Atumia mtandao wa Facebook kuwalawiti wanafunzi wenzake

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,149
Atumia mtandao wa Facebook kuwalawiti wanafunzi wenzake


Anthony Stancl Tuesday, February 10, 2009 8:21 AM
Mwanafunzi mmoja aliyejifanya msichana anayetafuta mpenzi katika mtandao wa Facebook na kuomba picha za utupu za wanafunzi wenzake na baadae kuwatishia kuzisambaza shule nzima picha hizo wasipokubali awalawiti amekamatwa baada ya kuwalawiti wavulana 7
Taarifa zilizotolewa zilisema kwamba Anthony Stancl mwwenye umri wa miaka 18 alijifanya msichana katika mtandao wa Facebook na kujaribu kutumia kila njia kuwavutia wanafunzi wenzake ili wamtumie picha zao za utupu na baadae kuwatishia wanafunzi hao kuzianika picha zao shule nzima iwapo hawatakubali matakwa yake.

Stancl mkazi wa New Berlin Wisconsinite, nchini Marekani amekamatwa na anashtakiwa kwa makosa ya kujifanya msichana,kubaka, kuwatishia wanafunzi wenzake wa kiume na kumiliki picha za ngono za watoto.

Stancl alianza mchezo wake huo mwaka 2007 baada ya kujisajili kwa jina la kike katika mtandao wa Facebook akijiita Emily na kuweka picha nzuri za kike akijifanya yeye ni msichana aliyekuwa akitafuta mpenzi.

Kwa mujibu wa polisi, baada ya kupata picha hizo za wanafunzi wenzake wavulana Stancl aliwatishia kuzisambaza picha hizo shule nzima na kuwataka wafanye naye mapenzi.

Stancl alifanikiwa kupata picha za utupu za wanafunzi wenzake 31 na alifanikiwa kuwalawiti wavulana saba kati yao.

Inasemekana Stancl alifanya uovu wake huo kwenye mabafu ya shule, sehemu za kuegesha magari na wengine alidiriki kwenda majumbani mwao na kuwafanyia uovu wake huo.

Mtandao wa Facebook umewataka wanachama wake wawe makini na marafiki wanaojiunga nao kwenye mtandao huo na imeahidi kutafuta njia za kuzuia matatizo kama hayo yasitokee tena baadae.
 
Atumia mtandao wa Facebook kuwalawiti wanafunzi wenzake


Anthony Stancl Tuesday, February 10, 2009 8:21 AM
Mwanafunzi mmoja aliyejifanya msichana anayetafuta mpenzi katika mtandao wa Facebook na kuomba picha za utupu za wanafunzi wenzake na baadae kuwatishia kuzisambaza shule nzima picha hizo wasipokubali awalawiti amekamatwa baada ya kuwalawiti wavulana 7
Taarifa zilizotolewa zilisema kwamba Anthony Stancl mwwenye umri wa miaka 18 alijifanya msichana katika mtandao wa Facebook na kujaribu kutumia kila njia kuwavutia wanafunzi wenzake ili wamtumie picha zao za utupu na baadae kuwatishia wanafunzi hao kuzianika picha zao shule nzima iwapo hawatakubali matakwa yake.

Stancl mkazi wa New Berlin Wisconsinite, nchini Marekani amekamatwa na anashtakiwa kwa makosa ya kujifanya msichana,kubaka, kuwatishia wanafunzi wenzake wa kiume na kumiliki picha za ngono za watoto.

Stancl alianza mchezo wake huo mwaka 2007 baada ya kujisajili kwa jina la kike katika mtandao wa Facebook akijiita Emily na kuweka picha nzuri za kike akijifanya yeye ni msichana aliyekuwa akitafuta mpenzi.

Kwa mujibu wa polisi, baada ya kupata picha hizo za wanafunzi wenzake wavulana Stancl aliwatishia kuzisambaza picha hizo shule nzima na kuwataka wafanye naye mapenzi.

Stancl alifanikiwa kupata picha za utupu za wanafunzi wenzake 31 na alifanikiwa kuwalawiti wavulana saba kati yao.

Inasemekana Stancl alifanya uovu wake huo kwenye mabafu ya shule, sehemu za kuegesha magari na wengine alidiriki kwenda majumbani mwao na kuwafanyia uovu wake huo.

Mtandao wa Facebook umewataka wanachama wake wawe makini na marafiki wanaojiunga nao kwenye mtandao huo na imeahidi kutafuta njia za kuzuia matatizo kama hayo yasitokee tena baadae.

...na wao walitaka tu kulawitiwa,...:( mtu anaona bora alawitiwe kuliko kusambazwa picha yake ya utupu? mwehu nini huyo?
 
...na wao walitaka tu kulawitiwa,...:(


Eti kisa picha tuu, pic zenyewe ziko kwenye facebook inwhich they dont allow any explicit material anyway , otherwise facebook themselfves would have them down as of immediately
Y worry for the school to know???? hence almost 99% of the kids at school have internet access on phones, home, school labs.....! I dont get it :confused:
 
...na wao walitaka tu kulawitiwa,...:( mtu anaona bora alawitiwe kuliko kusambazwa picha yake ya utupu? mwehu nini huyo?

Ni hapo sasa...! Aah! Siajabu ukakuta hao walio lawitiwa wana chembe chembe za ushoga...!

Kama ni picha tu na azianike... zikikauka si zita anuliwa...!? Tatizo liko wapi!?

Kwanza kwa nchi za Ulaya na Marekani kuonekana ukiwa mtupu wal si jambo la ajabu. Otherwise hizo picha nazo zilikuwa zimekaa kishoga shoga!
 
Ni hapo sasa...! Aah! Siajabu ukakuta hao walio lawitiwa wana chembe chembe za ushoga...!

Kama ni picha tu na azianike... zikikauka si zita anuliwa...!? Tatizo liko wapi!?

Kwanza kwa nchi za Ulaya na Marekani kuonekana ukiwa mtupu wal si jambo la ajabu. Otherwise hizo picha nazo zilikuwa zimekaa kishoga shoga!

Hamna mbona ni ajabu usione kwenye mapicha lakini na wao wanatazama pia ,demu akikatisha au akivaa viguo vya kuonyesha maungo wanamtazama na kurusha rusha maneno, ndio maana kunaongoza kwa ubakaji.
 
Kaaaazi kwelikweli kwani huo ndio wehu na uendawazimu wa watu weupe. Yaani heri kulawitiwa kwani itakuwa siri baina yenu kuliko picha zako za uchi ziwe mtaani, hii ni ajabu na kweli
 
Back
Top Bottom