe ugomvi na Lowassa mpaka anajichimbia nuymbani kwako ilikuwa ni hayo masharti sasa hayo mengine yameongezwa na akina Mwakyembe. .. Sidhani kama kuna mashika hapa watanzania tukianza kutafutana hivyo hakuna atakayestahili.... Hivi Mangufuli akichambuliwa kwa hasara alizoleta kwenye taifa hili atatosha kweli?

Dr atakuwa amekatiwa pension yake kwa shinikizo la madame. Siyo bure.

Alichotakiwa kutueleza ni nini kimemtoa CDM ..... Sasa mambo ya Sumaye yamekujaje wakati Sumaye alijiunga baada ya yeye kujiuzulu!? Labda itakuwa no kazi ya kile Kitengo!!
 
KWAHERI DR.SLAA SISI TUNASONGA MBELE.

Na Nicholaus Ngowi

1/9/2015

Unapotaka kueleza juu ya siasa za Tanzania hasa katika mfumo wa vyama huwezi kuacha kumzungumzia Dr.Wilbroad Peter Slaa ambaye amekuwa katibu mkuu wa CHADEMA kwa zaidi ya muongo mmoja.

Kwa kiasi kikubwa alijitahidi kuijenga CHADEMA imara ambayo imekuwa tumaini la watanzania kama chama mbadala na chama kikuu cha upinzani nchini.

Ni mtu aliyekitumikia chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA kwa uaminifu mkubwa na kwa mafanikio makubwa sana. Pamoja na uaminifu wake alifanya kazi kwa bidii kubwa na kwa kujituma.

Pamoja na mazuri haya ya Dr.Slaa kwa upande wangu Dr. Slaa amekuwa mwalimu wangu wa siasa hasa siasa za mabadiko zinazoegemea kujitoa na kujituma kwa ajili ya manufaa ya umma na kuipigania CHADEMA hata siku ambayo yeye na hawatakuwepo.

Kwangu Dr. Slaa atabaki kuwa mwalimu wangu wa siasa na nitabaki kumuheshimu kwa kazi kubwa aliyoifanya kuijenga CHADEMA chama ambacho kinaenda kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu chini ya Edward Ngoyai Lowasa.

Dr. Slaa Leo ametangaza rasmi kuachana na CHADEMA na pia kuachana rasmi na siasa za vyama vya siasa na kusema kuwa atawasaidia watanzania kwa namna nyingine.

Kipekee ninayaheshimu maamuzi ya Dr. Slaa kwani ni haki yake ya kikatiba kwa mujibu katiba yetu inayotoa fursa kujiunga ama kuchangamana na kundi au taasisi yoyote alimradi havunji katiba.

Dr. Slaa ambaye ametumia jumla ya saa moja na dakika thelathini na nne kueleza yale aliyotaka kuyaeleza ametumia muda mwingi kumponda mgombea urais wa CHADEMA na UKAWA Edward Ngoyai Lowasa.

Katika kueleza amesema kuwa licha ya wajumbe wengi wa kamati kuu kuunga mkono swala la Lowasa kuja CHADEMA yeye hakukubaliana nao na aliweka msimamo kuwa ili Lowasa aje ni lazima afanye mambo yafuatayo, mosi ni lazima atangaze kujitoa ccm, pili ni lazima atangaze anakwenda chama gani, na tatu ni lazima ajisafishe tuhuma zinazomkabili tofauti na hapo uchafu wake ungekuja CHADEMA . Hapa Dr. Slaa amenipa ukakasi kidogo na sitaki kuamini kwamba Dr. haijui katiba ya CHADEMA toleo la 2006. katika katiba ya CHADEMA hakuna mahali penye vigezo alivyotoa Dr. Slaa labda kama anataka yeye ndiye awe katiba ya chama chetu. Swali ninalopata hapa ni je Dr.Slaa alifanya hayo alipotoka ccm 1995 kuja CHADEMA?

Dr.Slaa anasema kuwa angekubaliana na ujio wa Lowasa endapo lowasa angekuwa mtaji yaani "aset" akiwa ana maana kuwa anakuja na watu wengi. Hivi ni nani asiyejua umati aliokuja nao lowasaa?

Anasema aliambiwa wangekuja viongozi wa CCM serious yaani wabunge 50, wenyeviti wa ccm wa mikoa 22, wenyeviti wa ccm wa wilaya 88. Nashindwa kuelewa kuwa kura za hao aliowataka Dr. Slaa na za mamilioni ya watanzania wanaomuunga mkono Lowasa zipi nyingi?

Dr. Slaa anasema waliokuja CHADEMA kutoka CCM ni makapi wimbo anaouimba NAPE. Hivi ni kweli kuwa alipotoka CCM 1995 na yeye alikuwa kapi?

Dr. Slaa alinifundisha kuheshimu maamuzi ya wengi ndani ya vikao kama moja ya msingi wa kidemocrasia. Pamoja na yeye kunifundisha hivyo ameshindwa kuheshimu maamuzi ya kamati kuu juu ya kumpokea Lowasa. Hivi Dr. Slaa ana nguvu kuliko kamati kuu?

Dr. Slaa anatuambia kuwa anshindia mihogo kwani mshahara wake anaolipwa na CHADEMA wa zaidi milioni 7 kwa mwezi anautumia mchumba wake Josephine kufanya shughuli za ujenzi wa CHADEMA. Hebu Dr. Slaa atuambie Josephine amefanya wapi kazi ya kuijenga CHADEMA? Na kama ni kweli anashindia mihogo amepata wapi fedha za kuandaa press conference Serena hotel na kurushwa live kwa gharama ya zaidi ya million 85?

Dr.unatuambia kuwa hoja sio urais hoja ni makapi toka CCM akiwemo Lowasa. Hivi si Dr.slaa alienda mwanza kuwapokea Ester Bulaya na James Lembeli? Iweje alienda kupokea makapi?

Dr.Slaa ametuambia kuwa amesoma theolojia na ni padri wa kanisa katoliki. Hivi jambazi au mwizi anapotubu huwa hasamehewi?

Sitaki kuendelea kusema mengi ila ukweli ni kwamba Dr.Slaa amesaliti harakati za mabadiliko kwa kiwango kiwango kikubwa.

Ninajua kwa kiasi kikubwa alijiandaa kuwa raisi ila baada ya CHADEMA kubadilishia gia angani naona ndoto zake zikapotea na hasira zake ni kutaka kumchafua mgombea wetu ili tukose wote.

Ili kufanikisha alichokisema ameshirikiana vya kutosha na chama tawala Pamoja na tiss na ndio maana kwa mara ya kwanza ameitumia TBC aliyoitukana muda wote wa siasa na mkutano ule kwa kiasi kikubwa umesimamiwa na tiss na baada ya mkutano kuisha zikafuata nyimbo za ccm.

Hakuna haja ya kuumia wala kupoteza muda kumjadili Dr.Slaa kikubwa ni kuendelea kuyatafuta mabadiliko ya nchi yetu.

Pamoja na Dr Slaa kuachana na Kanisa bado injili iliendelea hata leo kasaliti harakati mapambano yataendelea.

KWAHERI DR.SLAA SISI TUNASONGA MBELE.
 
Dr slaa kiukweli ameongea kwa uchungu na hisia kali, watanzania tuitendee haki nchi yetu, tumpe kura magufuli, hana kashfa nzito kama za lowassa, nawaomba sana tusiikomoe nchi yetu, walibya leo hii wanajuta, walidanganywa hivihivi, utajiri na amani yao yote
imetoweka, wanamkumbuka gadafi wao and it is too late

Tena ukome kutaja Libya kwenye siasa zetu Libya walifanya mapinduzi sisi tunafanya uchaguzi. Mbona hayo ya Libya hayakutokea Zambia, Malawi , Kenya na kwingineko? Km yatatokea ya Libya uchaguzi wa nn ss? Kubafu
 
i think you are not too Bright! CHADEMA wako makini sana na walijua tangu mwanzo kwamba Dr. ataongea tu..lazima wanazo facts za kujibu. Tayari Tundu Lisu keshajibu hizo tuhuma. Acha CHADEMA isonge..ilete ukombozi. CCM oyeee!

Ahahahaha ww empty set kabisa... Sasa huyo Lisu ndo kaongea nn?... Afu unajiita bright...
 
Itabid tuseme msemo mmoja wa marekani **whether he will bring development or not we will choose obama to show the world that America is for everyone.,na sis tunasema,whether he will bring development or not we will choose LOWASA from UKAWA to show the world that Tanzania is for every one, not ccm only. Tuma ujumbe huu kwa wadau wasiopungua hamsini ili kuleta mabadiliko ya kweli. Lowasa oyee,,

Swadakta hapa hakuna kurudi nyuma,kama Slaa anafikili ameharibu amenoa chagua Lowasa kwa mabadiliko, Tanzania si ya CCM ni ya watanzania
 
Bora tone la mavi kwenye litre 20 za maji safi kuliko tone la maji safi kwenye litre 20 za maji ya mtaroni. If u kno what i mean.


ENL 2015 the next..............
Hate it or Love it, the underdogs get to the top.
 
Na wakithubutu kujibizana na Dr. Slaa ataweka mambo yote hadhalani na issue itaingia mchanga huku ccm ikipeta ki ulaini kabisa.

Uzur wa huyu mzee huwa anaongea with vivid evidence.. Tofaut na wao wanafyatua tu lolote linalokuja mdomoni.
 
Back
Top Bottom