Atheists wanaweza kuwa wagonjwa wa akili?

Atheists wanaweza kuwa wagonjwa wa akili?



LIKUD hizi research zako unafanyiaga wapi? na unatumia methodology gani?
 
  • Kitanda vs Mwanadamu: Tunajua kitanda kina fundi kwa sababu tuna ushahidi wa viwanda, zana, na mafundi sio kwa sababu tu ni complex. Huwezi kuchukua sheria ya vitu vya kiwandani ukaihamisha moja kwa moja kwenye viumbe hai bila ushahidi.
  • Complexity ≠ Design: Mfumo tata unaweza kujitengeneza kupitia mchakato wa asili. Mfano: Snowflake na kristo za chumvi zina maumbo tata lakini zinatengenezwa na physics/chemistry bila fundi. Evolution ina zana za ziada ambazo kitanda hakina: replication, mutation, selection, na miaka bilioni kadhaa.
  • Natural Selection si Bahati: Random mutation inatoa mabadiliko, lakini mazingira (natural selection) ndiyo yanayochuja yaliyo bora. Random mutation ni waombaji kazi; mazingira ndiye mhojiaji.
  • Paradox ya Designer: Ukisema "kila kitu complex kinahitaji designer," basi huyo Designer anayeweza kuumba ulimwengu lazima awe na complex zaidi yake na yule zaidi yake anatakiwa kuwa na zaidi yake milele. Basi swali linabaki: Nani alim-design Designer? Ukisema yeye hahitaji designer, tayari umeivunja sheria yako ya kwanza.
  • Hesabu za Kufikirika (99% Probability): Kutoa namba ya asilimia bila data, model, au Bayesian priors ni maoni binafsi yaliyovaa suti ya hesabu.
  • Kosa la 'God of the Gaps': Sayansi kutoshtukia au kutojua chanzo cha kwanza cha uhai haimaanishi jawabu ni "Higher Power". Kusema "sijui" ni kauli ya kisayansi kuliko kujaza pengo kwa kitu kisicho na ushahidi.
 
Back
Top Bottom